Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Acts

7

1AYONAE ilegña y magas mamale: Taegüine este sija?
1Basi, Kuhani Mkuu akamwuliza, "Je, mambo haya ni kweli?"
2Ya güiya ilegña: Mañelujo lalaje yan mañaena, ecungog. Si Yuus y minalag fumatoigüe y tatata as Abraham anae estatabaja guiya Mesopotamia, antes di usaga Charran.
2Naye Stefano akasema, "Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
3Ya ilegña nu güiya: Suja gui tanomo yan y manparientesmo, ya maela jalom gui tano ni y finanuejo nu jago.
3Mungu alimwambia: Ondoka katika nchi yako; waache watu wa ukoo wako; nenda katika nchi nitakayokuonyesha!
4Ya güiya jumanao juyong gui tano y Chaldeosija, ya sumaga Charran: ya desde ayo, anae matae si tataña, ninamalofangüe as Yuus güine mague na tano anae mañasaga jamyo pago.
4Kwa hivyo, Abrahamu alihama nchi ya Kaldayo, akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu alimtoa tena Harani akaja kukaa katika nchi hii mnayokaa sasa.
5Ya ti ninae güe jafa na erensiaña güije, aje, taya ni para upolo y adengña gui jiloña: lao prinemete güe na uninae para güinajaña, yan y semiyaña despues di güiya, sa güiyaja trabia tataepatgon.
5Mungu hakumpa hata sehemu moja ya nchi hii iwe mali yake; hata hivyo, alimwahidia kumpa nchi hii iwe yake na ya wazawa wake, ingawaje wakati huu hakuwa na mtoto.
6Ya si Yuus jasangan taegüine, Na y semiyaña utaotao juyong gui ti tanoña; yan manmacone ya manmancautiba, ya manmatrata taelaye cuatro sientes años.
6Mungu alimwambia hivi: Wazao wako watapelekwa katika nchi inayotawaliwa na watu wengine, na huko watafanywa watumwa na kutendewa vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
7Ya y nasion ni y manmancautiba, bae jujusga, ilegña si Yuus; na despues di ayo, ufanmamaela juyong ya guajo jumasetbe güine na lugat.
7Lakini mimi nitalihukumu taifa hilo litakalowafanya watumwa. Kisha nitawatoa katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.
8Yan manae güe ni y traton sirconsision: ya si Abraham jalilis si Ysaac, ya masirconsida güe gui mina ocho na jaane; ya si Ysaac jalilis si Jacob; ya si Jacob jalilis y dose na patriarcasija.
8Halafu Mungu aliifanya tohara iwe ishara ya agano. Hivyo, Abrahamu alimtahiri mtoto wake Isaka, siku ya nane baada ya kuzaliwa. Na Isaka, vivyo hivyo, alimtahiri Yakobo. Naye Yakobo aliwatendea wale mababu kumi na wawili vivyo hivyo.
9Ya y patriarca sija pot y inigoñija, mabende si José guiya Egipto: lao si Yuus estaba guiya güiya,
9"Wale mababu walimwonea wivu Yosefu, wakamuuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,
10Ya ninalibre güe todo gui chinatsaga, yan ninae güe finaborese yan tiningo, gui menan Faraon, ray guiya Egipto; yan ninamagalaje güe guiya Egipto, yan todo y guimaña.
10akamwokoa katika taabu zake zote. Mungu alimjalia fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri, hata Farao akamweka awe mkuu wa ile nchi na nyumba ya kifalme.
11Ayonae mato niñalang todo gui tano Egipto yan Charran, yan dangculon chinatsaga: ya y mañaenata ti manmañoda nengcanoñija.
11Kisha, kulizuka njaa kubwa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa. Babu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.
12Lao anae si Jacob jajungog na guaja trigo guiya Egipto, jatago y mañaenata finenana na biaje.
12Basi, Yakobo alipopata habari kwamba huko Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma watoto wake, yaani babu zetu, waende huko Misri mara ya kwanza.
13Ya y mina dos biaje, matungo si José ni y mañeluña: ya y parientes José janatungo si Faraon.
13Katika safari yao ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, na Farao akaifahamu jamaa ya Yosefu.
14Ya manago si José na umaagange si tataña as Jacob para iya güiya, yan todo y manparientesña, setentaisinco na taotao.
14Yosefu alituma ujumbe kwa baba yake na jamaa yote, jumla watu sabini na tano, waje Misri.
15Ya si Jacob jumanao papa Egipto, ya matae güije yan y mañaenata sija.
15Hivyo, Yakobo alikwenda Misri ambako yeye na babu zetu wengine walikufa.
16Ya manmachule guato Siquem, ya manmapolo gui naftan, ni y finajan Abraham pot salape, gui famaguon Emmor guiya Siquem.
16Miili yao ililetwa mpaka Shekemu, ikazikwa katika kaburi Abrahamu alilonunua kutoka kwa kabila la Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
17Lao anae esta jijot y tiempon y promesa, ni y si Yuus manjula as Abraham, ya y taotao lumamegae, yan manlajyan guiya Egipto,
17"Wakati ulipotimia Mungu aitimize ahadi aliyompa Abrahamu, idadi ya wale watu kule Misri ilikwisha ongezeka na kuwa kubwa zaidi.
18Asta qui y otro ray cajulo, ya ti jatungo si José.
18Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.
19Este jausa y malamañaña gui manparientesta, yan jatrata taelaye y mañaenata, sa janafanmayute y famaguonñija ni y pago finañago para chañija fanlalâlâ.
19Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.
20Ya ayo na tiempo nae mafañago si Moises, ya sumenbonito; ya mapogsae gui guima tataña tres meses.
20Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,
21Ya anae mayute, y jagan Faraon jumoca, ya pinegsae para lajiña.
21na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.
22Ya si Moises, maeyag ni y todo y tiningo y taotao Egipto, ya mangaeninasiñaña y finoña yan y chechoña sija.
22Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.
23Ya anae cana jacumple cuarenta años y sacaña, mato gui corasonña na ubisita y mañeluña ni y famaguon Israel.
23"Alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.
24Ya jalie uno guiya sija ni y japadese y maltrato, ya jadefiende y mumatrata, ya japuno y taotao Egipto.
24Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri.
25Sa pineluña na jatungo y mañeluña na uninafanlibre as Yuus ni y canaeña; lao ti jatungo sija.
25(Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo.)
26Ya y inagpaña na jaane, jafanue sija nu güiya anae managuaguat, ya malago na unaunoja talo sija, ilegña: Señores, jamyo mañelo; jafa na mananataelaye y uno yan y otro?
26Kesho yake, aliwaona Waisraeli wawili wakipigana, akajaribu kuwapatanisha, akisema: Ninyi ni ndugu; kwa nini basi, kutendeana vibaya ninyi kwa ninyi?
27Lao ayo y minalalamen y tiguangña, jachonegñaejon, ilegña: Jaye munamagas jao gui jilo mame?
27Yule aliyekuwa anampiga mwenzake alimsukuma Mose kando akisema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wa watu?
28Malago jao unpunoyo taegüije anae unpuno nigap y taotao Egipto?
28Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?
29Ya ninafalago si Moises ni este na sinangan, ya tumaotao juyong gui tano Madian, gui anae jalilis y dos na lajiña.
29Baada ya kusikia hayo Mose alikimbia, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani na huko akapata watoto wawili.
30Ya anae jacumple cuarenta años, mato guiya güiya un angjet gui jalomtano gui egso Sinae, gui mañila y guafe gui jalom y trongcon chaguan.
30"Miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana alimtokea Mose katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto kule jangwani karibu na mlima Sinai.
31Ya anae jalie ayo si Moises, ninagosmanman ni y liniiña; ya anae lumajijot para ugueslie, y inagang y Señot mato guiya güiya,
31Mose alistaajabu sana kuona jambo hilo hata akasogea karibu ili achungulie; lakini alisikia sauti ya Bwana:
32Ilegña: Guajo y Yuus y mañaenamo, y Yuus Abraham, yan y Yuus Ysaac, yan y Yuus Jacob. Lao si Moises manlalaolao, ya ti siña jaatan.
32Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Mose akatetemeka kwa hofu na wala hakuthubutu kutazama zaidi.
33Ya y Señot ilegña nu güiya: Pula y sapatosmo gui adengmo; sa y lugat anae tumotojgue jao, santos na oda.
33Bwana akamwambia: Vua viatu vyako maana hapa unaposimama ni mahali patakatifu.
34Sa seguro julie, y manmasapet y taotaojo guiya Egipto, yan jujungog y inigongñiñija, ya tumunogyo para junafanlibre sija. Ya pago maela jao, sa jutago jao guato Egipto.
34Nimeyaona mabaya wanayotendewa watu wangu kule Misri. Nimesikia kilio chao, nami nimekuja kuwaokoa. Basi sasa, nitakutuma Misri.
35Este y as Moises ni y jarechasa ilegñija: Jaye munamagas jao yan unjues? Güiya tinago as Yuus na umagas yan uninafanlibre pot y canae y angjet ni y mafato guiya güiya gui jalomtano.
35"Huyu Mose ndiye yule watu wa Israeli waliyemkataa waliposema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wetu? Kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto, Mungu alimtuma Mose huyo awe kiongozi na mkombozi.
36Güiya chumule sija juyong, ya despues manfinanue ni y namanman, yan señat sija gui tano Egipto, yan y Tasen Agaga, yan y jalomtano cuarenta anos.
36Ndiye aliyewaongoza wale watu watoke Misri kwa kufanya miujiza na maajabu katika nchi ya Misri, katika bahari ya Shamu na jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
37Este ayo y as Moises, ni y ilegña ni y famaguon Israel: Y Yuusmiyo janacajulo un profeta guiya jamyo gui mañelunmiyo taegüine iya guajo.
37Mose ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: Mungu atawateulieni nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu ninyi wenyewe.
38Este ayo y estaba gui inetnon, gui jalomtano, yan y angjet ni y cumuentuse güe gui egso Sinae, yan y mañaenata; ni y rumesibe y nalâlâ na tinago para ufanmanaejit.
38Wakati watu wa Israeli walipokutana pamoja kule jangwani, Mose ndiye aliyekuwako huko pamoja nao. Alikuwa huko pamoja na babu zetu na yule malaika aliyeongea naye mlimani Sinai; ndiye aliyekabidhiwa yale maneno yaletayo uzima atupe sisi.
39Ni y mañaenata ti manmalago jaosgue lao mayute juyong guiya sija, ya y corasonñija manalo tate Egipto,
39"Lakini yeye ndiye babu zetu waliyemkataa kumsikiliza; walimsukuma kando, wakatamani kurudi Misri.
40Ilegñija as Aaron: Fatinasejam Yuus para ujanao gui menanmame, as este y as Moises ni y cumonejam juyong gui tano Egipto, ti intingo jafa ujuyong.
40Walimwambia Aroni: Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata Mose huyu aliyetuongoza kutoka Misri!
41Ya sija manmamatinas un tatnero, ya machule y inefrese para idolo sija, güije sija na jaane, ya ninafansenmagof ni y checho y canaeñija.
41Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.
42Ayonae jabira si Yuus, ya japolo na ujaadora y inetnon y langet; taegüije esta matugue gui leblon y profeta: O jamyo ni y guima Israel, inofreseyo pinino gâgâ sija yan inefrese sija gui cuarenta años gui jalomtano?
42Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii: Enyi watu wa Israeli! Si mimi mliyenitolea dhabihu na sadaka kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani!
43Yan injatsa y tabemaculon Moloc, yan y estreyas y Yuus Refán, jechura sija ni y infatinas para inadora sija; ya guajo juchule jamyo mas chago qui Babilonia.
43Ninyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki, na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu. Kwa sababu hiyo nitakupeleka mateka mbali kupita Babuloni!
44Y mañaenata, guaja ni y tabernaculon y testimonio gui jalomtano, taegüije tinanchoña ni ilegña as Moises na ufatinas taemanoja na jechura y liniiña.
44Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema lililoshuhudia kuweko kwa Mungu. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichoonyeshwa.
45Ni y mañaenata locue gui tiempoñija a machule jalom yan si Josué anae jumalom gui erensian y Gentiles, ni y si Yuus yumute juyong gui menan y mañaenata, asta y jaanen David;
45Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.
46Ni y sumoda finaborese gui menan Yuus, yan jagagao na ualiligao tabernaculo para si Yuus Jacob.
46Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.
47Lao si Salomon fumatinase güe un guma.
47Lakini Solomoni ndiye aliyemjengea Mungu nyumba.
48Sa y Gueftaquilo, ti sumasaga gui guima sija ni y finatinas canae; taegüije y sinangan y profeta.
48"Hata hivyo, Mungu Mkuu haishi katika nyumba zilizojengwa na binadamu; kama nabii asemavyo:
49Y langet tronujo, ya y tano fañajangan y papa adengjo; jafa na guma injatsayeyo? ilegña y Señot; pat jafa na sagayan nae jusaga?
49Bwana asema: Mbingu ni kiti changu cha enzi na dunia ni kiti changu cha kuwekea miguu.
50Ada ti y canaejo fumatinas todo este sija na güinaja?
50Ni nyumba ya namna gani basi mnayoweza kunijengea, na ni mahali gani nitakapopumzika? Vitu hivi vyote ni mimi nimevifanya, au sivyo?
51Jamyo ni y gaetongjo tiso, yan ti manmasirconsida y corason yan y talanga, sa siempre incontra y Espiritu Santo; taegüije y checho y mañaenanmiyo inchechegüe.
51"Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa. Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
52Jaye gui profeta ti japetsigue y mañaenanmiyo? ya japuno ayo sija y manmañangangane antes ni y mamamaela Uno na Tunas; ya jamyo pago inentrega, yan inpino;
52Je, yuko nabii yeyote ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua hao Mungu aliowatuma watangaze kuja kwake yule Mwenye Haki. Na sasa, ninyi mmemsaliti, mkamuua.
53Ni y inresibe y tinago pot y inareglan y angjet, ya ti inadaje.
53Ninyi mliipokea ile Sheria iliyoletwa kwenu na Malaika, lakini hamkuitii."
54¶ Ya anae jajungog estesija, manchinachat asta y corasonñija, ya janafañegcheg y nifenñija guiya güiya.
54Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.
55Lao güiya, bula ni y Espiritu Santo, ya jaatan meton y langet, ya jalie y minalag Yuus, yan si Jesus na tumotojgue gui agapa na canae Yuus.
55Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
56Ya ilegña, Estagüe na julie y langet na mababa, ya y Lajin taotao tumotojgue gui agapa na canae Yuus.
56Akasema, "Tazameni! Ninaona mbingu zimefunuliwa na Mwana wa Mtu amesimama upande wa kulia wa Mungu."
57Ayonae sija managang ni y dangculo na inagangñija, yan jatampe y talanganñija, ya manmalago guato guiya güiya;
57Hapo, watu wote katika kile kikao cha Baraza, wakapiga kelele na kuziba masikio yao kwa mikono yao. Kisha wakamrukia wote kwa pamoja,
58Ya mayute juyong gui siuda, ya mafagas ni y acho: ya y testigo sija, japolo papa y magagoñija gui adeng un patgon na taotao na y naanña si Saulo.
58wakamtoa nje ya mji, wakampiga mawe. Wale mashahidi wakayaweka makoti yao chini ya ulinzi wa kijana mmoja jina lake Saulo.
59Ya mafagas ni y acho si Esteban, ya jaaagang ni Yuus, ilegña: Señot, Jesus, resibe y Espiritujo.
59Waliendelea kumpiga mawe Stefano, huku akiwa anasali: "Bwana Yesu, ipokee roho yangu!"
60Ya dumimo papa, ya umagang ni y dangculo na inagangña, ilegña: Señot, chamo pumopolo este na isao gui cuentanñija; ya anae munjayan jasangan este, maego.
60Akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa: "Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii." Baada ya kusema hivyo, akafa.