1At that time did Jesus go on the sabbaths through the corn, and his disciples were hungry, and they began to pluck ears, and to eat,
1Wakati huo, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano siku ya Sabato. Basi, wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakala punje zake.
2and the Pharisees having seen, said to him, `Lo, thy disciples do that which it is not lawful to do on a sabbath.`
2Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, "Tazama, wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato."
3And he said to them, `Did ye not read what David did, when he was hungry, himself and those with him —
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4how he went into the house of God, and the loaves of the presentation did eat, which it is not lawful to him to eat, nor to those with him, except to the priests alone?
4Yeye aliingia katika Nyumba ya Mungu pamoja na wenzake, wakala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Yeye wala hao wenzake hawakuruhusiwa kula mikate hiyo isipokuwa tu makuhani peke yao.
5`Or did ye not read in the Law, that on the sabbaths the priests in the temple do profane the sabbath, and are blameless?
5Au je, hamjasoma katika Sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani huivunja Sheria Hekaluni, lakini hawafikiriwi kuwa na hatia?
6and I say to you, that a greater than the temple is here;
6Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko Hekalu.
7and if ye had known what is: Kindness I will, and not sacrifice — ye had not condemned the blameless,
7Kama tu mngejua maana ya maneno haya: Nataka huruma wala si dhabihu, hamngewahukumu watu wasio na hatia.
8for the son of man is lord even of the sabbath.`
8Maana Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
9And having departed thence, he went to their synagogue,
9Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.
10and lo, there was a man having the hand withered, and they questioned him, saying, `Is it lawful to heal on the sabbaths?` that they might accuse him.
10Kulikuwa na mtu mmoja mwenye mkono uliopooza. Basi, watu wakamwuliza Yesu, "Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?" Walimwuliza hivyo wapate kisa cha kumshtaki.
11And he said to them, `What man shall be of you, who shall have one sheep, and if this may fall on the sabbaths into a ditch, will not lay hold on it and raise [it]?
11Lakini Yesu akawaambia, "Tuseme mmoja wenu ana kondoo wake ambaye ametumbukia shimoni; je, hatamshika na kumtoa humo siku ya Sabato?
12How much better, therefore, is a man than a sheep? — so that it is lawful on the sabbaths to do good.`
12Mtu ana thamani kuliko kondoo! Basi, ni halali kutenda mema siku ya Sabato."
13Then saith he to the man, `Stretch forth thy hand,` and he stretched [it] forth, and it was restored whole as the other.
13Kisha akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Akaunyosha, nao ukawa mzima kabisa kama ule mwingine.
14And the Pharisees having gone forth, held a consultation against him, how they might destroy him,
14Basi, Mafarisayo wakatoka nje, wakashauriana jinsi watakavyomwangamiza Yesu.
15and Jesus having known, withdrew thence, and there followed him great multitudes, and he healed them all,
15Lakini Yesu alipojua jambo hilo, akatoka mahali pale. Watu wengi walimfuata, akawaponya wagonjwa wote,
16and did charge them that they might not make him manifest,
16akawaamuru wasiwaambie watu habari zake,
17that it might be fulfilled that was spoken through Isaiah the prophet, saying,
17ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie:
18`Lo, My servant, whom I did choose, My beloved, in whom My soul did delight, I will put My Spirit upon him, and judgment to the nations he shall declare,
18"Hapa ni mtumishi wangu niliyemteua, mpendwa wangu anipendezaye moyoni. Nitaiweka Roho yangu juu yake, naye atatangaza hukumu yangu kwa mataifa yote.
19he shall not strive nor cry, nor shall any hear in the broad places his voice,
19Hatakuwa na ubishi wala kupiga kelele, wala sauti yake haitasikika barabarani.
20a bruised reed he shall not break, and smoking flax he shall not quench, till he may put forth judgment to victory,
20Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi ufukao moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya hukumu ya haki itawale.
21and in his name shall nations hope.`
21Katika jina lake mataifa yatakuwa na tumaini."
22Then was brought to him a demoniac, blind and dumb, and he healed him, so that the blind and dumb both spake and saw.
22Hapo watu wakamletea Yesu kipofu mmoja ambaye alikuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata, akaweza kusema na kuona.
23And all the multitudes were amazed, and said, `Is this the Son of David?`
23Umati wote wa watu ulishangaa ukasema, "Je, huenda ikawa huyu ndiye Mwana wa Daudi?"
24but the Pharisees having heard, said, `This one doth not cast out demons, except by Beelzeboul, ruler of the demons.`
24Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, wakasema, "Mtu huyu anawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo."
25And Jesus, knowing their thoughts, said to them, `Every kingdom having been divided against itself is desolated, and no city or house having been divided against itself, doth stand,
25Yesu, akiwa anayajua mawazo yao, akawaambia, "Ufalme wowote uliogawanyika makundimakundi yanayopingana, hauwezi kudumu, na mji wowote au jamaa yoyote iliyogawanyika makundimakundi yanayopingana, itaanguka.
26and if the Adversary doth cast out the Adversary, against himself he was divided, how then doth his kingdom stand?
26Ikiwa Shetani anamfukuza Shetani, anajipinga mwenyewe. Basi, ufalme wake utasimamaje?
27`And if I, by Beelzeboul, do cast out the demons, your sons — by whom do they cast out? because of this they — they shall be your judges.
27Ninyi mnasema ati nawafukuza pepo kwa uwezo wa Beelzebuli; je, watoto wenu huwafukuza kwa uwezo wa nani? Kwa sababu hiyo wao ndio watakaowahukumu ninyi.
28`But if I, by the Spirit of God, do cast out the demons, then come already unto you did the reign of God.
28Lakini ikiwa ninawafukuza pepo kwa nguvu ya Roho wa Mungu, basi jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha fika kwenu.
29`Or how is one able to go into the house of the strong man, and to plunder his goods, if first he may not bind the strong man? and then his house he will plunder.
29"Au, anawezaje mtu kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, bila kwanza kumfunga huyo mtu mwenye nguvu? Hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
30`He who is not with me is against me, and he who is not gathering with me, doth scatter.
30"Yeyote asiyejiunga nami, anapingana nami; na yeyote asiyekusanya pamoja nami, hutawanya.
31Because of this I say to you, all sin and evil speaking shall be forgiven to men, but the evil speaking of the Spirit shall not be forgiven to men.
31Kwa sababu hiyo, nawaambieni, watu watasamehewa dhambi na kufuru zao zote, lakini hawatasamehewa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
32And whoever may speak a word against the Son of Man it shall be forgiven to him, but whoever may speak against the Holy Spirit, it shall not be forgiven him, neither in this age, nor in that which is coming.
32Tena, asemaye neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa, lakini yule asemaye neno la kumpinga Roho Mtakatifu, hatasamehewa, wala katika ulimwengu huu, wala katika ulimwengu ujao.
33`Either make the tree good, and its fruit good, or make the tree bad, and its fruit bad, for from the fruit is the tree known.
33"Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake yatakuwa mema; ufanyeni kuwa mbaya na matunda yake yatakuwa mabaya. Mti hujulikana kwa matunda yake.
34`Brood of vipers! how are ye able to speak good things — being evil? for out of the abundance of the heart doth the mouth speak.
34Enyi kizazi cha nyoka! Mnawezaje kusema mambo mema hali ninyi ni waovu? Maana mtu husema kutokana na yale yaliyojaa moyoni.
35The good man out of the good treasure of the heart doth put forth the good things, and the evil man out of the evil treasure doth put forth evil things.
35Mtu mwema hutoa mambo mema katika hazina yake njema; na mtu mbaya hutoa mambo mabaya katika hazina yake mbaya.
36`And I say to you, that every idle word that men may speak, they shall give for it a reckoning in a day of judgment;
36"Basi, nawaambieni, Siku ya hukumu watu watapaswa kujibu juu ya kila neno lisilofaa wanalosema.
37for from thy words thou shalt be declared righteous, and from thy words thou shalt be declared unrighteous.`
37Maana kwa maneno yako, utakubaliwa kuwa mwadilifu, na kwa maneno yako, utahukumiwa kuwa na hatia."
38Then answered certain of the scribes and Pharisees, saying, `Teacher, we will to see a sign from thee.`
38Kisha baadhi ya walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamwambia Yesu, "Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako."
39And he answering said to them, `A generation, evil and adulterous, doth seek a sign, and a sign shall not be given to it, except the sign of Jonah the prophet;
39Naye akawajibu, "Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara; hamtapewa ishara nyingine, ila tu ile ishara ya nabii Yona.
40for, as Jonah was in the belly of the fish three days and three nights, so shall the Son of Man be in the heart of the earth three days and three nights.
40Jinsi Yona alivyokaa siku tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha.
41`Men of Nineveh shall stand up in the judgment with this generation, and shall condemn it, for they reformed at the proclamation of Jonah, and lo, a greater than Jonah here!
41Watu wa Ninewi watatokea siku ya hukumu, nao watakihukumu kizazi hiki kwamba kina hatia. Maana Waninewi walitubu kwa sababu ya mahubiri ya Yona, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Yona!
42`A queen of the south shall rise up in the judgment with this generation, and shall condemn it, for she came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon, and lo, a greater than Solomon here!
42Malkia wa kusini atatokea wakati kizazi hiki kitakapohukumiwa, naye atakihukumu kwamba kina hatia. Maana yeye alisafiri kutoka mbali akaja kusikiliza maneno ya hekima ya Solomoni, na kumbe hapa kuna kikuu kuliko Solomoni.
43`And, when the unclean spirit may go forth from the man, it doth walk through dry places seeking rest, and doth not find;
43"Pepo mchafu akifukuzwa kwa mtu, huzururazurura jangwani akitafuta mahali pa kupumzika asipate.
44then it saith, I will turn back to my house whence I came forth; and having come, it findeth [it] unoccupied, swept, and adorned:
44Hapo hujisemea: Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka. Lakini anaporudi na kuikuta tupu, imefagiwa na kupambwa,
45then doth it go, and take with itself seven other spirits more evil than itself, and having gone in they dwell there, and the last of that man doth become worse than the first; so shall it be also to this evil generation.`
45huenda kuwachukua pepo wengine saba, wabaya kuliko yeye; na wote huja wakamwingia huyo mtu. Na hali ya mtu huyo sasa huwa mbaya kuliko hapo mwanzo. Ndivyo itakavyokuwa kwa watu hawa waovu."
46And while he was yet speaking to the multitudes, lo, his mother and brethren had stood without, seeking to speak to him,
46Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu zake walipofika na kusimama nje, wakitaka kusema naye.
47and one said to him, `Lo, thy mother and thy brethren do stand without, seeking to speak to thee.`
47Basi, mtu mmoja akamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kusema nawe."
48And he answering said to him who spake to him, `Who is my mother? and who are my brethren?`
48Lakini Yesu akamjibu mtu huyo, "Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni kina nani?"
49And having stretched forth his hand toward his disciples, he said, `Lo, my mother and my brethren!
49Kisha akaunyosha mkono wake kuelekea wanafunzi wake, akasema, "Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu!
50for whoever may do the will of my Father who is in the heavens, he is my brother, and sister, and mother.`
50Maana yeyote anayefanya anavyotaka Baba yangu aliye mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu."