1And in that day Jesus, having gone forth from the house, was sitting by the sea,
1Siku hiyohiyo, Yesu alitoka katika ile nyumba, akaenda na kuketi kando ya ziwa.
2and gathered together unto him were many multitudes, so that he having gone into the boat did sit down, and all the multitude on the beach did stand,
2Makundi makubwa ya watu yalimzunguka hata Yesu akapanda mashua, akaketi. Hao watu walisimama kwenye ukingo wa ziwa,
3and he spake to them many things in similes, saying: `Lo, the sower went forth to sow,
3naye Yesu akawaambia mambo mengi kwa mifano. "Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4and in his sowing, some indeed fell by the way, and the fowls did come and devour them,
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5and others fell upon the rocky places, where they had not much earth, and immediately they sprang forth, through not having depth of earth,
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6and the sun having risen they were scorched, and through not having root, they withered,
6Jua lilipochomoza, zilichomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7and others fell upon the thorns, and the thorns did come up and choke them,
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga.
8and others fell upon the good ground, and were giving fruit, some indeed a hundredfold, and some sixty, and some thirty.
8Lakini nyingine zilianguka penye udongo mzuri, zikaota, zikazaa: nyingine punje mia moja, nyingine sitini na nyingine thelathini.
9He who is having ears to hear — let him hear.`
9Mwenye masikio na asikie!"
10And the disciples having come near, said to him, `Wherefore in similes dost thou speak to them?`
10Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwuliza, "Kwa nini unasema na watu kwa mifano?"
11And he answering said to them that — `To you it hath been given to know the secrets of the reign of the heavens, and to these it hath not been given,
11Yesu akawajibu, "Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakujaliwa.
12for whoever hath, it shall be given to him, and he shall have overabundance, and whoever hath not, even that which he hath shall be taken from him.
12Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa; lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
13`Because of this, in similes do I speak to them, because seeing they do not see, and hearing they do not hear, nor understand,
13Ndiyo maana ninasema nao kwa mifano, kwa sababu wanatazama lakini hawaoni, wanasikiliza lakini hawasikii, wala hawaelewi.
14and fulfilled on them is the prophecy of Isaiah, that saith, With hearing ye shall hear, and ye shall not understand, and seeing ye shall see, and ye shall not perceive,
14Kwao yametimia yale aliyosema nabii Isaya: Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
15for made gross was the heart of this people, and with the ears they heard heavily, and their eyes they did close, lest they might see with the eyes, and with the ears might hear, and with the heart understand, and turn back, and I might heal them.
15Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameyaziba masikio yao, wameyafumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao. wangesikia kwa masikio yao, wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.
16`And happy are your eyes because they see, and your ears because they hear,
16"Lakini heri yenu ninyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia.
17for verily I say to you, that many prophets and righteous men did desire to see that which ye look on, and they did not see, and to hear that which ye hear, and they did not hear.
17Kweli nawaambieni, manabii na watu wengi wema walitamani kuyaona yale mnayoyaona, wasiyaone, na kuyasikia yale mnayoyasikia, wasiyasikie.
18`Ye, therefore, hear ye the simile of the sower:
18"Basi, ninyi sikilizeni maana ya mfano huo wa mpanzi.
19Every one hearing the word of the reign, and not understanding — the evil one doth come, and doth catch that which hath been sown in his heart; this is that sown by the way.
19Yeyote asikiaye ujumbe wa ufalme bila kuuelewa, ni kama zile mbegu zilizoanguka njiani; yule Mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake.
20`And that sown on the rocky places, this is he who is hearing the word, and immediately with joy is receiving it,
20Ile mbegu iliyopandwa penye mawe ni mfano wa mtu asikiaye ujumbe huo na mara akaupokea kwa furaha.
21and he hath not root in himself, but is temporary, and persecution or tribulation having happened because of the word, immediately he is stumbled.
21Lakini haumwingii na kuwa na mizizi ndani yake; huendelea kuuzingatia ujumbe huo kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya ujumbe huo, anakata tamaa mara.
22`And that sown toward the thorns, this is he who is hearing the word, and the anxiety of this age, and the deceitfulness of the riches, do choke the word, and it becometh unfruitful.
22Ile mbegu iliyoanguka kati ya miti ya miiba, ni mfano wa mtu asikiaye huo ujumbe, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu na anasa za mali huusonga ujumbe huo, naye hazai matunda.
23`And that sown on the good ground: this is he who is hearing the word, and is understanding, who indeed doth bear fruit, and doth make, some indeed a hundredfold, and some sixty, and some thirty.`
23Ile mbegu iliyopandwa katika udongo mzuri ni mfano wa mtu ausikiaye ujumbe huo na kuuelewa, naye huzaa matunda; mmoja mia, mwingine sitini na mwingine thelathini."
24Another simile he set before them, saying: `The reign of the heavens was likened to a man sowing good seed in his field,
24Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
25and, while men are sleeping, his enemy came and sowed darnel in the midst of the wheat, and went away,
25Lakini watu wakiwa wamelala, adui yake akaja akapanda magugu kati ya ngano, akaenda zake.
26and when the herb sprang up, and yielded fruit, then appeared also the darnel.
26Basi, mimea ilipoota na kuanza kuchanua, magugu pia yakaanza kuonekana.
27`And the servants of the householder, having come near, said to him, Sir, good seed didst thou not sow in thy field? whence then hath it the darnel?
27Watumishi wa yule mwenye shamba wakamwendea, wakamwambia, Mheshimiwa, bila shaka ulipanda mbegu nzuri katika shamba lako. Sasa magugu yametoka wapi?
28And he saith to them, A man, an enemy, did this; and the servants said to him, Wilt thou, then, [that] having gone away we may gather it up?
28Yeye akawajibu, Adui ndiye aliyefanya hivyo. Basi, watumishi wake wakamwuliza, Je, unataka twende tukayang'oe
29`And he said, No, lest — gathering up the darnel — ye root up with it the wheat,
29Naye akawajibu, La, msije labda mnapokusanya magugu, mkang'oa na ngano pia.
30suffer both to grow together till the harvest, and in the time of the harvest I will say to the reapers, Gather up first the darnel, and bind it in bundles, to burn it, and the wheat gather up into my storehouse.`
30Acheni vikue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji: kusanyeni kwanza magugu mkayafunge mafungumafungu ya kuchomwa. Lakini ngano ikusanyeni mkaiweke ghalani mwangu."
31Another simile he set before them, saying: `The reign of the heavens is like to a grain of mustard, which a man having taken, did sow in his field,
31Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja, akaipanda katika shamba lake.
32which less, indeed, is than all the seeds, but when it may be grown, is greatest of the herbs, and becometh a tree, so that the birds of the heaven do come and rest in its branches.`
32Yenyewe ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini ikishaota huwa kubwa kuliko mimea yote. Hukua ikawa mti, na ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake."
33Another simile spake he to them: `The reign of the heavens is like to leaven, which a woman having taken, hid in three measures of meal, till the whole was leavened.`
33Yesu akawaambia mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyotwaa mama mmoja, akaichanganya na unga pishi tatu, hata unga wote ukaumuka."
34All these things spake Jesus in similes to the multitudes, and without a simile he was not speaking to them,
34Yesu aliwaambia watu hayo yote kwa mifano. Hakuwaambia chochote bila kutumia mifano,
35that it might be fulfilled that was spoken through the prophet, saying, `I will open in similes my mouth, I will utter things having been hidden from the foundation of the world.`
35ili jambo lililonenwa na nabii litimie: "Nitasema kwa mifano; nitawaambia mambo yaliyofichika tangu kuumbwa ulimwengu."
36Then having let away the multitudes, Jesus came to the house, and his disciples came near to him, saying, `Explain to us the simile of the darnel of the field.`
36Kisha Yesu aliwaaga wale watu, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, "Tufafanulie ule mfano wa magugu shambani."
37And he answering said to them, `He who is sowing the good seed is the Son of Man,
37Yesu akawaambia, "Mpanzi wa zile mbegu nzuri ni Mwana wa Mtu.
38and the field is the world, and the good seed, these are the sons of the reign, and the darnel are the sons of the evil one,
38Lile shamba ni ulimwengu. Zile mbegu nzuri ni watu wale ambao Ufalme ni wao. Lakini yale magugu ni wale watu wa yule Mwovu.
39and the enemy who sowed them is the devil, and the harvest is a full end of the age, and the reapers are messengers.
39Adui aliyepanda yale magugu ni Ibilisi. Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika.
40`As, then, the darnel is gathered up, and is burned with fire, so shall it be in the full end of this age,
40Kama vile magugu yanavyokusanywa kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati;
41the Son of Man shall send forth his messengers, and they shall gather up out of his kingdom all the stumbling-blocks, and those doing the unlawlessness,
41Mwana wa Mtu atawatuma malaika wake wawakusanye kutoka katika Ufalme wake wale wote wenye kusababisha dhambi, na wote wenye kutenda maovu,
42and shall cast them to the furnace of the fire; there shall be the weeping and the gnashing of the teeth.
42na kuwatupa katika tanuru ya moto, na huko watalia na kusaga meno.
43`Then shall the righteous shine forth as the sun in the reign of their Father. He who is having ears to hear — let him hear.
43Kisha, wale wema watang'ara kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Sikieni basi, kama mna masikio!
44`Again, the reign of the heavens is like to treasure hid in the field, which a man having found did hide, and from his joy goeth, and all, as much as he hath, he selleth, and buyeth that field.
44"Ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu mmoja aliigundua, akaificha tena. Alifurahi sana hata akaenda kuuza yote aliyokuwa nayo, akalinunua shamba lile.
45`Again, the reign of the heavens is like to a man, a merchant, seeking goodly pearls,
45"Tena, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara mmoja mwenye kutafuta lulu nzuri.
46who having found one pearl of great price, having gone away, hath sold all, as much as he had, and bought it.
46Alipopata lulu moja ya thamani kubwa, alienda akauza yote aliyokuwa nayo, akainunua lulu ile.
47`Again, the reign of the heavens is like to a net that was cast into the sea, and did gather together of every kind,
47"Tena, Ufalme wa mbinguni unafanana na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina.
48which, when it was filled, having drawn up again upon the beach, and having sat down, they gathered the good into vessels, and the bad they did cast out,
48Ulipojaa, watu waliuvuta pwani, wakaketi, wakachagua samaki wazuri wakawaweka ndani ya vikapu vyao, na wabaya wakawatupa.
49so shall it be in the full end of the age, the messengers shall come forth and separate the evil out of the midst of the righteous,
49Ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati: malaika watatokea, watawatenganisha watu wabaya na watu wema,
50and shall cast them to the furnace of the fire, there shall be the weeping and the gnashing of the teeth.`
50na kuwatupa hao wabaya katika tanuru ya moto. Huko watalia na kusaga meno."
51Jesus saith to them, `Did ye understand all these?` They say to him, `Yes, sir.`
51Yesu akawauliza, "Je, mmeelewa mambo haya yote?" Wakamjibu, "Naam."
52And he said to them, `Because of this every scribe having been discipled in regard to the reign of the heavens, is like to a man, a householder, who doth bring forth out of his treasure things new and old.`
52Naye akawaambia, "Hivyo basi, kila mwalimu wa Sheria aliye mwanafunzi wa Ufalme wa mbinguni anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale."
53And it came to pass, when Jesus finished these similes, he removed thence,
53Yesu alipomaliza kusema mifano hiyo alitoka mahali hapo,
54and having come to his own country, he was teaching them in their synagogue, so that they were astonished, and were saying, `Whence to this one this wisdom and the mighty works?
54akaenda kijijini kwake. Huko akawa anawafundisha watu katika sunagogi hata wakashangaa, wakasema, "Huyu amepata wapi hekima hii na maajabu?
55is not this the carpenter`s son? is not his mother called Mary, and his brethren James, and Joses, and Simon, and Judas?
55Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56and his sisters — are they not all with us? whence, then, to this one all these?`
56Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?"
57and they were stumbled at him. And Jesus said to them, `A prophet is not without honor except in his own country, and in his own house:`
57Basi, wakawa na mashaka naye. Lakini Yesu akawaambia, "Nabii hakosi kuheshimiwa, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani mwake!"
58and he did not there many mighty works, because of their unbelief.
58Kwa hiyo, hakutenda miujiza mingi pale kwa sababu ya kutoamini kwao.