Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

16

1YA mato güe locue Derbe yan Lystra: Ya estagüe, estaba güije un disipulo na y naanña si Timoteo, lajin un palaoan Judio, ni y manjonggue; lao y tataña Griego.
1Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
2Ya gosmauleg y famaña gui mañelo ni y mangaegue Lystra yan Iconio.
2Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
3Güiya malago Pablo na ujasija jumanao: ya quinene ya ninamasirconsida, sa pot y Judio sija ni y mangaegue güije na lugat: sa todoja tumungo na y tataña Griego.
3Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
4Ya anae jajanagüe todo y siuda sija, manmanae para ujaadaje, y tinago sija, ni y tinago y apostoles yan y manamco ni y mangaegue guiya Jerusalem.
4Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
5Ayonae y iglesia sija nae mumemetgot y jinenggue, ya lumalamegae y numero cada jaane.
5Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
6¶ Ya anae jajanagüe todo inanacon tanon Frygia, yan Galasia, ya manchinema ni y Espiritu Santo na ujapredica y sinangan guiya Asia;
6Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
7Ya anae manmato jijot y Misia, manmalago na ufanjanao para Bitinia: lao ti manpinelo ni y Espiritun Jesus na ufanjanao;
7Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
8Ya manmalofan oriyan Misia, ya manunog Troas.
8Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
9Ya anae puenge, jalie si Pablo un vision, na un taotao Masedonia, tumotojgue güije ya gumagagao güe ilegña: Mamaela mague guiya Masedonia ya unayudajam.
9Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: "Vuka, uje Makedonia ukatusaidie."
10Ya anae munjayan jalie y vision, enseguidas manmalagojam na manjanao para Masedonia, ya pinelonmame na y Señot umagangjam para inpredica y ibangelio guiya sija.
10Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
11¶ Ya anae mangagamajam guinin Troas, manmatojam gui tunas na chalan para Samotrasia, ya y inagpaña na jaane manmatojam Neapolis;
11Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
12Ya desde ayo asta Filipos, ni y mas dangculo na siuda güije na patte guiya Masedonia, yan un colonia romana: ya mañagajam güije na siuda unos cuantos na jaane.
12Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
13Ya y sabado na jaane, manjanaojam juyong gui siuda gui oriyan sadog, anae pinelonmame un lugat tinayuyut: ya manmatachongjam ya incuentuse y famalaoan sija ni y mandaña güije.
13Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
14Ya un palaoan na y naanña si Lydia, na manbebende purpura gui siudad Tiatira, ni y jaadodora si Yuus, jajungogjam; sa binaba y corasonña ni y Señot para uatituye y jasasangan si Pablo.
14Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
15Ya anae matagpange y palaoan, yan y guimaña, jagagaojam ilegña: Yaguin injisga na fiet yo gui Señot, fanjalom gui guimajo, ya infañaga güije. Ya jaafuetsasjam.
15Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, "Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae." Akatuhimiza twende.
16¶ Ya susede anae manjanaojam para lugat tinayuyut, na manasodajam yan un patgon na palaoan na gae espiritu Pitonico, ni y janafangana megae y amuña pot y manadibibina:
16Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
17Ya jadadalag si Pablo yan jame, ya umaagang ilegña: Este sija na taotao y tentago y Gueftaquilo na Yuus ni y fumanuejit ni y chalan y satbasion.
17Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, "Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu."
18Ya este finatinasña y palaoan megae na jaane. Lao si Pablo gosninaestotba ya jabira güe ya ilegña ni y espiritu: Jutago jao pot y naan Jesucristo na unjuyong guiya güiya. Ya jumuyong güijeja na ora.
18Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, "Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!" Mara huyo pepo akamtoka.
19¶ Ya anae jalie y amuña na mapos y ninanggaña para ufangana, maguut si Pablo yan Silas, ya macone guato gui plasa gui menan manmagas,
19Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
20Ya anae manmacone guato gui manmagas y lay, ilegña: Este sija na taotao. Judios ya jaatbororota y siudata,
20Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, "Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
21Ya manmamananagüe costumbre ni y ti combiene para jita na utaresibe, ni utaadaje, sa jita taotao Roma.
21Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata."
22Ya mangajulo y linajyan taotao ya mandaña contra sija: ya y manmagas sija jatiteg guiya sija y magaguñija, ya manmanago na ufanmasaulag.
22Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
23Ya anae esta megae na sinaulag ni y manmasaulagñija, manmapolo gui jalom calaboso, ya maencatga y atcaede na uguesadje sija.
23Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
24Ya ayo y rumesibe este na tinago, manpinelo sija guiya jalolom na calaboso, ya jaguesgode y adengñija gui sipo.
24Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
25Ya y tatalo puenge manaetae si Pablo yan Silas, yan jacantaye si Yuus alabansa sija: ya manjiningog ni ayo sija y manmaprereso.
25Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
26Ya derepente guaja güije un dangculon linao, ya asta y simienton y calaboso yinengyong: ya enseguidas manmababa todo y petta, ya todo y preso manmapula y guedenñija.
26Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
27Ya anae magmata y atcaede, ya jalie na mababa y pettan y calaboso, jalagnos y espadaña ya malago na upuno maesa güe, sa pineloña na manmalago y preso sija.
27Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
28Lao si Pablo umagang ni y dangculo na inagang, ilegña: Chamo munalalamen jao: sa estagüejamja todos.
28Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: "Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa."
29Ayonae mangagao candet sija, ya tumayog jalom, ya mato manlalaolao ni y minaañao, ya podong gui menan Pablo yan Silas,
29Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
30Ya jacone sija juyong, ya ilegña: Señores, jafa jufatinas para jusatbo?
30Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, "Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?"
31Ya sija ilegñija: Jenggue y Señot Jesus ya unsatbo yan y iya guimamo.
31Wao wakamjibu, "Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote."
32Ya masangane güe ni y sinangan y Señot, yan todo y mañasaga gui guimaña.
32Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
33Ya ayoja na ora gui puenge nae jacone ya jafagase y sinaulagñija: ya matagpange güe enseguidas yan todo y iyoña.
33Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
34Ya jacone sija guato gui guimaña ya japlantaye nañija gui menañija, ya ninasenmagof sa jajonggue si Yuus yan todo y iya guimaña.
34Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
35¶ Ya anae egaan na jaane, manmanago y manmagas sargento sija ilegñija: Setta ayo sija na taotao ya ufanjanao.
35Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, "Wafungueni wale watu."
36Ya y atcaede jasangane si Pablo ni este na sinangan, ilegña: Manmanago y manmagas na infanmasotta: ya pago fañuja ya infanjanao en pas.
36Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: "Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani."
37Lao si Pablo ilegña nu sija: Janafanmasaulagjam sin infanmaecungog, yan manmapresojam, ya taotao Roma jamja: ya pago inmanafanjuyong sin infanatungo? Aje: lao nafanmato ya sija unafanjuyongjam.
37Lakini Paulo alimjibu, "Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie."
38Ya y sargento sija jasangane y manmagas ni este na sinangan: ya ninafanmaañao anae jajungog na taotao Roma sija.
38Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
39Ya manmato ya manmagagao sija, ya anae manatanjuyong, manmagagao na ufanjuyong gui siuda.
39Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
40Ya anae manjuyong gui calaboso, manjalom gui guima Lydia; ya anae jalie y mañelo, jaconsuela ya manjanao.
40Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.