1YA ilegña ni y disipuluña sija: Ti siña ti ufato y escandalo; lao ay, ay ayo y munafato!
1Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.
2Maulegña na umagode gui agagaña un alutong, ya umayute gui tase, antes qui uninaquepodong uno güine gui mandiquique sija.
2Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.
3Adaje jamyo: Yanguin umisao y chelumo contra jago, reprende: y yanguin mañotsot, asie.
3Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, mwonye; akitubu, msamehe.
4Yanguin siete biaje gui un jaane umisao contra jago, ya siete biaje mafato guiya jago, ya ilelegña: Mañotsotyo, un asie.
4Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema Nimetubu, lazima umsamehe."
5¶ Ya y apostoles, ilegñija nu y Señot: Aumenta, y jinengguenmame.
5Mitume wakamwambia Bwana, "Utuongezee imani."
6Ya y Señot ilegña: Yanguin mangaejinenggue jamyo taegüije y granon mostasa, ya mojon ilegmiyo nu este na sicómoro trongcon jayo: Chapag jao güenao, ya unplanta jao gui tase; ya mojon infaninesgueja.
6Naye Bwana akajibu, "Kama imani yenu ingekuwa ndogo hata kama chembe ndogo ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu: Ng'oka ukajipandikize baharini, nao ungewatii.
7Lao jaye guiya jamyo y guaja tentagoña, na manalalado, pat mamamasto quinilo, y yanguin mato guinin y fangualuan, ualog nu güiya; maela enseguidas y fatachong, ya unchocho?
7"Tuseme mmoja wenu ana mtumishi ambaye analima shambani au anachunga kondoo. Je, anaporudi kutoka shambani, atamwambia: Haraka, njoo ule chakula?
8Ya ti ualog nu güiya finena: Nalisto y senajo para juchocho, ya undudog jao, ya unsetbeyo asta qui munjayanyo chumocho, yan gumimen: ya despues nae unchocho, ya unguimen?
8La! Atamwambia: Nitayarishie chakula, ujifunge tayari kunitumikia mpaka nitakapomaliza kula na kunywa, ndipo nawe ule na unywe.
9Numae grasias ayo na tentago, sa jafatinas y matagoña? Jinasoco na aje.
9Je utamshukuru huyo mtumishi kwa sababu ametimiza aliyoamriwa?
10Taegüineja locue jamyo, yanguin esta inchegüe todo ayo sija y jutago jamyo, ualog: Maninutil jam na tentago; sa ayoja y para y chechomame inchegüe.
10Hali kadhalika na ninyi mkisha fanya yote mliyoamriwa, semeni: Sisi ni watumishi tusio na faida, tumetimiza tu yale tuliyotakiwa kufanya."
11¶ Ya susede anae jumanao para Jerusalem, ya malofan gui inanaco Samaria, yan Galilea.
11Yesu akiwa safarini kwenda Yerusalemu alipitia mipakani mwa Samaria na Galilaya.
12Ya anae jumalom gui un songsong, manasoda güije yan dies na taotao na manategtog; ya manojgue desde y chago.
12Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.
13Ya jajatsa y inagangñija, ya ilegñija: Jesus, Maestro, gaease nu jame.
13Wakapaza sauti wakisema, "Yesu Mwalimu, tuonee huruma!"
14Ya anae jalie, ilegña nu sija: Janao ya infanue y mamale nu jamyo. Ya susede anae manjajanao, manjuyong mangasgas.
14Alipowaona akawaambia, "Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani." Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.
15Ya y uno guiya sija, anae jalie na jomlo güe, jabira güe tate, ya janaagagang mannae si Yuus minalag.
15Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.
16Ya jatomba güe papa gui fion adeng si Jesus, ya janae grasias: este na taotao, Samaritano.
16Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.
17Ya manope si Jesus, ilegña: Ada ti dies y mangasgas? ya manmangue y nuebe?
17Hapo Yesu akasema, "Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?
18Taya masoda tumalo mague para unae si Yuus grasias, na esteja y taotao juyong.
18Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?"
19Ya ilegña bu güiya: Cajulo ya unjanao; y jinengguemo munajomlo jao.
19Halafu akamwambia huyo mtu, "Simama, uende zako; imani yako imekuponya."
20¶ Ya anae mafaesen ni y Fariseo sija, ngaean nae ufato y raenon Yuus, jaope ilegña: Y raenon Yuus, ti matungo finatoña.
20Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, "Ufalme wa Mungu utakuja lini?" Naye akawajibu, "Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.
21Ni ujaalog: Estagüe! pat ayogüe! sa y raenon Yuus, gaegueja gui sumanjalommiyo.
21Wala hakuna atakayeweza kusema, Uko hapa, au Uko pale. Kwa kweli Ufalme wa Mungu uko kati yenu."
22¶ Ya ilegña ni y disipuluña sija: Ufato y jaane sija, na infanmalago na inlie uno gui jaanin y Lajin taotao, ya ti inlie.
22Halafu akawaambia wanafunzi wake, "Siku zinakuja ambapo mtatamani kuona mojawapo ya siku za Mwana wa Mtu, lakini hamtaiona.
23Ya ujaalog nu jamyo: Estagüe, pat ayogüe; chamiyo tumatitiye, ni indalalaque sija.
23Na watu watawaambieni: Tazameni yuko hapa; ninyi msitoke wala msiwafuate.
24Sa taegüijeja y lamlam, yan mañila gui un lugat gui papa y langet, ya inina y otro banda gui papa y langet; taegüineja locue y Lajin taotao, gui jaaniña.
24Kwa maana kama vile umeme unavyotokea ghafla na kuangaza anga upande mmoja hadi mwingine, ndivyo Mwana wa Mtu atakavyokuwa siku yake.
25Lao nesesita na ufamadese finena megae, ya umarechasa ni este na generasion.
25Lakini kabla ya hayo, itambidi ateseke sana na kukataliwa na kizazi hiki.
26Sa jaftaemanoja y jaanin Noe, taegüijeja locue y jaanin y Lajin taotao.
26Kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Mtu.
27Mañocho, yan manguimen, yan manasagua, yan manafanasagua, asta ayo na jaane anae jumalom si Noe gui atca, ya mato y dilubio ya manyinilang sija todo.
27Watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka wakati ule Noa alipoingia katika safina. Gharika ikatokea na kuwaangamiza wote.
28Taegüineja locue jasusede gui jaanin Lot: mañocho, manguimen, manmamajan, manmanbende, manmananom, yan manmanjatsa guma;
28Itakuwa kama ilivyotokea wakati wa Loti. Watu waliendelea kula na kunywa, kununua na kuuza, kupanda mbegu na kujenga.
29Lao ayoja na jaane anae jumanao si Lot guiya Sodoma, janauchan guafe, yan asufre guinin y langet, ya manyinilang todo sija.
29Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikanyesha kama mvua kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.
30Taegüijeja uguaja güije na jaane yanguin ufamanue y Lajin taotao.
30Ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mtu atakapofunuliwa.
31Ayo na jaane, ayo y gaegue gui jilo guma ya y güinajaña gaegue gui jalom guma, chaña tumutunog ya uchule; parejoja locue yan y gaegue gui fangualuan, chaña tumatalo tate.
31"Siku hiyo, yeyote atakayekuwa juu ya paa asishuke nyumbani kuchukua mali yake. Kadhalika, naye atakayekuwa shambani asirudi nyuma.
32Jaso y asaguan Lot.
32Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti.
33Masquesea jaye y umaliligao na usatba y linâlâña, ufinalingaeguan; ya masquesea jaye y finalingaeguan y liânâlña umasatba.
33Yeyote anayetaka kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na yeyote anayeipoteza, ataiokoa.
34Jusangane jamyo, na ayo na puenge uguaja dos na taotao gui un catre; y uno umacone ya y otro umapolo.
34Nawaambieni, siku ile usiku watu wawili watakuwa wanalala pamoja, mmoja atachukuliwa na yule mwingine ataachwa.
35Dos na palaoan dumadaña manguleg; y uno umacone, ya y otro umapolo.
35Wanawake wawili watakuwa wakisaga nafaka pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa."
36Dos na taotao ugaegue gui fangualuan; y uno umacone, ya y otro umapolo.
36Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
37Ya manmanope ilegñija nu güiya: Manggue Señot? Ya jaope ilegña: Manoja nae gaegue y tataotao, ayoja nae mandaña y pojaro aguila sija.
37Hapo wakamwuliza, "Ni wapi Bwana?" Naye akawaambia, "Ulipo mzoga, ndipo tai watakapokusanyikia."