1YA susede uno gui güije sija na jaane, anae jafananagüe y taotao sija gui templo, ya japredidica y ibangelio; manmato guiya güiya y magas mamale, yan y escriba, yan y manamco sija;
1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2Ya macuentuse, ilegñija nu güiya: Sangane jam, jafa na ninasiña na unfatitinas este sija na güinaja? Pat jaye numae jao ni este na ninasiña?
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
3Ya manope si Jesus, ilegña nu sija: Jufaesen locue jamyo un finaesen, ya sanganeyo;
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
4Y tagpangen Juan, guinin y langet, pat guinin y taotao sija?
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
5Ya sija, jajaso gui sumanjalomñija, ilegñija: Yanguin ilegmame: Guinin y langet; ualog, jafa nae na ti injenggue güe?
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6Lao yanguin ilegmame: Guinin y taotao sija; infanmamagas nu y acho ni y taotao, sa pineloñija na profeta si Juan.
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
7Ya manmanope na ti jatungo guine mano.
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
8Ayonae ilegña si Jesus nu sija: Ni guajo locue ti jusangane jamyo, jafa na ninasiña na jufatitinas este sija na güinaja.
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
9¶ Ya jatutujon sumangane sija ni este na acomparasion; Un taotao, manplanta un fangualuan ubas, ya japoluye ni manfáfachocho, ya jumanao para y chago na tano, apmam na tiempo.
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10Ya y tiempon mangoco, jatago un tentago para y manmachóchocho, para umanae ni y tinegcha y gualo; lao masaulag ni y manmachóchocho, ya manajanao taesinajguan.
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11Ya jatago talo y otro tentago: ya masaulag locue talo, ya manamamajlao, ya manajanao taesinajguan.
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12Ya jatalo tumago y mina tres na tentago: ya manaerida, ya mayute juyong.
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13Ayonae ilegña y señot y fangualuan: Jafa jufatinas? Bae jutago y guefyajo na lajijo, sa buente ufangaerespeto nu güiya.
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14Lao anae malie ni y manmachóchocho, manasangane ilegñija: Estagüe y heredero; nije tapuno, ya usaga y inereda guiya jita.
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15Ya mayute juyong gui jiyong y fangualuan, ya mapuno. Jafa pago ufatinas y señot y fangualuan nu sija?
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16Ufato, ya uyulang este sija y manmachóchocho, ya ufannae otro ni y fangualuan. Ya anae majungog ayo, ilegñija: Munga este.
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
17Lao jaatan sija ya ilegña: Jafa nae este y esta matugue: Y acho ni y jarechasa y manmamatitinas y guima, esteja mapolo cuentan ulo gui esquina?
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18Jayeja y pedong gui jilo ayo na acho, umayamag pedasitos; lao jayeja y jinegse, ufinapetbos.
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
19¶ Ya y magas mamale, yan y escriba sija, maaliligao para umaqueguot güije na ora; lao manmaañao nu y taotao sija, sa matungoja na jasangan este na acomparasion, contra sija.
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20Ya mapupulanja yan manmanago na umaespipia, para ujafaquemanunas sija na taotao, ya uquefanmañule ni y sinanganña, ya umaqueentrega güe gui inaregla yan ninasiñan y gobietno.
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21Ya mafaesen güe, ilegñija: Maestro, intingo na unsasangan yan mamananagüe jao tunas, ya ti numanasajnge jao taotao, lao mamananagüe jao ni y magajet na chalan Yuus.
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22Tunas na infanmanaejam si Sesat tributo, pat aje?
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
23Lao jatungoja y mañañija, ya ilegña nu sija:
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24Fanueyo nu y salape. Jaye gaeimagen este yan este na tinigue? Ya manmanope ilegñija: Iyon Sesat.
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
25Ya ilegña nu sija: Nae si Sesat ni y iyon Sesat, ya innae si Yuus nu y iyon Yuus.
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
26Ya ti siña maguot pot y sinanganña gui menan y taotao sija; ya ninafanmanman ni y inepeña ya manmamatquilo.
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27¶ Ya manmato guiya güiya Saduseo sija, ni y sumangan na taya quinajulon manmatae; ya mafaesen güe,
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28Ylegñija: Maestro, si Moises jatuguiejam, na yanguin dos chumelo na laje, ya y uno guaja asaguaña, ya matae taya patgonña; ayo y cheluña uniasagua y palaoan, ya unacajulo semiya gui cheluña.
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29Ya guaja siete na lalaje na mañelu: ya y finenana umasagua, ya matae taya patgonña.
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30Ya inasagua y palaoan ni y miná dos;
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31Ya inasagua talo ni y miná tres; yan taegüenaoja locue todo y siete manmatae ya taya famaguonñija.
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
32Ya y palaoan uttimo matae locue.
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33Ya y quinajulon manmatae, jaye gaeasagua y palaoan? sa inasagua todo ni y siete.
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
34Ya si Jesus ilegña nu sija: Y famaguon este na tiempo manásagua yan manafanásagua:
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
35Lao ayo sija y ufanmanmerese güije na tiempo, yan y quinajulon manmatae, ni ufanasagua, ni umanafanasagua:
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
36Ni ti siña manmatae talo: sa manparejoja yan y angjet sija; yan manfamaguon Yuus, sa manfamaguon y quinajulon. manmatae.
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37Ya pot y manmatae ni umanafangajulo, asta si Moises mamanue gui finajalomtano, anae jafanaan y Señot, Yuus Abraham yan Yuus Ysaac yan Yuus Jacob.
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38Sa ti güiya Yuus manmatae, na manlâlâ: sa todosija manlala guiya güiya.
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
39Ya manmanope palo gui escriba sija ilegñija: Maestro, mauleg sinanganmo.
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
40Ya desde ayo, ti matatnga mafaesen güe talo jafa.
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41¶ Ya ilegña nu sija: Jafa na ilegñija na si Cristo lajin David?
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42Ya güiyaja si David umalog gui leblon y Salmos: Y Señot ilegña ni y Señotjo, Fatáchong gui agapa na canaejo,
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43Asta qui jupolo y enemigumo sija para fañajangan y adengmo.
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44Enao muna si David finanaan güe Señot, ya jaftaemano mina ulajiña?
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
45¶ Ya majujungogja ni y taotao sija, anae ilegña ni y disipuluña:
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46Adaje jamyo ni y escriba sija, sa yanñija manmamocat yan y anaco na magago, yan yanñija manmasaluda gui plasa, yan y finénana na tachong gui sinagoga sija; yan y finénana na saga gui guipot;
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47Yan jalachae y guima y biuda sija, yan manmamanunue ni y anaco tinaetaeñija pot taya; estesija ujaresibe mandangculo na sinentensia.
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"