Young`s Literal Translation

Swahili: New Testament

Revelation

9

1And the fifth messenger did sound, and I saw a star out of the heaven having fallen to the earth, and there was given to it the key of the pit of the abyss,
1Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu.
2and he did open the pit of the abyss, and there came up a smoke out of the pit as smoke of a great furnace, and darkened was the sun and the air, from the smoke of the pit.
2Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu.
3And out of the smoke came forth locusts to the earth, and there was given to them authority, as scorpions of the earth have authority,
3Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
4and it was said to them that they may not injure the grass of the earth, nor any green thing, nor any tree, but — the men only who have not the seal of God upon their foreheads,
4Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
5and it was given to them that they may not kill them, but that they may be tormented five months, and their torment [is] as the torment of a scorpion, when it may strike a man;
5Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
6and in those days shall men seek the death, and they shall not find it, and they shall desire to die, and the death shall flee from them.
6Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
7And the likenesses of the locusts [are] like to horses made ready to battle, and upon their heads as crowns like gold, and their faces as faces of men,
7Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8and they had hair as hair of women, and their teeth were as [those] of lions,
8Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9and they had breastplates as breastplates of iron, and the noise of their wings [is] as the noise of chariots of many horses running to battle;
9Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
10and they have tails like to scorpions, and stings were in their tails; and their authority [is] to injure men five months;
10Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
11and they have over them a king — the messenger of the abyss — a name [is] to him in Hebrew, Abaddon, and in the Greek he hath a name, Apollyon.
11Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi.
12The first wo did go forth, lo, there come yet two woes after these things.
12Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
13And the sixth messenger did sound, and I heard a voice out of the four horns of the altar of gold that is before God,
13Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
14saying to the sixth messenger who had the trumpet, `Loose the four messengers who are bound at the great river Euphrates;`
14Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, "Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!"
15and loosed were the four messengers, who have been made ready for the hour, and day, and month, and year, that they may kill the third of men;
15Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
16and the number of the forces of the horsemen [is] two myriads of myriads, and I heard the number of them.
16Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
17And thus I saw the horses in the vision, and those sitting upon them, having breastplates of fire, and jacinth, and brimstone; and the heads of the horses [are] as heads of lions, and out of their mouths proceedeth fire, and smoke, and brimstone;
17Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
18by these three were the third of men killed, from the fire, and from the smoke, and from the brimstone, that is proceeding out of their mouth,
18Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
19for their authorities are in their mouth, and in their tails, for their tails [are] like serpents, having heads, and with them they do injure;
19maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
20and the rest of men, who were not killed in these plagues, neither did reform from the works of their hands, that they may not bow before the demons, and idols, those of gold, and those of silver, and those of brass, and those of stone, and those of wood, that are neither able to see, nor to hear, nor to walk,
20Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
21yea they did not reform from their murders, nor from their sorceries, nor from their whoredoms, nor from their thefts.
21Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.