1And morning having come, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Jesus, so as to put him to death;
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
2and having bound him, they did lead away, and delivered him up to Pontius Pilate, the governor.
2Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
3Then Judas — he who delivered him up — having seen that he was condemned, having repented, brought back the thirty silverlings to the chief priests, and to the elders, saying,
3Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
4`I did sin, having delivered up innocent blood;` and they said, `What — to us? thou shalt see!`
4Akawaambia, "Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe." Lakini wao wakasema, "Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako."
5and having cast down the silverlings in the sanctuary, he departed, and having gone away, he did strangle himself.
5Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
6And the chief priests having taken the silverlings, said, `It is not lawful to put them to the treasury, seeing it is the price of blood;`
6Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, "Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu."
7and having taken counsel, they bought with them the field of the potter, for the burial of strangers;
7Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8therefore was that field called, `Field of blood,` unto this day.
8Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
9Then was fulfilled that spoken through Jeremiah the prophet, saying, `And I took the thirty silverlings, the price of him who hath been priced, whom they of the sons of Israel did price,
9Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: "Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
10and gave them for the field of the potter, as the Lord did appoint to me.`
10wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza."
11And Jesus stood before the governor, and the governor did question him, saying, `Art thou the king of the Jews!` And Jesus said to him, `Thou sayest.`
11Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, "Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamwambia, "Wewe umesema."
12And in his being accused by the chief priests and the elders, he did not answer any thing,
12Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
13then saith Pilate to him, `Dost thou not hear how many things they witness against thee?`
13Hivyo Pilato akamwuliza, "Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?"
14And he did not answer him, not even to one word, so that the governor did wonder greatly.
14Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
15And at the feast the governor had been accustomed to release one to the multitude, a prisoner, whom they willed,
15Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
16and they had then a noted prisoner, called Barabbas,
16Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
17they therefore having been gathered together, Pilate said to them, `Whom will ye I shall release to you? Barabbas or Jesus who is called Christ?`
17Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, "Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?"
18for he had known that because of envy they had delivered him up.
18Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
19And as he is sitting on the tribunal, his wife sent unto him, saying, `Nothing — to thee and to that righteous one, for many things did I suffer to-day in a dream because of him.`
19Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: "Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake."
20And the chief priests and the elders did persuade the multitudes that they might ask for themselves Barabbas, and might destroy Jesus;
20Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
21and the governor answering said to them, `Which of the two will ye [that] I shall release to you?` And they said, `Barabbas.`
21Mkuu wa mkoa akawauliza, "Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?" Wakamjibu, "Baraba!"
22Pilate saith to them, `What then shall I do with Jesus who is called Christ?` They all say to him, `Let be crucified!`
22Pilato akawauliza, "Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?" Wote wakasema, "Asulubiwe!"
23And the governor said, `Why, what evil did he?` and they were crying out the more, saying, `Let be crucified.`
23Pilato akauliza, "Kwa nini? Amefanya kosa gani?" Wao wakazidi kupaaza sauti: "Asulubiwe!"
24And Pilate having seen that it profiteth nothing, but rather a tumult is made, having taken water, he did wash the hands before the multitude, saying, `I am innocent from the blood of this righteous one; ye — ye shall see;`
24Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, "Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe."
25and all the people answering said, `His blood [is] upon us, and upon our children!`
25Watu wote wakasema, "Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!"
26Then did he release to them Barabbas, and having scourged Jesus, he delivered [him] up that he may be crucified;
26Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
27then the soldiers of the governor having taken Jesus to the Praetorium, did gather to him all the band;
27Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
28and having unclothed him, they put around him a crimson cloak,
28Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
29and having plaited him a crown out of thorns they put [it] on his head, and a reed in his right hand, and having kneeled before him, they were mocking him, saying, `Hail, the king of the Jews.`
29Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, "Shikamoo mfalme wa Wayahudi!"
30And having spit on him, they took the reed, and were smiting on his head;
30Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
31and when they had mocked him, they took off from him the cloak, and put on him his own garments, and led him away to crucify [him].
31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
32And coming forth, they found a man, a Cyrenian, by name Simon: him they impressed that he might bear his cross;
32Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
33and having come to a place called Golgotha, that is called Place of a Skull,
33Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la kichwa,"
34they gave him to drink vinegar mixed with gall, and having tasted, he would not drink.
34wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
35And having crucified him, they divided his garments, casting a lot, that it might be fulfilled that was spoken by the prophet, `They divided my garments to themselves, and over my vesture they cast a lot;`
35Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
36and sitting down, they were watching him there,
36Wakaketi, wakawa wanamchunga.
37and they put up over his head, his accusation written, `This is Jesus, the king of the Jews.`
37Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, "Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi."
38Then crucified with him are two robbers, one on the right hand, and one on the left,
38Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
39and those passing by were speaking evil of him, wagging their heads,
39Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
40and saying, `Thou that art throwing down the sanctuary, and in three days building [it], save thyself; if Son thou art of God, come down from the cross.`
40"Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!"
41And in like manner also the chief priests mocking, with the scribes and elders, said,
41Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
42`Others he saved; himself he is not able to save! If he be King of Israel, let him come down now from the cross, and we will believe him;
42"Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
43he hath trusted on God, let Him now deliver him, if He wish him, because he said — Son of God I am;`
43Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka."
44with the same also the robbers, who were crucified with him, were reproaching him.
44Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
45And from the sixth hour darkness came over all the land unto the ninth hour,
45Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
46and about the ninth hour Jesus cried out with a great voice, saying, `Eli, Eli, lama sabachthani?` that is, `My God, my God, why didst Thou forsake me?`
46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eli, Eli, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
47And certain of those standing there having heard, said — `Elijah he doth call;`
47Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, "Anamwita Eliya."
48and immediately, one of them having run, and having taken a spunge, having filled [it] with vinegar, and having put [it] on a reed, was giving him to drink,
48Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
49but the rest said, `Let alone, let us see if Elijah doth come — about to save him.`
49Wengine wakasema, "Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa."
50And Jesus having again cried with a great voice, yielded the spirit;
50Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
51and lo, the vail of the sanctuary was rent in two from top unto bottom, and the earth did quake, and the rocks were rent,
51Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52and the tombs were opened, and many bodies of the saints who have fallen asleep, arose,
52makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
53and having come forth out of the tombs after his rising, they went into the holy city, and appeared to many.
53nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
54And the centurion, and those with him watching Jesus, having seen the earthquake, and the things that were done, were exceedingly afraid, saying, `Truly this was God`s Son.`
54Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu."
55And there were there many women beholding from afar, who did follow Jesus from Galilee, ministering to him,
55Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
56among whom was Mary the Magdalene, and Mary the mother of James and of Joses, and the mother of the sons of Zebedee.
56Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
57And evening having come, there came a rich man, from Arimathea, named Joseph, who also himself was discipled to Jesus,
57Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58he having gone near to Pilate, asked for himself the body of Jesus; then Pilate commanded the body to be given back.
58Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
59And having taken the body, Joseph wrapped it in clean linen,
59Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
60and laid it in his new tomb, that he hewed in the rock, and having rolled a great stone to the door of the tomb, he went away;
60akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
61and there were there Mary the Magdalene, and the other Mary, sitting over-against the sepulchre.
61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
62And on the morrow that is after the preparation, were gathered together the chief priests, and the Pharisees, unto Pilate,
62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
63saying, `Sir, we have remembered that that deceiver said while yet living, After three days I do rise;
63Wakasema, "Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64command, then, the sepulchre to be made secure till the third day, lest his disciples, having come by night, may steal him away, and may say to the people, He rose from the dead, and the last deceit shall be worse than the first.`
64Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali."
65And Pilate said to them, `Ye have a watch, go away, make secure — as ye have known;`
65Pilato akawaambia, "Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo."
66and they, having gone, did make the sepulchre secure, having sealed the stone, together with the watch.
66Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.