1And when he openeth the seventh seal, there came silence in the heaven about half-an-hour,
1Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
2and I saw the seven messengers who before God have stood, and there were given to them seven trumpets,
2Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
3and another messenger did come, and he stood at the altar, having a golden censer, and there was given to him much perfume, that he may give [it] to the prayers of all the saints upon the golden altar that [is] before the throne,
3Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
4and go up did the smoke of the perfumes to the prayers of the saints out of the hand of the messenger, before God;
4Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
5and the messenger took the censer, and did fill it out of the fire of the altar, and did cast [it] to the earth, and there came voices, and thunders, and lightnings, and an earthquake.
5Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
6And the seven messengers who are having the seven trumpets did prepare themselves that they may sound;
6Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
7and the first messenger did sound, and there came hail and fire, mingled with blood, and it was cast to the land, and the third of the trees was burnt up, and all the green grass was burnt up.
7Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
8And the second messenger did sound, and as it were a great mountain with fire burning was cast into the sea, and the third of the sea became blood,
8Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
9and die did the third of the creatures that [are] in the sea, those having life, and the third of the ships were destroyed.
9theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
10And the third messenger did sound, and there fell out of the heaven a great star, burning as a lamp, and it did fall upon the third of the rivers, and upon the fountains of waters,
10Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
11and the name of the star is called Wormwood, and the third of the waters doth become wormwood, and many of the men did die of the waters, because they were made bitter.
11(Nyota hiyo inaitwa "Uchungu.") Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
12And the fourth messenger did sound, and smitten was the third of the sun, and the third of the moon, and the third of the stars, that darkened may be the third of them, and that the day may not shine — the third of it, and the night in like manner.
12Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
13And I saw, and I heard one messenger, flying in the mid-heaven, saying with a great voice, `Wo, wo, wo, to those dwelling upon the land from the rest of the voices of the trumpet of the three messengers who are about to sound.`
13Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, "Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!"