Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

17

1YA anae guinen manmalofan inanaco Amfipolis yan Apolonia, manmato Tesalónica, anae guaja sinagogan Judios,
1Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2Ya si Pablo segun costumbreña, jumalom güije sija, ya tres sabado jaadingane sija ni y Tinigue.
2Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3Jadeclararayeja sija, na si Cristo nesesita ufamadese, ya ucajulo talo guinin y manmatae: ya este na Jesus ni y jusangane jamyo, güiya y Cristo.
3Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, "Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo."
4Ya palo guiya sija manmanjonggue, ya mandaña yan si Pablo yan Silas: yan y mandeboto na Griego un dangculon manada; ya ti didide na manmagas na famalaoan.
4Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5Lao y Judio sija pot y inigoñija, palo manaelaye na taotao gui mancanaya; ya mandaña un linajyan taotao jaatborota y siuda; ya maataca y guima Jason, ya maprocura manmaquecone sija juyong gui menan taotao.
5Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6Ya anae ti manmasoda, macone si Jason yan palo gui mañelo guato gui manmagas y siuda, ya managang ilegñija: Este yuje sija y munafanaatlibes y tano, ya manmato güine locue;
6Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: "Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7Ni y jaresibe si Jason; ya todo este sija cumocontra y tinago Sesat; ilegñija na guaja otro ray, si Jesus.
7Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu."
8Ya jaatborota todo y taotao yan y manmagas y siuda anae majungog este sija.
8Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9Ya anae manmañule segurida gui as Jason yan y pumalo, manmasotta.
9Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10¶ Ya anae puenge enseguidas matago ni y mañelo si Pablo yan Silas para Berea; ya anae manmato, manjalom gui sinagogan y Judios.
10Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11Este sija mas manmauleg qui ayo iya Tesalónica, sa rumesibe y sinangan contodo y minalagoñija, yan matataetae y Tinigue cada jaane, para umalie cao magajet ayo sija.
11Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12Enaomina megae guiya sija manmanjonggue; yan y manjulon locue na famalaoan Griego, yan y lalaje ti didide.
12Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13Lao y Judios Tesalónica anae jatungo na japredidica si Pablo y sinangan Yuus guiya Berea, manmato locue güije, ya manafangalamten yan manafaninestotba y linajyan taotao sija.
13Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14Ya enseguidas matago ni y mañelo si Pablo na ujanao asta y tase; lao si Silas yan Timoteo mañagaja güije.
14Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15Ya ayo y umadadaje si Pablo, macone asta Atenas; ya manresibe tinago para si Silas yan Timoteo, na ujalaguse guato guiya güiya, ya manmapos.
15Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16¶ Ya mientras manninanangga as Pablo guiya Atenas, calamten y espirituña gui sanjalomña anae jalie y siuda na bula y idolos.
16Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17Enaomina gui sinagoga jaadingane y Judio sija, yan y mandeboto na taotao sija, yan todo y asodaña gui plasa todo y jaane.
17Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18Ya palo ni y manmalate gui finanagüe y Epicureo yan Estoicosija, managuaguat yan güiya, ya palo ilegñija: Jafa cumequeilegña este na caducon cuicuentos? Otro palo ilegñija: Buente mannae notisia y nuebo na yuus; sa jasangane sija as Jesus, yan y quinajulo talo.
18Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, "Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?" Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, "Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni."
19Ya macone güe guato gui as Areopago, ilegñija. Siñajam intingo este y nuebo na finanagüe ni y unsasangan?
19Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, "Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20Sa uunafanmanjujungogjam ni y güinaja ni tatnae injingog, enaomina manmalagojam intingo jafa estesija.
20Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani."
21(Sa todo iya Atenas, yan y manaotao juyong ni y mañasaga güije, taya chechoñiñija na para ufanguentosja, yan para ufanecungog ni y nuebo na güinaja.)
21Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22Ayonae tumojgue si Pablo gui talo gui Areopago, ya ilegña; Jamyo ni y lalajen Atenas, julie na guefdeboto jamyo.
22Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, "Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23Sa anae malofanyo, ya juatan jafa y inadoranmimiyo, jusoda gui un attat este na tinigue: PARA Y TI MATUNGO NA YUUS. Ayo y inadodoraja ni y ti intingo; güiya jusangangane jamyo.
23Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24Si Yuus ni y fumatinas y tano yan todo y güinaja ni y mangaegue gui sumanjalomña; güiya Señot gui langet yan y tano, ti sumasaga gui templo ni y finatinas canae;
24Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25Ni umasetbe ni y canae taotao sija, taegüije y guaja janesesita; sa güiya mannae todo linâlâ, yan jinagong, yan todo y güinaja;
25Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26Ya güiya fumatinas unoja na jâgâ todo y nasion y taotao sija para ufañaga gui jilo y tano, jadetetmina tinancha y tiempoñija, yan y uttimon y saganñija;
26Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27Para ujaaligao y Señot, yaguin siña buente masiente ya umasoda güe, sa ti chago güe cada uno guiya jita.
27Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28Sa iya güiya nae utafanlâlâ yan utafangalamten, yan utafanguaja sustansiata; taegüije y palo gui poetan miyo, ilegñija: Sa jita locue y rasaña.
28Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29Yaguin jita y rasan Yuus, mungajit jumaso na y yiniusan Yuus parejo yan oro, pat salape, pat acho, pat y finatinas y jinason y taotao.
29Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30Ya ti jaconsidera si Yuus y tiempo anae manaetiningo; lao pago, manago na todo y taotao ufanmañotsot;
30Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31Sa jatancho un jaane, ni y anae para ujusga ni y tininas, y tano, ni ayo na taotao y jatago; ni y mannae testimonio todo y taotao, sa janacajulo guinin y manmatae.
31Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!"
32Ya anae jajungog sija y quinajulo talo guinin y manmatae, palo manmanbotlea; ya y palo ilegñija: Injingog jao talo otro biaje, pot este.
32Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, "Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!"
33Ya ayonae mapos si Pablo gui entaloñija.
33Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34Lao palo mandaña guiya güiya, manmanjonggue: ya y palo güije sija, si Dionisio, taotao Areopago, yan un palaoan na y naanña Dámaris, yan palo mangachongñiñija.
34Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.