Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

John

7

1And Jesus was walking after these things in Galilee, for he did not wish to walk in Judea, because the Jews were seeking to kill him,
1Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2and the feast of the Jews was nigh — that of tabernacles —
2Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3his brethren, therefore, said unto him, `Remove hence, and go away to Judea, that thy disciples also may behold thy works that thou dost;
3Basi ndugu zake wakamwambia, "Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4for no one in secret doth anything, and himself seeketh to be in public; if thou dost these things — manifest thyself to the world;`
4Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu."
5for not even were his brethren believing in him.
5(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6Jesus, therefore, saith to them, `My time is not yet present, but your time is always ready;
6Basi, Yesu akawaambia, "Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7the world is not able to hate you, but me it doth hate, because I testify concerning it that its works are evil.
7Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8Ye — go ye up to this feast; I do not yet go up to this feast, because my time hath not yet been fulfilled;`
8Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika."
9and saying these things to them, he remained in Galilee.
9Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10And when his brethren went up, then also he himself went up to the feast, not manifestly, but as in secret;
10Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11the Jews, therefore, were seeking him, in the feast, and said, `Where is that one?`
11Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: "Yuko wapi?"
12and there was much murmuring about him among the multitudes, some indeed said — `He is good;` and others said, `No, but he leadeth astray the multitude;`
12Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, "Ni mtu mwema." Wengine walisema, "La! Anawapotosha watu."
13no one, however, was speaking freely about him, through fear of the Jews.
13Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14And it being now the middle of the feast, Jesus went up to the temple, and he was teaching,
14Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15and the Jews were wondering, saying, `How hath this one known letters — not having learned?`
15Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema "Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?"
16Jesus answered them and said, `My teaching is not mine, but His who sent me;
16Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17if any one may will to do His will, he shall know concerning the teaching, whether it is of God, or — I do speak from myself.
17Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18`He who is speaking from himself his own glory doth seek, but he who is seeking the glory of him who sent him, this one is true, and unrighteousness is not in him;
18Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19hath not Moses given you the law? and none of you doth the law; why me do ye seek to kill?`
19Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?"
20The multitude answered and said, `Thou hast a demon, who doth seek to kill thee?`
20Hapo watu wakamjibu, "Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?"
21Jesus answered and said to them, `One work I did, and ye all wonder,
21Yesu akawajibu, "Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22because of this, Moses hath given you the circumcision — not that it is of Moses, but of the fathers — and on a sabbath ye circumcise a man;
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23if a man doth receive circumcision on a sabbath that the law of Moses may not be broken, are ye wroth with me that I made a man all whole on a sabbath?
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24judge not according to appearance, but the righteous judgment judge.`
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki."
25Certain, therefore, of the Jerusalemites said, `Is not this he whom they are seeking to kill?
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, "Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26and, lo, he doth speak freely, and they say nothing to him; did the rulers at all know truly that this is truly the Christ?
26Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27but this one — we have known whence he is; and the Christ, when he doth come, no one doth know whence he is.`
27Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!"
28Jesus cried, therefore, in the temple, teaching and saying, `Ye have both known me, and ye have known whence I am; and I have not come of myself, but He who sent me is true, whom ye have not known;
28Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29and I have known Him, because I am from Him, and He did send me.`
29Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."
30They were seeking, therefore, to seize him, and no one laid the hand on him, because his hour had not yet come,
30Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31and many out of the multitude did believe in him, and said — `The Christ — when he may come — will he do more signs than these that this one did?`
31Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, "Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?"
32The Pharisees heard the multitude murmuring these things concerning him, and the Pharisees and the chief priests sent officers that they may take him;
32Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33Jesus, therefore, said to them, `Yet a little time I am with you, and I go away unto Him who sent me;
33Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34ye will seek me, and ye shall not find; and where I am, ye are not able to come.`
34Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika."
35The Jews, therefore, said among themselves, `Whither is this one about to go that we shall not find him? — to the dispersion of the Greeks is he about to go? and to teach the Greeks;
35Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, "Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36what is this word that he said, Ye will seek me, and ye shall not find? and, Where I am, ye are not able to come?`
36Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?"
37And in the last, the great day of the feast, Jesus stood and cried, saying, `If any one doth thirst, let him come unto me and drink;
37Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, "Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38he who is believing in me, according as the Writing said, Rivers out of his belly shall flow of living water;`
38Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!"
39and this he said of the Spirit, which those believing in him were about to receive; for not yet was the Holy Spirit, because Jesus was not yet glorified.
39(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40Many, therefore out of the multitude, having heard the word, said, `This is truly the Prophet;`
40Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, "Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!"
41others said, `This is the Christ;` and others said, `Why, out of Galilee doth the Christ come?
41Wengine wakasema, "Huyu ndiye Kristo!" Lakini wengine walisema, "Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42Did not the Writing say, that out of the seed of David, and from Bethlehem — the village where David was — the Christ doth come?`
42Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!"
43A division, therefore, arose among the multitude because of him.
43Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44And certain of them were willing to seize him, but no one laid hands on him;
44Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45the officers came, therefore, unto the chief priests and Pharisees, and they said to them, `Wherefore did ye not bring him?`
45Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, "Kwa nini hamkumleta?"
46The officers answered, `Never so spake man — as this man.`
46Walinzi wakawajibu, "Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!"
47The Pharisees, therefore, answered them, `Have ye also been led astray?
47Mafarisayo wakawauliza, "Je, nanyi pia mmedanganyika?
48did any one out of the rulers believe in him? or out of the Pharisees?
48Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49but this multitude, that is not knowing the law, is accursed.`
49Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!"
50Nicodemus saith unto them — he who came by night unto him — being one of them,
50Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51`Doth our law judge the man, if it may not hear from him first, and know what he doth?`
51"Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?"
52They answered and said to him, `Art thou also out of Galilee? search and see, that a prophet out of Galilee hath not risen;`
52Nao wakamjibu, "Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!"
53and each one went on to his house, but Jesus went on to the mount of the Olives.
53Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;