1After these things Jesus went away beyond the sea of Galilee (of Tiberias),
1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
2and there was following him a great multitude, because they were seeing his signs that he was doing on the ailing;
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
3and Jesus went up to the mount, and he was there sitting with his disciples,
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
4and the passover was nigh, the feast of the Jews.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
5Jesus then having lifted up [his] eyes and having seen that a great multitude doth come to him, saith unto Philip, `Whence shall we buy loaves, that these may eat?` —
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
6and this he said, trying him, for he himself had known what he was about to do.
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
7Philip answered him, `Two hundred denaries` worth of loaves are not sufficient to them, that each of them may receive some little;`
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
8one of his disciples — Andrew, the brother of Simon Peter — saith to him,
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
9`There is one little lad here who hath five barley loaves, and two fishes, but these — what are they to so many?`
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
10And Jesus said, `Make the men to sit down;` and there was much grass in the place, the men then sat down, in number, as it were, five thousand,
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
11and Jesus took the loaves, and having given thanks he distributed to the disciples, and the disciples to those reclining, in like manner, also of the little fishes as much as they wished.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12And when they were filled, he saith to his disciples, `Gather together the broken pieces that are over, that nothing may be lost;`
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
13they gathered together, therefore, and filled twelve hand-baskets with broken pieces, from the five barley loaves that were over to those having eaten.
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
14The men, then, having seen the sign that Jesus did, said — `This is truly the Prophet, who is coming to the world;`
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
15Jesus, therefore, having known that they are about to come, and to take him by force that they may make him king, retired again to the mountain himself alone.
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
16And when evening came, his disciples went down to the sea,
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
17and having entered into the boat, they were going over the sea to Capernaum, and darkness had already come, and Jesus had not come unto them,
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
18the sea also — a great wind blowing — was being raised,
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19having pushed onwards, therefore, about twenty-five or thirty furlongs, they behold Jesus walking on the sea, and coming nigh to the boat, and they were afraid;
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
20and he saith to them, `I am [he], be not afraid;`
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
21they were willing then to receive him into the boat, and immediately the boat came unto the land to which they were going.
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
22On the morrow, the multitude that was standing on the other side of the sea, having seen that there was no other little boat there except one — that into which his disciples entered — and that Jesus went not in with his disciples into the little boat, but his disciples went away alone,
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
23(and other little boats came from Tiberias, nigh the place where they did eat the bread, the Lord having given thanks),
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
24when therefore the multitude saw that Jesus is not there, nor his disciples, they also themselves did enter into the boats, and came to Capernaum seeking Jesus;
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
25and having found him on the other side of the sea, they said to him, `Rabbi, when hast thou come hither?`
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
26Jesus answered them and said, `Verily, verily, I say to you, Ye seek me, not because ye saw signs, but because ye did eat of the loaves, and were satisfied;
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27work not for the food that is perishing, but for the food that is remaining to life age-during, which the Son of Man will give to you, for him did the Father seal — [even] God.`
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
28They said therefore unto him, `What may we do that we may work the works of God?`
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
29Jesus answered and said to them, `This is the work of God, that ye may believe in him whom He did send.`
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
30They said therefore to him, `What sign, then, dost thou, that we may see and may believe thee? what dost thou work?
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31our fathers the manna did eat in the wilderness, according as it is having been written, Bread out of the heaven He gave them to eat.`
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
32Jesus, therefore, said to them, `Verily, verily, I say to you, Moses did not give you the bread out of the heaven; but my Father doth give you the true bread out of the heaven;
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33for the bread of God is that which is coming down out of the heaven, and giving life to the world.`
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
34They said, therefore, unto him, `Sir, always give us this bread.`
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
35And Jesus said to them, `I am the bread of the life; he who is coming unto me may not hunger, and he who is believing in me may not thirst — at any time;
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36but I said to you, that ye also have seen me, and ye believe not;
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37all that the Father doth give to me will come unto me; and him who is coming unto me, I may in no wise cast without,
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38because I have come down out of the heaven, not that I may do my will, but the will of Him who sent me.
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39`And this is the will of the Father who sent me, that all that He hath given to me I may not lose of it, but may raise it up in the last day;
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40and this is the will of Him who sent me, that every one who is beholding the Son, and is believing in him, may have life age-during, and I will raise him up in the last day.`
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
41The Jews, therefore, were murmuring at him, because he said, `I am the bread that came down out of the heaven;`
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
42and they said, `Is not this Jesus, the son of Joseph, whose father and mother we have known? how then saith this one — Out of the heaven I have come down?`
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
43Jesus answered, therefore, and said to them, `Murmur not one with another;
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
44no one is able to come unto me, if the Father who sent me may not draw him, and I will raise him up in the last day;
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
45it is having been written in the prophets, And they shall be all taught of God; every one therefore who heard from the Father, and learned, cometh to me;
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46not that any one hath seen the Father, except he who is from God, he hath seen the Father.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47`Verily, verily, I say to you, He who is believing in me, hath life age-during;
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
48I am the bread of the life;
48Mimi ni mkate wa uzima.
49your fathers did eat the manna in the wilderness, and they died;
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50this is the bread that out of the heaven is coming down, that any one may eat of it, and not die.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51`I am the living bread that came down out of the heaven; if any one may eat of this bread he shall live — to the age; and the bread also that I will give is my flesh, that I will give for the life of the world.`
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
52The Jews, therefore, were striving with one another, saying, `How is this one able to give us [his] flesh to eat?`
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53Jesus, therefore, said to them, `Verily, verily, I say to you, If ye may not eat the flesh of the Son of Man, and may not drink his blood, ye have no life in yourselves;
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54he who is eating my flesh, and is drinking my blood, hath life age-during, and I will raise him up in the last day;
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
55for my flesh truly is food, and my blood truly is drink;
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56he who is eating my flesh, and is drinking my blood, doth remain in me, and I in him.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
57`According as the living Father sent me, and I live because of the Father, he also who is eating me, even that one shall live because of me;
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
58this is the bread that came down out of the heaven; not as your fathers did eat the manna, and died; he who is eating this bread shall live — to the age.`
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
59These things he said in a synagogue, teaching in Capernaum;
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
60many, therefore, of his disciples having heard, said, `This word is hard; who is able to hear it?`
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
61And Jesus having known in himself that his disciples are murmuring about this, said to them, `Doth this stumble you?
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
62if then ye may behold the Son of Man going up where he was before?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
63the spirit it is that is giving life; the flesh doth not profit anything; the sayings that I speak to you are spirit, and they are life;
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
64but there are certain of you who do not believe;` for Jesus had known from the beginning who they are who are not believing, and who is he who will deliver him up,
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
65and he said, `Because of this I have said to you — No one is able to come unto me, if it may not have been given him from my Father.`
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
66From this [time] many of his disciples went away backward, and were no more walking with him,
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
67Jesus, therefore, said to the twelve, `Do ye also wish to go away?`
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
68Simon Peter, therefore, answered him, `Sir, unto whom shall we go? thou hast sayings of life age-during;
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
69and we have believed, and we have known, that thou art the Christ, the Son of the living God.`
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
70Jesus answered them, `Did not I choose you — the twelve? and of you — one is a devil.
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
71And he spake of Judas, Simon`s [son], Iscariot, for he was about to deliver him up, being one of the twelve.
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.