Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Revelation

10

1And I saw another strong messenger coming down out of the heaven, arrayed with a cloud, and a rainbow upon the head, and his face as the sun, and his feet as pillars of fire,
1Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu, na upinde wa mvua kichwani mwake. Uso wake ulikuwa kama jua, na miguu yake ilikuwa kama moto.
2and he had in his hand a little scroll opened, and he did place his right foot upon the sea, and the left upon the land,
2Mikononi mwake alishika kitabu kidogo kimefunguliwa. Aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari, na wa kushoto juu ya nchi kavu,
3and he cried with a great voice, as a lion doth roar, and when he cried, speak out did the seven thunders their voices;
3na kuita kwa sauti kubwa kama ya mngurumo wa simba. Alipopaaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo.
4and when the seven thunders spake their voices, I was about to write, and I heard a voice out of the heaven saying to me, `Seal the things that the seven thunders spake,` and, `Thou mayest not write these things.`
4Na hizo ngurumo saba ziliposema, mimi nikataka kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni: "Maneno ya ngurumo hizo saba ni siri; usiyaandike!"
5And the messenger whom I saw standing upon the sea, and upon the land, did lift up his hand to the heaven,
5Kisha yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni,
6and did swear in Him who doth live to the ages of the ages, who did create the heaven and the things in it, and the land and the things in it, and the sea and the things in it — that time shall not be yet,
6akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, Mungu aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, bahari na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo. Akasema, "Wakati wa kusubiri zaidi umekwisha!
7but in the days of the voice of the seventh messenger, when he may be about to sound, and the secret of God may be finished, as He did declare to His own servants, to the prophets.
7Lakini wakati ule malaika wa saba atakapotoa sauti yake, wakati atakapopiga tarumbeta yake, Mungu atakamilisha mpango wake wa siri kama alivyowatangazia watumishi wake manabii."
8And the voice that I heard out of the heaven is again speaking with me, and saying, `Go, take the little scroll that is open in the hand of the messenger who hath been standing upon the sea, and upon the land:`
8Kisha ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni pale awali ikasema nami tena: "Nenda ukakichukue kile kitabu kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika asimamaye juu ya bahari na juu ya nchi kavu."
9and I went away unto the messenger, saying to him, `Give me the little scroll;` and he saith to me, `Take, and eat it up, and it shall make thy belly bitter, but in thy mouth it shall be sweet — as honey.`
9Basi, nikamwendea huyo malaika, nikamwambia anipe hicho kitabu kidogo. Naye akaniambia, "Kichukue, ukile; kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali, lakini tumboni kitakuwa kichungu!"
10And I took the little scroll out of the hand of the messenger, and did eat it up, and it was in my mouth as honey — sweet, and when I did eat it — my belly was made bitter;
10Basi, nikakichukua kitabu hicho kidogo kutoka mkononi mwa huyo malaika, nikakila; nacho kilikuwa kitamu kinywani mwangu kama asali, lakini nilipokimeza kikawa kichungu tumboni mwangu.
11and he saith to me, `It behoveth thee again to prophesy about peoples, and nations, and tongues, and kings — many.`
11Kisha nikaambiwa, "Inakubidi tena kutangaza ujumbe wa Mungu kuhusu watu wengi, mataifa, watu wa lugha nyingi na wafalme!"