1`Then shall the reign of the heavens be likened to ten virgins, who, having taken their lamps, went forth to meet the bridegroom;
1"Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2and five of them were prudent, and five foolish;
2Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3they who were foolish having taken their lamps, did not take with themselves oil;
3Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4and the prudent took oil in their vessels, with their lamps.
4Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5`And the bridegroom tarrying, they all nodded and were sleeping,
5Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6and in the middle of the night a cry was made, Lo, the bridegroom doth come; go ye forth to meet him.
6Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7`Then rose all those virgins, and trimmed their lamps,
7Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8and the foolish said to the prudent, Give us of your oil, because our lamps are going out;
8Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9and the prudent answered, saying — Lest there may not be sufficient for us and you, go ye rather unto those selling, and buy for yourselves.
9Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10`And while they are going away to buy, the bridegroom came, and those ready went in with him to the marriage-feasts, and the door was shut;
10Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11and afterwards come also do the rest of the virgins, saying, Sir, sir, open to us;
11Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12and he answering said, Verily I say to you, I have not known you.
12Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi."
13`Watch therefore, for ye have not known the day nor the hour in which the Son of Man doth come.
13Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14`For — as a man going abroad did call his own servants, and did deliver to them his substance,
14"Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15and to one he gave five talents, and to another two, and to another one, to each according to his several ability, went abroad immediately.
15Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16`And he who did receive the five talents, having gone, wrought with them, and made other five talents;
16Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17in like manner also he who [received] the two, he gained, also he, other two;
17Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18and he who did receive the one, having gone away, digged in the earth, and hid his lord`s money.
18Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19`And after a long time cometh the lord of those servants, and taketh reckoning with them;
19"Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20and he who did receive the five talents having come, brought other five talents, saying, `Sir, five talents thou didst deliver to me; lo, other five talents did I gain besides them.
20Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21`And his lord said to him, Well done, servant, good and faithful, over a few things thou wast faithful, over many things I will set thee; enter into the joy of thy lord.
21Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22`And he who also did receive the two talents having come, said, Sir, two talents thou didst deliver to me; lo, other two talents I did gain besides them.
22"Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23`His lord said to him, Well done, servant, good and faithful, over a few things thou wast faithful, over many things I will set thee; enter into the joy of thy lord.
23Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24`And he also who hath received the one talent having come, said, Sir, I knew thee, that thou art a hard man, reaping where thou didst not sow, and gathering from whence thou didst not scatter;
24"Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25and having been afraid, having gone away, I hid thy talent in the earth; lo, thou hast thine own!
25Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26`And his lord answering said to him, Evil servant, and slothful, thou hadst known that I reap where I did not sow, and I gather whence I did not scatter!
26"Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27it behoved thee then to put my money to the money-lenders, and having come I had received mine own with increase.
27Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28`Take therefore from him the talent, and give to him having the ten talents,
28Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29for to every one having shall be given, and he shall have overabundance, and from him who is not having, even that which he hath shall be taken from him;
29Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30and the unprofitable servant cast ye forth to the outer darkness; there shall be the weeping and the gnashing of the teeth.
30Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31`And whenever the Son of Man may come in his glory, and all the holy messengers with him, then he shall sit upon a throne of his glory;
31"Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32and gathered together before him shall be all the nations, and he shall separate them from one another, as the shepherd doth separate the sheep from the goats,
32na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33and he shall set the sheep indeed on his right hand, and the goats on the left.
33Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34`Then shall the king say to those on his right hand, Come ye, the blessed of my Father, inherit the reign that hath been prepared for you from the foundation of the world;
34"Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35for I did hunger, and ye gave me to eat; I did thirst, and ye gave me to drink; I was a stranger, and ye received me;
35Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36naked, and ye put around me; I was infirm, and ye looked after me; in prison I was, and ye came unto me.
36nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37`Then shall the righteous answer him, saying, Lord, when did we see thee hungering, and we nourished? or thirsting, and we gave to drink?
37Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38and when did we see thee a stranger, and we received? or naked, and we put around?
38Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39and when did we see thee infirm, or in prison, and we came unto thee?
39Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40`And the king answering, shall say to them, Verily I say to you, Inasmuch as ye did [it] to one of these my brethren — the least — to me ye did [it].
40Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41Then shall he say also to those on the left hand, Go ye from me, the cursed, to the fire, the age-during, that hath been prepared for the Devil and his messengers;
41"Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake.
42for I did hunger, and ye gave me not to eat; I did thirst, and ye gave me not to drink;
42Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43a stranger I was, and ye did not receive me; naked, and ye put not around me; infirm, and in prison, and ye did not look after me.
43Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44`Then shall they answer, they also, saying, Lord, when did we see thee hungering, or thirsting, or a stranger, or naked, or infirm, or in prison, and we did not minister to thee?
44"Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45`Then shall he answer them, saying, Verily I say to you, Inasmuch as ye did [it] not to one of these, the least, ye did [it] not to me.
45Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46And these shall go away to punishment age-during, but the righteous to life age-during.`
46Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele."