1And when he came down from the mount, great multitudes did follow him,
1Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata.
2and lo, a leper having come, was bowing to him, saying, `Sir, if thou art willing, thou art able to cleanse me;`
2Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, "Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!"
3and having stretched forth the hand, Jesus touched him, saying, `I will, be thou cleansed,` and immediately his leprosy was cleansed.
3Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka! Takasika." Mara huyo mtu akapona ukoma wake.
4And Jesus saith to him, `See, thou mayest tell no one, but go, thyself shew to the priest, and bring the gift that Moses commanded for a testimony to them.`
4Kisha Yesu akamwambia, "Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka iliyoamriwa na Mose kuwathibitishia kwamba umepona."
5And Jesus having entered into Capernaum, there came to him a centurion calling upon him,
5Yesu alipokuwa anaingia mjini Kafarnaumu, ofisa mmoja Mroma alimwendea, akamsihi
6and saying, `Sir, my young man hath been laid in the house a paralytic, fearfully afflicted,`
6akisema, "Mheshimiwa, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza na anaumwa sana."
7and Jesus saith to him, `I, having come, will heal him.`
7Yesu akamwambia, "Nitakuja kumponya."
8And the centurion answering said, `Sir, I am not worthy that thou mayest enter under my roof, but only say a word, and my servant shall be healed;
8Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, sistahili uingie nyumbani mwangu. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona.
9for I also am a man under authority, having under myself soldiers, and I say to this one, Go, and he goeth, and to another, Be coming, and he cometh, and to my servant, Do this, and he doth [it].`
9Maana, hata mimi niliye mtu chini ya mamlaka ya wengine, ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda! naye huenda; na mwingine, Njoo! naye huja; na mtumishi wangu, Fanya kitu hiki! naye hufanya."
10And Jesus having heard, did wonder, and said to those following, `Verily I say to you, not even in Israel so great faith have I found;
10Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia watu waliokuwa wanamfuata, "Kweli nawaambieni, sijapata kumwona mtu yeyote katika Israeli aliye na imani kama hii.
11and I say to you, that many from east and west shall come and recline (at meat) with Abraham, and Isaac, and Jacob, in the reign of the heavens,
11Basi, nawaambieni kwamba watu wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaka na Yakobo katika Ufalme wa mbinguni.
12but the sons of the reign shall be cast forth to the outer darkness — there shall be the weeping and the gnashing of the teeth.`
12Lakini wale ambao wangalipaswa kuwa katika Ufalme huo watatupwa nje, gizani, ambako watalia na kusaga meno."
13And Jesus said to the centurion, `Go, and as thou didst believe let it be to thee;` and his young man was healed in that hour.
13Kisha Yesu akamwambia huyo ofisa Mroma, "Nenda nyumbani; na iwe kama ulivyoamini." Na mtumishi wake akapona saa ileile.
14And Jesus having come into the house of Peter, saw his mother-in-law laid, and fevered,
14Yesu alifika nyumbani kwa Petro, akamkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, ana homa kali.
15and he touched her hand, and the fever left her, and she arose, and was ministering to them.
15Basi, Yesu akamgusa huyo mama mkono, na homa ikamwacha; akasimama, akamtumikia.
16And evening having come, they brought to him many demoniacs, and he did cast out the spirits with a word, and did heal all who were ill,
16Ilipokuwa jioni, walimletea watu wengi waliokuwa wamepagawa na pepo; naye, kwa kusema neno tu, akawafukuza hao pepo. Aliwaponya pia watu wote waliokuwa wagonjwa.
17that it might be fulfilled that was spoken through Isaiah the prophet, saying, `Himself took our infirmities, and the sicknesses he did bear.`
17Alifanya hivyo ili yale aliyosema nabii Isaya yatimie: "Yeye mwenyewe ameondoa udhaifu wetu, ameyachukua magonjwa yetu."
18And Jesus having seen great multitudes about him, did command to depart to the other side;
18Yesu alipoona kundi la watu limemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake waende ng'ambo ya ziwa.
19and a certain scribe having come, said to him, `Teacher, I will follow thee wherever thou mayest go;`
19Mwalimu mmoja wa Sheria akamwendea, akamwambia, "Mwalimu, mimi nitakufuata kokote uendako."
20and Jesus saith to him, `The foxes have holes, and the birds of the heaven places of rest, but the Son of Man hath not where he may lay the head.`
20Yesu akamjibu, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
21And another of his disciples said to him, `Sir, permit me first to depart and to bury my father;`
21Kisha mtu mwingine miongoni mwa wanafunzi wake akamwambia, "Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzike baba yangu."
22and Jesus said to him, `Follow me, and suffer the dead to bury their own dead.`
22Lakini Yesu akamwambia, "Nifuate! Waache wafu wazike wafu wao."
23And when he entered into the boat his disciples did follow him,
23Yesu alipanda mashua, na wanafunzi wake wakaenda pamoja naye.
24and lo, a great tempest arose in the sea, so that the boat was being covered by the waves, but he was sleeping,
24Ghafla, dhoruba kali ikatokea ziwani, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua. Yesu alikuwa amelala usingizi.
25and his disciples having come to him, awoke him, saying, `Sir, save us; we are perishing.`
25Wanafunzi wakamwendea, wakamwamsha wakisema, "Bwana, tuokoe, tunaangamia!"
26And he saith to them, `Why are ye fearful, O ye of little faith?` Then having risen, he rebuked the winds and the sea, and there was a great calm;
26Yesu akawaambia, "Enyi watu wenye imani haba; mbona mnaogopa?" Basi, akainuka, akazikemea pepo na mawimbi; kukawa shwari kabisa.
27and the men wondered, saying, `What kind — is this, that even the wind and the sea do obey him?`
27Watu wakashangaa, wakasema, "Ni mtu wa namna gani huyu? Hata pepo na mawimbi vinamtii!"
28And he having come to the other side, to the region of the Gergesenes, there met him two demoniacs, coming forth out of the tombs, very fierce, so that no one was able to pass over by that way,
28Yesu alifika katika nchi ya Wagerasi, ng'ambo ya ziwa, na huko watu wawili waliopagawa na pepo wakakutana naye wakitokea makaburini. Watu hawa walikuwa wenye kutisha mno, hata hakuna mtu aliyethubutu kupita katika njia hiyo.
29and lo, they cried out, saying, `What — to us and to thee, Jesus, Son of God? didst thou come hither, before the time, to afflict us?`
29Nao wakaanza kupiga kelele, "Una shauri gani nasi, wewe Mwana wa Mungu? Je, umekuja kututesa kabla ya wakati wake?"
30And there was far off from them a herd of many swine feeding,
30Karibu na mahali hapo kulikuwa na nguruwe wengi wakichungwa.
31and the demons were calling on him, saying, `If thou dost cast us forth, permit us to go away to the herd of the swine;`
31Basi, hao pepo wakamsihi, "Ikiwa utatutoa, basi uturuhusu tuwaingie nguruwe wale."
32and he saith to them, `Go.` And having come forth, they went to the herd of the swine, and lo, the whole herd of the swine rushed down the steep, to the sea, and died in the waters,
32Yesu akawaambia, "Haya, nendeni." Hapo wakawatoka watu hao, wakawaingia nguruwe. Kundi lote la nguruwe likaporomoka kwenye ule mteremko mkali, likatumbukia ziwani; nguruwe wote wakafa maji.
33and those feeding did flee, and, having gone to the city, they declared all, and the matter of the demoniacs.
33Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakaenda mjini. Huko walitoa habari zote na mambo yaliyowapata wale watu waliokuwa wamepagawa.
34And lo, all the city came forth to meet Jesus, and having seen him, they called on [him] that he might depart from their borders.
34Basi, watu wote katika mji ule walitoka, wakamwendea Yesu; na walipomwona, wakamsihi aondoke katika nchi yao.