1YA ayo sija na jaane anae lumamegae y disipulo sija, mangogonggong y Helenitas sija contra y Hebreo sija, sa y manbiuda guiya sija, ti manmaatiende gui sinetbeñija cada jaane.
1Baadaye, idadi ya wanafunzi ilipokuwa inazidi kuongezeka, kulitokea manung'uniko kati ya wanafunzi waliosema Kigiriki na wale waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigiriki walinung'unika kwamba wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika ugawaji wa mahitaji ya kila siku.
2Ayonae y dose, jaagang y manadan disipulo guato guiya sija, ya ilegñija: Ti tunas na tapolo y sinangan Yuus, ya tasetbe y lamasa sija.
2Kwa hiyo, mitume kumi na wawili waliita jumuiya yote ya wanafunzi, wakasema, "Si vizuri sisi tuache kulihubiri neno la Mungu ili tushughulikie ugawaji wa mahitaji.
3Enaomina mañelo, aligao entre jamyo siete na taotao ni y manmauleg, ni y manbula Espiritu, yan minejnalom, ya tapolo para este na chocho.
3Hivyo, ndugu zetu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema, waliojawa na Roho na wenye hekima; nasi tutawakabidhi jukumu hilo.
4Lao jita, tasigueja fitme y manmanaetae, yan y sinetbe y sinangan.
4Sisi, lakini, tutashughulika na sala na kazi ya kuhubiri neno la Mungu."
5Ya ayo na sinangan, ninafanmagof y manada todo; ya maayeg si Esteban, un taotao na bula jinenggue yan Espiritu Santo, yan si Felipe, yan si Prócoro, yan si Nicanor, yan si Timón, yan si Parmenas, yan si Nicolás proseliton Antioquia.
5Jambo hilo likaipendeza jumuiya yote ya waumini. Wakawachagua Stefano, mtu mwenye imani kubwa na mwenye kujawa na Roho Mtakatifu, Filipo, Prokoro, Nikanora, Timona, Parmena na Nikolao wa Antiokia ambaye hapo awali alikuwa ameongokea dini ya Kiyahudi.
6Ya manmaplanta gui menan y apostoles: ya anae munjayan manmanaetae, japolo y canaeñija gui jiloñija.
6Wakawaweka mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono.
7Ya y sinangan Yuus lumalamegae; ya y disipulo megae manmaumentaña guiya Jerusalem; ya dangculon manadan mamale locue, manmanosgue ni y jinenggue.
7Neno la Mungu likazidi kuenea na idadi ya waumini huko Yerusalemu ikaongezeka zaidi, na kundi kubwa la makuhani wakaipokea imani.
8¶ Ya si Esteban, bula y grasia yan ninasifia, jafatinas namanman na milagro yan señat gui entalo y taotao sija.
8Mungu alimjalia Stefano neema tele, akampa nguvu nyingi hata akawa anatenda miujiza na maajabu kati ya watu.
9Lao guaja mangajulo güije gui sinagoga ni y manmafanaan sinagogan Libertinos, yan Sireneo sija, yan Alejandrino sija, yan ayo sija iya Silisia, yan Asia, managuaguat yan si Esteban.
9Lakini watu fulani wakatokea ili wabishane na Stefano. Baadhi ya watu hao walikuwa wa sunagogi moja lililoitwa "Sunagogi la Watu Huru", nao walitoka Kurene na Aleksandria; wengine walitoka Kilikia na Asia.
10Lao tisiña macontra y tiningo, yan y Espiritu ni y jasangan.
10Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyeongoza maneno yake.
11Ya manmasusuug y taotao sija na ujaalog: Injingogja güe na jasangan y chinatfino contra si Moises, yan contra si Yuus.
11Kwa hiyo waliwahonga watu kadhaa waseme: "Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kumkashifu Mose na kumkashifu Mungu."
12Ya manafangalamten y taotao sija, yan y manamco, yan y escribasija; ya manmato guiya güiya, ya macone güe guato gui sinedrio,
12Kwa namna hiyo, waliwachochea watu, wazee na walimu wa Sheria. Basi, wakamjia Stefano, wakamkamata na kumleta mbele ya Baraza kuu.
13Ya manmamalo testigo na ti magajet, ni ilegñija: Este na taotao ti malago bumasta cumuentos chinatfino contra este y santos na lugat, yan contra y tinago:
13Walileta Barazani mashahidi wa uongo ambao walisema, "Mtu huyu haachi kamwe kusema maneno ya kupakashifu mahali hapa patakatifu na Sheria ya Mose.
14Sa injingogja gue ilegña, na este y as Jesus taotao Nasaret uyulang este na lugat, yan utulaeca, y costumbre ni y jaentregajit si Moises.
14Kwa maana tulikwisha msikia akisema eti huyo Yesu wa Nazareti atapaharibu kabisa mahali hapa na kufutilia mbali desturi zile tulizopokea kutoka kwa Mose."
15Ya todo ayo sija y manmatatachong gui sinedrio, maaatan güe, ya malie y mataña na calang matan angjet.
15Wote waliokuwa katika kile kikao cha Baraza walimkodolea macho Stefano, wakauona uso wake umekuwa kama wa malaika.