Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Matthew

9

1And having gone to the boat, he passed over, and came to his own city,
1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2and lo, they were bringing to him a paralytic, laid upon a couch, and Jesus having seen their faith, said to the paralytic, `Be of good courage, child, thy sins have been forgiven thee.`
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
3And lo, certain of the scribes said within themselves, `This one doth speak evil.`
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
4And Jesus, having known their thoughts, said, `Why think ye evil in your hearts?
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
5for which is easier? to say, The sins have been forgiven to thee; or to say, Rise, and walk?
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
6`But, that ye may know that the Son of Man hath power upon the earth to forgive sins — (then saith he to the paralytic) — having risen, take up thy couch, and go to thy house.`
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
7And he, having risen, went to his house,
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
8and the multitudes having seen, wondered, and glorified God, who did give such power to men.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
9And Jesus passing by thence, saw a man sitting at the tax-office, named Matthew, and saith to him, `Be following me,` and he, having risen, did follow him.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
10And it came to pass, he reclining (at meat) in the house, that lo, many tax-gatherers and sinners having come, were lying (at meat) with Jesus and his disciples,
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
11and the Pharisees having seen, said to his disciples, `Wherefore with the tax-gatherers and sinners doth your teacher eat?`
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
12And Jesus having heard, said to them, `They who are whole have no need of a physician, but they who are ill;
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
13but having gone, learn ye what is, Kindness I will, and not sacrifice, for I did not come to call righteous men, but sinners, to reformation.`
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
14Then come to him do the disciples of John, saying, `Wherefore do we and the Pharisees fast much, and thy disciples fast not?`
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
15And Jesus said to them, `Can the sons of the bride-chamber mourn, so long as the bridegroom is with them? but days shall come when the bridegroom may be taken from them, and then they shall fast.
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
16`And no one doth put a patch of undressed cloth on an old garment, for its filling up doth take from the garment, and a worse rent is made.
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
17`Nor do they put new wine into old skins, and if not — the skins burst, and the wine doth run out, and the skins are destroyed, but they put new wine into new skins, and both are preserved together.`
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
18While he is speaking these things to them, lo, a ruler having come, was bowing to him, saying that `My daughter just now died, but, having come, lay thy hand upon her, and she shall live.`
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
19And Jesus having risen, did follow him, also his disciples,
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
20and lo, a woman having an issue of blood twelve years, having come to him behind, did touch the fringe of his garments,
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
21for she said within herself, `If only I may touch his garment, I shall be saved.`
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
22And Jesus having turned about, and having seen her, said, `Be of good courage, daughter, thy faith hath saved thee,` and the woman was saved from that hour.
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
23And Jesus having come to the house of the ruler, and having seen the minstrels and the multitude making tumult,
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
24he saith to them, `Withdraw, for the damsel did not die, but doth sleep,` and they were deriding him;
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
25but, when the multitude was put forth, having gone in, he took hold of her hand, and the damsel arose,
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
26and the fame of this went forth to all the land.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
27And Jesus passing on thence, two blind men followed him, calling and saying, `Deal kindly with us, Son of David.`
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
28And he having come to the house, the blind men came to him, and Jesus saith to them, `Believe ye that I am able to do this?` They say to him, `Yes, sir.`
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
29Then touched he their eyes, saying, `According to your faith let it be to you,`
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
30and their eyes were opened, and Jesus strictly charged them, saying, `See, let no one know;`
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
31but they, having gone forth, did spread his fame in all that land.
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
32And as they are coming forth, lo, they brought to him a man dumb, a demoniac,
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
33and the demon having been cast out, the dumb spake, and the multitude did wonder, saying that `It was never so seen in Israel:`
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
34but the Pharisees said, `By the ruler of the demons he doth cast out the demons.`
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
35And Jesus was going up and down all the cities and the villages, teaching in their synagogues, and proclaiming the good news of the reign, and healing every sickness and every malady among the people.
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
36And having seen the multitudes, he was moved with compassion for them, that they were faint and cast aside, as sheep not having a shepherd,
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
37then saith he to his disciples, `The harvest indeed [is] abundant, but the workmen few;
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38beseech ye therefore the Lord of the harvest, that he may put forth workmen to His harvest.`
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."