1And it came to pass, when Jesus finished all these words, he said to his disciples,
1Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2`Ye have known that after two days the passover cometh, and the Son of Man is delivered up to be crucified.`
2"Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe."
3Then were gathered together the chief priests, and the scribes, and the elders of the people, to the court of the chief priest who was called Caiaphas;
3Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4and they consulted together that they might take Jesus by guile, and kill [him],
4Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5and they said, `Not in the feast, that there may not be a tumult among the people.`
5Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6And Jesus having been in Bethany, in the house of Simon the leper,
6Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7there came to him a woman having an alabaster box of ointment, very precious, and she poured on his head as he is reclining (at meat).
7mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8And having seen [it], his disciples were much displeased, saying, `To what purpose [is] this waste?
8Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, "Ya nini hasara hii?
9for this ointment could have been sold for much, and given to the poor.`
9Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha."
10And Jesus having known, said to them, `Why do ye give trouble to the woman? for a good work she wrought for me;
10Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11for the poor always ye have with you, and me ye have not always;
11Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12for she having put this ointment on my body — for my burial she did [it].
12Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13Verily I say to you, Wherever this good news may be proclaimed in the whole world, what this [one] did shall also be spoken of — for a memorial of her.`
13Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye."
14Then one of the twelve, who is called Judas Iscariot, having gone unto the chief priests, said,
14Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15`What are ye willing to give me, and I will deliver him up to you?` and they weighed out to him thirty silverlings,
15akawaambia, "Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?" Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16and from that time he was seeking a convenient season to deliver him up.
16na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17And on the first [day] of the unleavened food came the disciples near to Jesus, saying to him, `Where wilt thou [that] we may prepare for thee to eat the passover?`
17Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, "Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?"
18and he said, `Go away to the city, unto such a one, and say to him, The Teacher saith, My time is nigh; near thee I keep the passover, with my disciples;`
18Yeye akawajibu, "Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu."
19and the disciples did as Jesus appointed them, and prepared the passover.
19Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20And evening having come, he was reclining (at meat) with the twelve,
20Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21and while they are eating, he said, `Verily I say to you, that one of you shall deliver me up.`
21Walipokuwa wakila, Yesu akasema, "Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti."
22And being grieved exceedingly, they began to say to him, each of them, `Is it I, Sir?`
22Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, "Bwana! Je, ni mimi?"
23And he answering said, `He who did dip with me the hand in the dish, he will deliver me up;
23Yesu akajibu, "Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24the Son of Man doth indeed go, as it hath been written concerning him, but wo to that man through whom the Son of Man is delivered up! good it were for him if that man had not been born.`
24Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa."
25And Judas — he who delivered him up — answering said, `Is it I, Rabbi?` He saith to him, `Thou hast said.`
25Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, "Mwalimu! Je, ni mimi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
26And while they were eating, Jesus having taken the bread, and having blessed, did brake, and was giving to the disciples, and said, `Take, eat, this is my body;`
26Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni mle; huu ni mwili wangu."
27and having taken the cup, and having given thanks, he gave to them, saying, `Drink ye of it — all;
27Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, "Nyweni nyote;
28for this is my blood of the new covenant, that for many is being poured out — to remission of sins;
28maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29and I say to you, that I may not drink henceforth on this produce of the vine, till that day when I may drink it with you new in the reign of my Father.`
29Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu."
30And having sung a hymn, they went forth to the mount of the Olives;
30Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31then saith Jesus to them, `All ye shall be stumbled at me this night; for it hath been written, I will smite the shepherd, and the sheep of the flock shall be scattered abroad;
31Kisha Yesu akawaambia, "Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32but, after my having risen, I will go before you to Galilee.`
32Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya."
33And Peter answering said to him, `Even if all shall be stumbled at thee, I will never be stumbled.`
33Petro akamwambia Yesu "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe."
34Jesus said to him, `Verily I say to thee, that, this night, before cock-crowing, thrice thou wilt deny me.`
34Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
35Peter saith to him, `Even if it may be necessary for me to die with thee, I will not deny thee;` in like manner also said all the disciples.
35Petro akamwambia, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe." Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36Then come with them doth Jesus to a place called Gethsemane, and he saith to the disciples, `Sit ye here, till having gone away, I shall pray yonder.`
36Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali."
37And having taken Peter, and the two sons of Zebedee, he began to be sorrowful, and to be very heavy;
37Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38then saith he to them, `Exceedingly sorrowful is my soul — unto death; abide ye here, and watch with me.`
38Hapo akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami."
39And having gone forward a little, he fell on his face, praying, and saying, `My Father, if it be possible, let this cup pass from me; nevertheless, not as I will, but as Thou.`
39Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: "Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe."
40And he cometh unto the disciples, and findeth them sleeping, and he saith to Peter, `So! ye were not able one hour to watch with me!
40Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, "Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41watch, and pray, that ye may not enter into temptation: the spirit indeed is forward, but the flesh weak.`
41Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu."
42Again, a second time, having gone away, he prayed, saying, `My Father, if this cup cannot pass away from me except I drink it, Thy will be done;`
42Akaenda tena mara ya pili akasali: "Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike."
43and having come, he findeth them again sleeping, for their eyes were heavy.
43Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44And having left them, having gone away again, he prayed a third time, saying the same word;
44Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45then cometh he unto his disciples, and saith to them, `Sleep on henceforth, and rest! lo, the hour hath come nigh, and the Son of Man is delivered up to the hands of sinners.
45Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, "Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46Rise, let us go; lo, he hath come nigh who is delivering me up.`
46Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti."
47And while he is yet speaking, lo, Judas, one of the twelve did come, and with him a great multitude, with swords and sticks, from the chief priests and elders of the people.
47Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48And he who did deliver him up did give them a sign, saying, `Whomsoever I will kiss, it is he: lay hold on him;`
48Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni."
49and immediately, having come to Jesus, he said, `Hail, Rabbi,` and kissed him;
49Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, "Shikamoo, Mwalimu!" Kisha akambusu.
50and Jesus said to him, `Comrade, for what art thou present?` Then having come near, they laid hands on Jesus, and took hold on him.
50Yesu akamwambia, "Rafiki, fanya ulichokuja kufanya." Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51And lo, one of those with Jesus, having stretched forth the hand, drew his sword, and having struck the servant of the chief priest, he took off his ear.
51Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52Then saith Jesus to him, `Turn back thy sword to its place; for all who did take the sword, by the sword shall perish;
52Hapo Yesu akamwambia, "Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53dost thou think that I am not able now to call upon my Father, and He will place beside me more than twelve legions of messengers?
53Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54how then may the Writings be fulfilled, that thus it behoveth to happen?`
54Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?"
55In that hour said Jesus to the multitudes, `As against a robber ye did come forth, with swords and sticks, to take me! daily with you I was sitting teaching in the temple, and ye did not lay hold on me;
55Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, "Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56but all this hath come to pass, that the Writings of the prophets may be fulfilled;` then all the disciples, having left him, fled.
56Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie." Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57And those laying hold on Jesus led [him] away unto Caiaphas the chief priest, where the scribes and the elders were gathered together,
57Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58and Peter was following him afar off, unto the court of the chief priest, and having gone in within, he was sitting with the officers, to see the end.
58Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59And the chief priests, and the elders, and all the council, were seeking false witness against Jesus, that they might put him to death,
59Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60and they did not find; and many false witnesses having come near, they did not find; and at last two false witnesses having come near,
60lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61said, `This one said, I am able to throw down the sanctuary of God, and after three days to build it.`
61wakasema, "Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu."
62And the chief priest having stood up, said to him, `Nothing thou dost answer! what do these witness against thee?
62Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
63and Jesus was silent. And the chief priest answering said to him, `I adjure thee, by the living God, that thou mayest say to us, if thou art the Christ — the Son of God.`
63Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, "Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!"
64Jesus saith to him, `Thou hast said; nevertheless I say to you, hereafter ye shall see the Son of Man sitting on the right hand of the power, and coming upon the clouds, of the heaven.`
64Yesu akamwambia, "Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni."
65Then the chief priest rent his garments, saying, — `He hath spoken evil; what need have we yet of witnesses? lo, now ye heard his evil speaking;
65Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, "Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66what think ye?` and they answering said, `He is worthy of death.`
66Ninyi mwaonaje?" Wao wakamjibu, "Anastahili kufa!"
67Then did they spit in his face and buffet him, and others did slap,
67Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68saying, `Declare to us, O Christ, who he is that struck thee?`
68wakasema, "Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!"
69And Peter without was sitting in the court, and there came near to him a certain maid, saying, `And thou wast with Jesus of Galilee!`
69Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, "Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya."
70And he denied before all, saying, `I have not known what thou sayest.`
70Petro akakana mbele ya wote akisema, "Sijui hata unasema nini."
71And he having gone forth to the porch, another female saw him, and saith to those there, `And this one was with Jesus of Nazareth;`
71Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, "Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti."
72and again did he deny with an oath — `I have not known the man.`
72Petro akakana tena kwa kiapo: "Simjui mtu huyo."
73And after a little those standing near having come, said to Peter, `Truly thou also art of them, for even thy speech doth make thee manifest.`
73Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, "Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha."
74Then began he to anathematise, and to swear — `I have not known the man;` and immediately did a cock crow,
74Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, "Simjui mtu huyo!" Mara jogoo akawika.
75and Peter remembered the saying of Jesus, he having said to him — `Before cock-crowing, thrice thou wilt deny me;` and having gone without, he did weep bitterly.
75Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: "Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu." Basi, akatoka nje akalia sana.