1AYONAE si Agripa ilegña as Pablo: Jupetmite jao na uncuentos pot jago namaesa. Ayonae si Pablo jaestira mona y canaeña ya manope pot güiya namaesa.
1Basi, Agripa akamwambia Paulo, "Unaruhusiwa kujitetea." Hapo Paulo alinyosha mkono wake akajitetea hivi:
2Magofyo ray, Agripa, sa jufanope pot guajo gui menamo pago na jaane, pot todo y mafaaelajo ni y Judio sija.
2"Mfalme Agripa, ninajiona mwenye bahati leo kujitetea mbele yako kuhusu yale mashtaka yote ambayo Wayahudi walikuwa wamesema juu yangu.
3Yan pot y jutungo na jago untungo todo y costumbre yan y finaesen gui entre y Judios; pot enaomina jutayuyut jao na con pasensiamo umaecungogyo.
3Hasa kwa vile wewe mwenyewe ni mtaalamu wa desturi za Wayahudi na migogoro yao, ninakuomba basi unisikilize kwa uvumilivu.
4Y jaanejo desde y pinatgonjo, ni y finenana gui entre y nasionjo yan guiya Jerusalem, todo y Judios tumungo.
4"Wayahudi wanajua habari za maisha yangu tangu utoto, jinsi nilivyoishi tangu mwanzo kati ya taifa langu huko Yerusalemu.
5Matungojayo desde y tutujonña, yaguin manmalago masangan, na taemanoja y mas tunas na secta y religionta, jumajanaoyo taegüije y Fariseo.
5Wananifahamu kwa muda mrefu, na wanaweza kushuhudia, kama wakipenda, kwamba tangu mwanzo niliishi kama mmoja wa kikundi chenye siasa kali zaidi katika dini yetu, yaani kikundi cha Mafarisayo.
6Ya pago, tumotojgueyo ya majus gayo pot y ninanggan y promesa ni y jafatinas si Yuus gui mañaenata.
6Na sasa niko hapa nihukumiwe kwa sababu ninaitumainia ile ahadi ambayo Mungu aliwaahidia babu zetu.
7Ni y manmaprometa y dose tribus, masestbeja si Yuus jaane yan puenge, mananangga na ufato. Ya pot ayo na ninangga ray Agripa, na mafaaelayo ni y Judio sija.
7Ahadi hiyo ndiyo ileile inayotumainiwa na makabila kumi na mawili ya taifa letu, wakimtumikia Mungu kwa dhati mchana na usiku. Mheshimiwa mfalme, Wayahudi wananishtaki kwa sababu ya tumaini hilo!
8Jaftaemano majusga y tijongguiyon entre jamyo, na si Yuus janacajulo y manmatae?
8Kwa nini ninyi mnaona shida sana kuamini kwamba Mungu huwafufua wafu?
9Guajo magajet na jujaso gui jinalomjo, na nesesitayo jufatinas megae contra y naan Jesus Nasareno.
9Kwa kweli mimi mwenyewe niliamini kwamba ni wajibu wangu kufanya mambo mengi kulipinga jina la Yesu wa Nazareti.
10Ya jufatinas este locue guiya Jerusalem; ya megae na mañantos jupreso, anae manresibeyo ninasiña guinin y magas mamale; ya anae para ufanmapuno, junae vosso contra sija.
10Mambo hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Mimi binafsi, nikiwa nimepewa mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu, nilipata kuwatia gerezani wengi wa watu wa Mungu. Nao walipohukumiwa kuuawa, nilipiga kura ya kukubali.
11Ya jucastiga sija gui sinagoga, ya juprocura na junafanman chatfino contra si Yuus; ya pot gogoslalaloyo contra sija, jupetsigue sija achogja asta otro siuda sija.
11Mara nyingi niliwafanya waadhibiwe katika masunagogi yote nikiwashurutisha waikane imani yao. Hasira yangu kwao ilikuwa kubwa hata nikawasaka mpaka miji ya mbali.
12Ya anae jumajanaoyo para Damasco yan y ninasiña guinin y magas mamale sija,
12"Kwa mujibu huohuo, nilikwenda Damasko wakati mmoja, nikiwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa makuhani wakuu.
13Y taloane, O ray, julie gui chalan y candet guinin y langet, na malagña qui y ininan y atdao, ya manina gui oriyajo yan ayo y mangachochongjo manjanao.
13Mheshimiwa, wakati nilipokuwa njiani, saa sita mchana, niliona mwanga mkubwa kuliko wa jua ukiangaza kutoka mbinguni, ukanizunguka mimi na wale wasafiri wenzangu.
14Ya anae mamodongjam todo gui jilo oda, jujungog y inagang na jacuentuseyo gui fino Hebreo, ilegña: Saulo, Saulo, jafa na unpetsisigueyo? mapot para jago y unfamateg contra y títuca.
14Sisi sote tulianguka chini, nami nikasikia sauti ikiniambia kwa Kiebrania: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa? Unajiumiza bure kama punda anayepiga teke fimbo ya bwana wake.
15Ya ilegco: Jaye jao Señot? ya ilegña: Guajo si Jesus ni y unpetsisigue.
15Mimi nikauliza: Ni nani wewe Bwana? Naye Bwana akajibu: Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
16Lao, cajulo ya untojgue; sa jufatoigüe jao pot este na jinaso, para junaministro jao yan untestigo ni este sija na güinaja y liniimo, yan ayo sija y pot y jufatoigüe jao;
16Haidhuru, inuka sasa; simama wima. Nimekutokea ili nikuweke rasmi kuwa mtumishi wangu. Utawathibitishia watu wengine mambo uliyoyaona leo na yale ambayo bado nitakuonyesha.
17Junalibre jao gui pueblo yan y Gentiles, ya pago junajanao jao para iya sija,
17Nitakuokoa na watu wa Israeli na watu wa mataifa mengine ambao mimi ninakutuma kwao.
18Para unbaba y atadogñija, yan unbira sija gui jemjom para y manana, yan y ninasiñan Satanas para as Yuus, ya ujaresibe y inasiin y isaoñija, yan erensia gui entalo ayo sija y manafangasgas pot y jinenggue ni y gaegue guiya guajo.
18Utayafumbua macho yao na kuwawezesha watoke gizani na kuingia katika mwanga; watoke katika utawala wa Shetani, wamgeukie Mungu; ili kwa kuamini, wapate kusamehewa dhambi na kuchukua nafasi yao kati ya wale ambao wamepata kuwa watu wa Mungu.
19Ya pot ayo, ti chatmatagoyo, O ray Agripa, para y vision y langet:
19"Hivyo, mfalme Agripa, sikuweza kuwa mkaidi kwa maono hilo la mbinguni.
20Lao jusangane finenana ayo sija y mangaegue Damasco, yan iya Jerusalem, yan todo y tano Judea, yan y Gentiles, na ufanmañotsot ya ujabira sija para as Yuus, yan ufanmachocho y chechoñija ni y para mañotsot.
20Ila nilianza kuhubiri kwanza kwa watu wa Damasko, halafu kwa wale wa Yerusalemu na nchi yote ya Yudea, na pia kwa watu wa mataifa mengine. Niliwahimiza wamgeukie Mungu na kuonyesha kwa vitendo kwamba wamebadilisha mioyo yao.
21Sa pot este sija na maconeyo ni y Judios gui guimayuus para jumapuno.
21Kwa sababu hiyo, Wayahudi walinikamata nikiwa Hekaluni, wakajaribu kuniua.
22Lao jatacayo y inayudan Yuus, ya jusisigueja asta pago na jaane, mannanaeyo testimonio parejoja y diquique yan y dangculo; taya jusasangan na ayo y ufato ni y sinangan Moises yan y proteta sija;
22Lakini Mungu alinisaidia; na hivyo mpaka siku ya leo nimesimama imara nikitoa ushuhuda kwa wote, wakubwa na wadogo. Ninayosema ni yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia;
23Na si Cristo, nesesitagüe ufamadese, ya güiya ufinenana, pot ucajulo guinin y manmatae, ufannae candet gui pueblo yan y Gentiles.
23yaani ilimpasa Kristo ateseke na kuwa wa kwanza kufufuka kutoka wafu, ili atangaze kwamba mwanga wa ukombozi unawaangazia sasa watu wote, Wayahudi na pia watu wa mataifa mengine."
24¶ Ya anae cumuecuentos, umagang si Festo ni y dangculo na inagangña, ilegña: Caduco jao Pablo: megae na tiningo ninacaduco jao.
24Paulo alipofika hapa katika kujitetea kwake, Festo alisema kwa sauti kubwa, "Paulo! Una wazimu! Kusoma kwako kwingi kunakutia wazimu!"
25Lao si Pablo ilegña: Ti caducoyo Festo; lao jusasangan y sinangan ni y magajet yan y tinas.
25Lakini Paulo akasema, "Sina wazimu mheshimiwa Festo: Ninachosema ni ukweli mtupu.
26Sa y ray jatungoja estesija, cumuentosyoja gui menaña locue libre; sa seguroyo na taya güine sija na güinaja umanaatog guiya güiya; sa estesija, ti manmafatinas gui rincon.
26Wewe Mfalme unayafahamu mambo haya, kwa hiyo ninaweza kuongea bila uoga mbele yako. Sina mashaka kwamba matukio hayo yanajulikana kwako maana jambo hili halikutendeka mafichoni.
27Ray Agripa, unjonggue y profeta sija? jutungo na unjonggue.
27Mfalme Agripa, je, una imani na manabii? Najua kwamba unaamini."
28Ayonae si Agripa ilegña as Pablo, Canaja unnamamañañayo para juquilisyano.
28Agripa akamjibu Paulo, "Kidogo tu utanifanya Mkristo!"
29Ya si Pablo ilegña. Malagoyo as Yuus, na ti jagoja, lao todo ayo sija y jumungogyo pago na jaane, ufantaegüine iya guajo, fuera di y mapresujo.
29Paulo akamjibu, "Namwomba Mungu kwamba, kwa muda mfupi au mrefu, si wewe tu bali wote wanaonisikia leo wapate kuwa kama nilivyo mimi, lakini bila hii minyororo."
30¶ Ya anae munjayan jasangan este, cumajulo y ray yan y magalaje, yan Bernise, yan ayo sija y mangachongñiñija manmatachong.
30Hapo mfalme Agripa, mkuu wa mkoa, Bernike na wale wote waliokuwa pamoja nao, walisimama.
31Ya anae mañuja, manguentos uno yan y otro, ilegñija: Taya finatinasña este na taotao, na jamerese y finatae, pat umapreso.
31Walipokwisha ondoka, waliambiana, "Mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo au kifungo."
32Ayonae ilegña si Agripa as Festo: Este na taotao, umanalibre, yaguin ti jagagao jinisgaña gui as Sesat.
32Naye Agripa akamwambia Festo, "Mtu huyu angeweza kufunguliwa kama asingalikuwa amekata rufani kwa Kaisari."