Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Luke

2

1And it came to pass in those days, there went forth a decree from Caesar Augustus, that all the world be enrolled —
1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2this enrollment first came to pass when Cyrenius was governor of Syria —
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3and all were going to be enrolled, each to his proper city,
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4and Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, to Judea, to the city of David, that is called Bethlehem, because of his being of the house and family of David,
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5to enroll himself with Mary his betrothed wife, being with child.
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6And it came to pass, in their being there, the days were fulfilled for her bringing forth,
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7and she brought forth her son — the first-born, and wrapped him up, and laid him down in the manger, because there was not for them a place in the guest-chamber.
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8And there were shepherds in the same region, lodging in the field, and keeping the night-watches over their flock,
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9and lo, a messenger of the Lord stood over them, and the glory of the Lord shone around them, and they feared a great fear.
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10And the messenger said to them, `Fear not, for lo, I bring you good news of great joy, that shall be to all the people —
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11because there was born to you to-day a Saviour — who is Christ the Lord — in the city of David,
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12and this [is] to you the sign: Ye shall find a babe wrapped up, lying in the manger.`
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
13And suddenly there came with the messenger a multitude of the heavenly host, praising God, and saying,
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14`Glory in the highest to God, and upon earth peace, among men — good will.`
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
15And it came to pass, when the messengers were gone away from them to the heavens, that the men, the shepherds, said unto one another, `We may go over indeed unto Bethlehem, and see this thing that hath come to pass, that the Lord did make known to us.`
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
16And they came, having hasted, and found both Mary, and Joseph, and the babe lying in the manger,
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17and having seen, they made known abroad concerning the saying spoken to them concerning the child.
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18And all who heard, did wonder concerning the things spoken by the shepherds unto them;
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19and Mary was preserving all these things, pondering in her heart;
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20and the shepherds turned back, glorifying and praising God, for all those things they heard and saw, as it was spoken unto them.
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21And when eight days were fulfilled to circumcise the child, then was his name called Jesus, having been so called by the messenger before his being conceived in the womb.
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22And when the days of their purification were fulfilled, according to the law of Moses, they brought him up to Jerusalem, to present to the Lord,
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23as it hath been written in the Law of the Lord, — `Every male opening a womb shall be called holy to the Lord,`
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
24and to give a sacrifice, according to that said in the Law of the Lord, `A pair of turtle-doves, or two young pigeons.`
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25And lo, there was a man in Jerusalem, whose name [is] Simeon, and this man is righteous and devout, looking for the comforting of Israel, and the Holy Spirit was upon him,
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26and it hath been divinely told him by the Holy Spirit — not to see death before he may see the Christ of the Lord.
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27And he came in the Spirit to the temple, and in the parents bringing in the child Jesus, for their doing according to the custom of the law regarding him,
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28then he took him in his arms, and blessed God, and he said,
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29`Now Thou dost send away Thy servant, Lord, according to Thy word, in peace,
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30because mine eyes did see Thy salvation,
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31which Thou didst prepare before the face of all the peoples,
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32a light to the uncovering of nations, and the glory of Thy people Israel.`
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
33And Joseph and his mother were wondering at the things spoken concerning him,
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34and Simeon blessed them, and said unto Mary his mother, `Lo, this [one] is set for the falling and rising again of many in Israel, and for a sign spoken against —
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35(and also thine own soul shall a sword pass through) — that the reasonings of many hearts may be revealed.`
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
36And there was Anna, a prophetess, daughter of Phanuel, of the tribe of Asher, she was much advanced in days, having lived with an husband seven years from her virginity,
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37and she [is] a widow of about eighty-four years, who did depart not from the temple, with fasts and supplications serving, night and day,
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38and she, at that hour, having come in, was confessing, likewise, to the Lord, and was speaking concerning him, to all those looking for redemption in Jerusalem.
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39And when they finished all things, according to the Law of the Lord, they turned back to Galilee, to their city Nazareth;
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40and the child grew and was strengthened in spirit, being filled with wisdom, and the grace of God was upon him.
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41And his parents were going yearly to Jerusalem, at the feast of the passover,
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42and when he became twelve years old, they having gone up to Jerusalem, according to the custom of the feast,
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43and having finished the days, in their returning the child Jesus remained behind in Jerusalem, and Joseph and his mother did not know,
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44and, having supposed him to be in the company, they went a day`s journey, and were seeking him among the kindred and among the acquaintances,
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45and not having found him, they turned back to Jerusalem seeking him.
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46And it came to pass, after three days, they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both hearing them and questioning them,
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47and all those hearing him were astonished at his understanding and answers.
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48And, having seen him, they were amazed, and his mother said unto him, `Child, why didst thou thus to us? lo, thy father and I, sorrowing, were seeking thee.`
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
49And he said unto them, `Why [is it] that ye were seeking me? did ye not know that in the things of my Father it behoveth me to be?`
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
50and they did not understand the saying that he spake to them,
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51and he went down with them, and came to Nazareth, and he was subject to them, and his mother was keeping all these sayings in her heart,
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52and Jesus was advancing in wisdom, and in stature, and in favour with God and men.
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.