Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

28

1YA anae manescapa esta, ayonae matungo na y isla naanña Melita.
1Tulipokwisha fika salama kwenye nchi kavu, tuligundua kwamba kile kisiwa kinaitwa Malta.
2Ya y taotao ti mangilisyano, jafamaulegjam: sa manmanotne guafe ya jaresibejam cada uno, sa pot y ichan, yan y manenggeng.
2Wenyeji wa hapo walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inaanza kunyesha na kulikuwa na baridi, hivyo waliwasha moto, wakatukaribisha.
3Ya anae janafandaña si Pablo y palitun jayo, ya jamanojo ya japolo gui jilo y guate, jumuyong un vibora guinin y maipe, ya cheton gui canaeña.
3Paulo aliokota mzigo mdogo wa kuni akawa anazitia motoni. Hapo, kwa sababu ya lile joto la moto, nyoka akatoka katika kuni akamnasa Paulo mkononi na kujishikilia hapo.
4Ya anae malie ni y taotao ti mangilisyano y beneno na gâgâ na umacalaye gui canaeña, manasangane ilegñija: Este na taotao pegno, masqueseaja umescapa gui tase; lao ti upinelo ni y inenog na ulâlâ.
4Wenyeji wa pale walipokiona kile kiumbe kinaning'inia kwenye mkono wake waliambiana, "Bila shaka mtu huyu amekwisha ua mtu, na ingawa ameokoka kuangamia baharini, Haki haitamwacha aendelee kuishi!"
5Ya jasacude y gâgâ guato gui jalom guafe, ya ti ninalamen.
5Lakini Paulo alikikung'utia kile kiumbe motoni na hakuumizwa hata kidogo.
6Ya mataaatanja cao uninapogpog, pat upodong enseguidas ya umatae; lao anae esta laapmam na maatan, ya malie na ti ninalamen, jatulaeca y jinasoñija, ya ilegñija na yuus güe.
6Wale watu walikuwa wakitazamia kwamba angevimba au hapohapo angeanguka chini na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu bila kuona kwamba Paulo amepatwa na jambo lolote lisilo la kawaida, walibadilisha fikira zao juu yake, wakasema kuwa ni mungu.
7¶ Ayo na lugat, guaja fangualuanña sija y magas y isla, na y naanña si Publio; ni y rumesibejam, ya janafañagajam tres na jaane.
7Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya Publio, mkuu wa kile kisiwa. Publio alitukaribisha kirafiki, tukawa wageni wake kwa siku tatu.
8Ya y tatan Publio estaba na umaason sa malango calentura, yan jinaga: ya jumalom si Pablo, ya anae munjayan manaetae, japolo y canaeña gui jilo y malango, ya janajomlo.
8Basi, ikawa kwamba baba yake Publio alikuwa amelala kitandani, mgonjwa, ana homa na kuhara. Paulo alikwenda kumwona na baada ya kusali, akaweka mikono yake juu ya mgonjwa, akamponya.
9Ya anae munjayan este, y palo locue gui isla ni y guaja chetnotñija, manmato ya uninafanjomlo.
9Kutokana na tukio hilo, wagonjwa wote katika kile kisiwa walikuja wakaponywa.
10Ya gosmegae manmatunanmame; ya anae majanaojam, manmacatgayejam ni ayo sija y innesesita,
10Watu walitupatia zawadi mbalimbali na wakati tulipoanza tena safari, walitia ndani ya meli masurufu tuliyohitaji.
11¶ Ya anae malofan tres meses, manjanaojam gui un batco Alejandrina, ni y estaba gui isla na mannanangga na ufalofan y tiempon manenggeng, na y señatña Castor yan Polux.
11Baada ya miezi mitatu tulianza tena safari yetu kwa meli moja ya Aleksandria iitwayo "Miungu Pacha". Meli hiyo ilikuwa imetia nanga kisiwani wakati wote wa baridi.
12Ya anae manmatojam Siracusa, mañagajam güije tres na jaane.
12Tulifika katika mji wa Sirakusa, tukakaa hapo kwa siku tatu.
13Ya desde ayo manoriyajam, ya manmatojam guiya Regio; ya anae malofan un jaane na manguaefe y manglo sanjaya, manmatojam guiya Puteoli gui inagpaña.
13Toka huko tuling'oa nanga, tukazunguka na kufika Regio. Baada ya siku moja, upepo ulianza kuvuma kutoka kusini, na baada ya siku mbili tulifika bandari ya Potioli.
14Ya manmañodajam mañelumame güije, ya manmalago na infañaga ya infanjame siete na jaane; ya ayonae infanmalag Roma.
14Huko tuliwakuta ndugu kadhaa ambao walituomba tukae nao kwa juma moja. Hivi ndivyo tulivyopata kufika Roma.
15Ya desde ayo, anae manmajungogjam ni y mañelunmame, manmato para ujatagamjam, asta y Metcadon Appio, yan y Tres Taberna; ni y anae jalie si Pablo, janae grasia si Yuus, ya jaangoco.
15Ndugu wa kule Roma walipopata habari zetu, wakaja kutulaki kwenye soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akapata moyo.
16¶ Ya anae manmatojam Roma, y senturuon jaentrega y preso sija gui magas y guatdia: lao si Pablo mapolo na usaga namaesa yan un sendalo ni y umadadaje güe.
16Tulipofika Roma, Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake pamoja na askari mmoja wa kumlinda.
17Ya susede anae malofan tres na jaane, jaagang si Pablo y manmagas y Judio sija; ya anae manmato ya mandaña, ilegña nu sija: Guajo mañelujo lalaje, achogja taya finatinaso contra y taotao sija, ni contra y costumbren y mañaenata jumaentrega preso desde Jerusalem asta y canae y taotao Roma:
17Baada ya siku tatu, Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiyahudi wa mahali hapo. Walipokusanyika, Paulo aliwaambia, "Wananchi wenzangu, mimi, ingawa sikufanya chochote kibaya wala kupinga desturi za wazee wetu, nilitiwa nguvuni kule Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.
18Ni y para yaguin munjayan maegsaminayo, manmalago na jumasotta, sa taya jafa finatinaso para jumapuno.
18Waliponihoji na kuona kwamba sikuwa na hatia yeyote, walitaka kuniacha.
19Lao anae macontra ni y Judio sija, nesesitayo na jugagao jinisga gui as Sesat; ti pot para jufaaela y nasionjo.
19Lakini Wayahudi wengine walipinga jambo hilo, nami nikalazimika kukata rufani kwa Kaisari, ingawa sikuwa na chochote cha kuwashtaki wananchi wenzangu.
20Ya pot este rason juagang jamyo, para julie jamyo, yan para utafanguentos: sa pot y ninanggan Israel na magodeyo ni este na cadena.
20Ni kwa sababu hiyo nimeomba kuonana na kuongea nanyi, maana nimefungwa minyororo hii kwa sababu ya tumaini lile la Israeli."
21Ya ilegñija nu güiya: Jame taya rinesibenmame carta guiya Judea pot jago, ni uno gui mañelo ni y manmato, cumuentos pat manmañangane jafa pot jago.
21Wao wakamwambia, "Sisi hatujapokea barua yoyote kutoka Yudea, wala hakuna ndugu yeyote aliyefika hapa na kutoa habari rasmi au kusema chochote kibaya juu yako.
22Lao manmalagojam na injingog jao, jafa jinasosomo; sa este na secta, intingoja na masqueseaja mano guato masangan contra.
22Lakini tunafikiri inafaa tusikie kutoka kwako mwenyewe mambo yaliyo kichwani mwako. Kwa maana tujualo sisi kuhusu hicho kikundi ni kwamba kinapingwa kila mahali."
23¶ Ya anae esta matanchue un jaane, manmato megae guiya güiya, gui sagaña; ya jasangane yan janamatungo y raenon Yuus: janafanmañaña sija pot si Jesus, yan pot y tinago Moises, yan pot y profeta sija; desde y egaan asta y pupuenge.
23Basi, walipanga naye siku kamili ya kukutana, na wengi wakafika huko alikokuwa anakaa. Tangu asubuhi mpaka jioni Paulo aliwaeleza na kuwafafanulia juu ya Ufalme wa Mungu akijaribu kuwafanya wakubali habari juu ya Yesu kwa kutumia Sheria ya Mose na maandiko ya manabii.
24Ya palo, manmanjonggue ni y sinangan, palo ti manmanjonggue.
24Baadhi yao walikubali maneno yake, lakini wengine hawakuamini.
25Ya anae ti unoja corasonñija, manjanao anae munjayan jasangan si Pablo un sinangan: Mauleg sinanganña y Espiritu Santo pot y profeta Isaias gui mañaenata,
25Basi, kukawa na mtengano wa fikira kati yao. Walipokuwa wanakwenda zao, Paulo alisema jambo hili, "Kweli ni sawa yale aliyoyanena Roho Mtakatifu kwa wazee wenu kwa njia ya nabii Isaya
26Ilegña: Janao fanmalag este sija na taotao, ya inalog, Inecungog, ya injingog, ya ti incomprende; ya y inquelie, inlie, ya ti intingo.
26akisema: Nenda kwa watu hawa ukawaambie: kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
27Sa y corason este sija na taotao, manmajetog, ya y talanganñija mapot manmanjungog, ya jajuchom y atadogñija; sa noseaja ufanmanlie ni y atadogñija, yan ufanmanjungog ni y talanganñija, yan ujatungo ni y corasonñija, ya ufanmañotsot, ya janafanjomlo sija.
27Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameziba masikio yao, wamefumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao. Wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya."
28Enaomina tingo na y este satbasion gui as Yuus manajanao para y Gentiles sija; ya sija ujajungog.
28Halafu Paulo akamaliza na kusema, "Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!"
29(Ya anae munjayan jasangan este sija na sinangan, manjanao y Judio sija, ya gueguesmanafaesen entre sija;)
29Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.
30Ya si Pablo sumaga dos años gui inatquilaña na guma; ya jaresibe todo ayo sija y manmato guiya güiya,
30Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.
31Japredidica y raenon Yuus, yan mamananagüe ni ayo sija y pot y Señot Jesucristo, contodo y linibriña, ya taya ni un taotao chumoma.
31Alikuwa akihubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.