Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

27

1YA anae esta majasuye na para infanmaudae gui batco para Italia, maentrega si Pablo, yan otro manpreso gui uno na y naanña si Julio, senturion gui sendalon Augusto.
1Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho "Kikosi cha Augusto."
2Ya anae manjalomjam gui batcon Adrumeto, comoque janao para y costan Asia, manjanaojam; ya manjajame yan un Aristarcho, taotao Masedonio na sagaña Tesalónica.
2Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3Ya y inagpaña na jaane, manmatojam Sidon: ya si Julio jagosgüaeya si Pablo, ya janae linibre na ujanao para y manamiguña para unamagof güe.
3Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4Ya mamaudaejam gui batco manlayagjam papa jijot Chipre, desde ayo, sa y manglo contra.
4Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5Ya anae manjanaojam gui tasen jijot Silisia yan Pamfilia, manmatojam Mira, gui siudad Lisia.
5Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6Ya jasoda güije y senturion un batcon Alejandria, na jumajanao para Italia; ya janafanjalomjam.
6Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7Ya manmaudaejam gui batco megae na jaane, sa mumayayama senñateng, yan canaja ti manmatojam guato Gnido, ti japolojam y manglo, ya manmayama jijot papa Creta, guiya Salmon;
7Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8Ya gosmapot manmalofanjam umoriya inanaco güije na tase, manmatojam gui un lugat na mafanaan Bonito-Puerto, na jijot gui siuda Lasea.
8Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo "Bandari Nzuri", karibu na mji wa Lasea.
9¶ Ya anae megae na tiempo malofan, ya senpiligro y jinanaomame, sa y Ayunat esta malofan, ya si Pablo mansinangane sija,
9Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10Ya ilegña nu sija: Señores, julie na este na jinanao, guaja uninalamen yan megae uninafanaelaye, ya ti y catgaja yan y batco, lao asta y jaanita locue.
10"Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu."
11Lao y senturion, jajonggueñaja y magas batco yan y gaeiyo y batco, qui ayo sija y sinangan Pablo.
11Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12Sa taya puerto nae siña para ufañaga y tiempon manenggeng, ya mas megae majaso na ufanmalofan güije gui tase locue, para ujaquelie jaftaemano nae siña manmato Fenix, ya ayo nae ufañaga güije y tiempon manenggeng, gui puerton Creta, ni y jadalalalaque y sanjaya gui sanlichan yan y sanlago gui sanlichan.
12Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13Ya anae manguaefe didide y manglo sanjaya, pinelonñija na ujataca y malagoñija, jadingo ayo ya manjanao guato oriyan Creta.
13Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14Lao despues ti apmam na tiempo cajulo un dangculon manglo contra y batco, na mafanaan Euroclydon;
14Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao "Upepo wa Kaskazi" ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15Ya tinemba y batco ya tisiña injanao contra y manglo, inpelo na umachule ni y manglo.
15Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16Ya malago asta y papa un isla na mafanaan Clauda, ya megae y chechomame pot y bote.
16Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17Ni y anae manmajatsa julo, ya manmaayuda, magode y batco gui sampapa; ya manmaañao na umayute gui Sirte, manatunog y layag ya ayonae manmachule ni y manglo.
17Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18Ya janafangoschatsagajam y pinagyo, ya y inagpaña na jaane, jayute gui tase y catga, manachadeg y batco,
18Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19Ya y mina tres na jaane, inyite juyong ni y canaemameja y güinajan y batco.
19Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20Ya megae na jaane na ti anog y atdao, ni y pution sija, ya ti didide na pagyo mato guiya jame, ya todo y ninangganmamame na infansatbo, malingo.
20Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21Lao despues di apmam na timañocho, tumojgue si Pablo gui entaloñija ya ilegña: Señores, yaguin inecungogyo, ti tadingo Creta para tagana este na ninalamen yan minalingo.
21Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, "Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22Lao pago juencatga jamyo na namauleg y inangoconmiyo; sa taya ni un taotao gui entre jamyo ufalingo y linâlâña, na y batcoja.
22Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23Sa tumotojgue gui oriyajo pago na puenge y angjet Yuus, ni y jayeyo, yan jaye y jusetbe.
23Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24Ya ilegña: Chamo maaañao Pablo; sa nesesita unmacone guato gui menan Sesat; ya estagüeja na ninae jao as Yuus ni ayo sija y mangachochongmo gui batco.
24akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25Enaomina señores, namauleg y inangoconmiyo; sa jujonggue na si Yuus, utaegüijeja y esta jasanganeyo.
25Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26Lao nesesita tayutejit gui jilo un isla.
26Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani."
27¶ Ya anae mato y mina catorse na puenge, taegüigüijeja jachuchulejajam papa yan julo tasen Adratico, ya y buente tatalopuenge, jinasonñija y marinero sija na esta manjijot gui un tano.
27Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28Ya masondalea, ya masoda biente brasa; ya anae manjanao didide mona, masondalea talo, ya masoda quinse brasa.
28Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29Ayonae manmaañaojam, na nosea infanbasnag gui jilo y acho, ya mayute cuatro na angcla juyong gui popa, ya madesesea na umanana.
29Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30Ya y marinero cumequefanmalago gui batco anae esta manatunog y bote gui tase, ya jinasonñija na siña ujayute y angcla gui proa.
30Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31Ya si Pablo ilegña ni y senturion yan y sendalo sija: Yaguin ti mañaga estesija gui batco, ti siña jamyo mansatbo.
31Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, "Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka."
32Ayonae y sendalo sija, jautot y tale todo gui bote, ya jasotta na upodong.
32Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33Ya anae manana, si Pablo jagagao sija todos na ujafañocho, ilegña: Este y mina catorse na jaane ni y tanananggaja, sisiguejajit di manayunat, ti mañochojit ni jafa.
33Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: "Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34Enaomina jutatayuyut jamyo na infañocho, sa este para linâlâmiyo: sa ni uno gui gapon ulonmiyo ufalingo guiya jamyo.
34Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea."
35Ya anae munjayan jasangan este, jachule y pan ya janae grasia si Yuus gui menañija todos: ya anae jaipe, jatutujon cumano.
35Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36Ya ayo todo sija y manmauleg minagofñija, mañocho locue.
36Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37Ya jame todos ni y manestaba gui batco, dosientos setenta y saes na taotao sija.
37Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38Ya anae manjaspog, manañajlalang y batco, ya mayute y trigo gui jalom tase.
38Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39Ya anae manana, ti matungo y tano: lao masoda un diquique na sadog na guaja oriyaña; ya jinasoñija na ujanajalom y batco.
39Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40Ya anae manmajatsa y angcla ya masotta gui tase, ya manmapula y tale y timon, ya jajatsa y layag para y manglo, ya jatutujon manjanao para y oriyan tase.
40Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41Ya podong gui jalom un lugat anae umasoda y dos tase, ya malago y batco gui jilo tano; ya y sanmena na patte cheton, ya sumagaja ti siña calamten, lao y santate na patte mayamag ni y finijom y napo sija.
41Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42Ya manatungo y sendalo sija, na ujapuno todo y preso sija, na nosea uguaja guiya sija tumungo numango ya uescapa.
42Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43Lao y senturion malago na unasatbo si Pablo, ya jaadaje sija gui jinasoñija; ya manago na y siña numango uyute sija finena gui tase, ya ujafanjanao para y tano.
43Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44Ya y manetejnan, palo gui jilo tabbla, yan palo gui pidason mayamag batco, ya taegüenao nae manmalofan, ya todo sija mansatbo ya manescapa seguro para y tano.
44na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.