Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Luke

22

1And the feast of the unleavened food was coming nigh, that is called Passover,
1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2and the chief priests and the scribes were seeking how they may take him up, for they were afraid of the people.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3And the Adversary entered into Judas, who is surnamed Iscariot, being of the number of the twelve,
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4and he, having gone away, spake with the chief priests and the magistrates, how he might deliver him up to them,
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5and they rejoiced, and covenanted to give him money,
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6and he agreed, and was seeking a favourable season to deliver him up to them without tumult.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7And the day of the unleavened food came, in which it was behoving the passover to be sacrificed,
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8and he sent Peter and John, saying, `Having gone on, prepare to us the passover, that we may eat;`
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
9and they said to him, `Where wilt thou that we might prepare?`
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
10And he said to them, `Lo, in your entering into the city, there shall meet you a man, bearing a pitcher of water, follow him to the house where he doth go in,
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11and ye shall say to the master of the house, The Teacher saith to thee, Where is the guest-chamber where the passover with my disciples I may eat?
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12and he shall show you a large upper room furnished, there make ready;`
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
13and they, having gone away, found as he hath said to them, and they made ready the passover.
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14And when the hour come, he reclined (at meat), and the twelve apostles with him,
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15and he said unto them, `With desire I did desire to eat this passover with you before my suffering,
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16for I say to you, that no more may I eat of it till it may be fulfilled in the reign of God.`
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
17And having taken a cup, having given thanks, he said, `Take this and divide to yourselves,
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18for I say to you that I may not drink of the produce of the vine till the reign of God may come.`
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
19And having taken bread, having given thanks, he brake and gave to them, saying, `This is my body, that for you is being given, this do ye — to remembrance of me.`
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
20In like manner, also, the cup after the supping, saying, `This cup [is] the new covenant in my blood, that for you is being poured forth.
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21`But, lo, the hand of him delivering me up [is] with me on the table,
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22and indeed the Son of Man doth go according to what hath been determined; but wo to that man through whom he is being delivered up.`
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
23And they began to reason among themselves, who then of them it may be, who is about to do this thing.
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24And there happened also a strife among them — who of them is accounted to be greater.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25And he said to them, `The kings of the nations do exercise lordship over them, and those exercising authority upon them are called benefactors;
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26but ye [are] not so, but he who is greater among you — let him be as the younger; and he who is leading, as he who is ministering;
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27for who is greater? he who is reclining (at meat), or he who is ministering? is it not he who is reclining (at meat)? and I — I am in your midst as he who is ministering.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28`And ye — ye are those who have remained with me in my temptations,
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29and I appoint to you, as my Father did appoint to me, a kingdom,
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30that ye may eat and may drink at my table, in my kingdom, and may sit on thrones, judging the twelve tribes of Israel.`
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31And the Lord said, `Simon, Simon, lo, the Adversary did ask you for himself to sift as the wheat,
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32and I besought for thee, that thy faith may not fail; and thou, when thou didst turn, strengthen thy brethren.`
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
33And he said to him, `Sir, with thee I am ready both to prison and to death to go;`
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
34and he said, `I say to thee, Peter, a cock shall not crow to-day, before thrice thou mayest disown knowing me.`
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
35And he said to them, `When I sent you without bag, and scrip, and sandals, did ye lack anything?` and they said, `Nothing.`
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
36Then said he to them, `But, now, he who is having a bag, let him take [it] up, and in like manner also a scrip; and he who is not having, let him sell his garment, and buy a sword,
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37for I say to you, that yet this that hath been written it behoveth to be fulfilled in me: And with lawless ones he was reckoned, for also the things concerning me have an end.`
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
38And they said, `Sir, lo, here [are] two swords;` and he said to them, `It is sufficient.`
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
39And having gone forth, he went on, according to custom, to the mount of the Olives, and his disciples also followed him,
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40and having come to the place, he said to them, `Pray ye not to enter into temptation.`
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
41And he was withdrawn from them, as it were a stone`s cast, and having fallen on the knees he was praying,
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42saying, `Father, if Thou be counselling to make this cup pass from me —; but, not my will, but Thine be done.` —
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
43And there appeared to him a messenger from heaven strengthening him;
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44and having been in agony, he was more earnestly praying, and his sweat became, as it were, great drops of blood falling upon the ground.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45And having risen up from the prayer, having come unto the disciples, he found them sleeping from the sorrow,
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46and he said to them, `Why do ye sleep? having risen, pray that ye may not enter into temptation.`
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
47And while he is speaking, lo, a multitude, and he who is called Judas, one of the twelve, was coming before them, and he came nigh to Jesus to kiss him,
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48and Jesus said to him, `Judas, with a kiss the Son of Man dost thou deliver up?`
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
49And those about him, having seen what was about to be, said to him, `Sir, shall we smite with a sword?`
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
50And a certain one of them smote the servant of the chief priest, and took off his right ear,
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51and Jesus answering said, `Suffer ye thus far,` and having touched his ear, he healed him.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52And Jesus said to those having come upon him — chief priests, and magistrates of the temple, and elders — `As upon a robber have ye come forth, with swords and sticks?
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53while daily I was with you in the temple, ye did stretch forth no hands against me; but this is your hour and the power of the darkness.`
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
54And having taken him, they led and brought him to the house of the chief priest. And Peter was following afar off,
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55and they having kindled a fire in the midst of the court, and having sat down together, Peter was sitting in the midst of them,
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56and a certain maid having seen him sitting at the light, and having earnestly looked at him, she said, `And this one was with him!`
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
57and he disowned him, saying, `Woman, I have not known him.`
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
58And after a little, another having seen him, said, `And thou art of them!` and Peter said, `Man, I am not.`
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
59And one hour, as it were, having intervened, a certain other was confidently affirming, saying, `Of a truth this one also was with him, for he is also a Galilean;`
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
60and Peter said, `Man, I have not known what thou sayest;` and presently, while he is speaking, a cock crew.
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61And the Lord having turned did look on Peter, and Peter remembered the word of the Lord, how he said to him — `Before a cock shall crow, thou mayest disown me thrice;`
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
62and Peter having gone without, wept bitterly.
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
63And the men who were holding Jesus were mocking him, beating [him];
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64and having blindfolded him, they were striking him on the face, and were questioning him, saying, `Prophesy who he is who smote thee?`
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
65and many other things, speaking evilly, they spake in regard to him.
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66And when it became day there was gathered together the eldership of the people, chief priests also, and scribes, and they led him up to their own sanhedrim,
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67saying, `If thou be the Christ, tell us.` And he said to them, `If I may tell you, ye will not believe;
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68and if I also question [you], ye will not answer me or send me away;
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69henceforth, there shall be the Son of Man sitting on the right hand of the power of God.`
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
70And they all said, `Thou, then, art the Son of God?` and he said unto them, `Ye say [it], because I am;`
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
71and they said, `What need yet have we of testimony? for we ourselves did hear [it] from his mouth.`
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."