Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Luke

4

1YA si Jesus, bula Espirita Santo, tumato guato gui Jordan, ya quinene ni Espiritu asta y desierto.
1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2Ya sumaga güije cuarenta na jaane ya tinienta nu y anite. Ya ti chumocho ni jafa, güije sija na jaane; ya anae esta macumple, ñalang güe.
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3Ya ilegña nu güiya y anite: Yaguin jago Lajin Yuus, tago este y acho ya ufamapan.
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4Ya si Jesus manope qüe: Esta mamatugue, na ti y panja munalâlâ y taotao.
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
5Ya jacone güe quinene julo, ya finanue güe todo y raeno gui jilo y tano gui un momento y tiempo,
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6Ya y anite ilegña nu güiya: Bae junae jao ni este na ninasiña todo, yan y minalagñija; sa guajo maentrega, ya jaye y malagojo, junae.
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7Enaomina jago, yaguin unadora gui menajo, todosija iyomo.
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
8Ya manope si Jesus, ya ilegña: Esta matugue na y Señot Yuusmo unadora, ya güiyaja unsetbe.
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
9Ya quinene talo guiya Jerusalem ya pinelo gui sumanjilo y templo, ya ilegña nu güiya: Yaguin jago Lajin Yuus, yutejao güine papa:
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10Sa esta matugue, na y angjetña sija jaencatga nu jago para unmaadaje,
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11Ya y canaeñija unquilile sa chamo matompo y adengmo gui acho.
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
12Manope si Jesus ya ilegña: Esta masangan: Chamo tietienta y Señot Yuusmo.
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
13Anae esta munjayan todo y tentasionña y anite mapos guiya güiya un rato.
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14¶ Si Jesus tumato gui ninasiñan y Espiritu asta Galilea: ya jumanao y famaña guiya todo y tano gui oriyaña.
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15Ya güiya mamananagüe gui guimayuusñija, ya ninafanonra nu y todo.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16¶ Ya mato guiya Nasaret anae jagas mapogsae: ya jumalom taemanoja y costumbreña gui jaanin sabado, gui guimayuus ya cajulo para utaetae.
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17Ya manaegüe y leblon y profeta Isaias. Ya anae jababa y leblo, jasoda anae esta matugue:
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18Y Espiritun y Señot gaegue gui jilojo, sa japalae yo para jupredica y mauleg na sinangan gui mamobble: ya matago yo para jusangane mancautibo, linibre, ya para y manbachet ufanmanlie, ya para junafanlibre y manchiguit,
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19Para jusaganñaejon y guaeyayon na año y Señot.
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
20¶ Ya jajuchom y leblo ya anae janatalo y ministro, matachong; ya todo y mangaegue gui guimayuus, güiyaja manatan.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21Ya jatutujon sumangane sija: Pago esta macumple este na tinigue gui talanganmiyo.
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
22Ya todoja manmannae testimonio ya esta ninafanmanman nu minauleg sinangan ni manjujuyong, gui pachotña; ya ilegñija: Ti güiya ini y lajin José.
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
23Ya ilegña nu sija: Magajet insanganeyo nu este na sinangan: Medico, amte namaesajaoja: todo sija injingog na unfatinas guiya Capernaum, fatinas locue güine gui tanomo.
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
24Ya ilegña: Magajet na jusangane jamyo, na ni un profeta guaegayon gui tanoña.
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25Lao magajet jusangane jamyo: Megae na biuda sija guaja gui Israel gui jaanin Elias, anae y langet majuchom tres años yan saes mesas, anae guaja dangculo na ñinalang gui todo y tano;
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26Lao ni uno guiya sija nae, esta matago si Elias, na as Sarepta, guiya tanon Sidon, guiya un palaoan biuda.
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27Ya megae na ategtog locue guaja guiya Israel gui tiempon y profeta Eliseo; lao taya guiya sija esta magasgas, na si Naaman taotao Siro.
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
28Ayo nae todo y taotao gui guimayuus manbula y linalalo, anae jajungog estesija;
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29Ya mangajulo, ya chumulegüe gui sanjiyong y siuda, ya macone asta gui sanjilo y egso, anae esta maplanta y siudañija, para ufanyute gui papa.
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30Lao güiya, malofan gui entaloñija, ya mapos.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31¶ Ya mato papa guiya Capernaum, siudan Galilea, ya ayo nae mamananagüe gui sabado na jaane:
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32Ya sija ninafanmanman nu y finanagüeña; sa y sinanganña gaeninasiña.
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33Ya gaegue gui guimayuus un taotao na guaja anite ináplacha; ya umagang dangculo na inagang.
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34Jei! pelojam! para jafajam nu jago, Jesus Nasareno? Matojao para unyulangjam? jutungojao jayejao; jago ayo na Santos gui as Yuus!
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
35Ya si Jesus jalalatde ya ilegña: Pacaca ya maela juyong guiya güiya. Ya anae y anite mayute güe gui entaloñija, jumuyong guiya güiya; ya taya ninalamen.
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36Ya minamanman mato gui jilo todo sija, ya manadingan uno yan otro, ilegñija: Jafa na cuentos este? Sa nu y gobietnaña yan y ninasiñaña jatago y áplacha na anite sija ya unfanjuyong?
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
37Ya y famaña masanganñaejon todo y lugat sija gui oriyaña ayona.
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38¶ Ya jacajulo jumanao juyong gui guimayuus ya jumalom gui guiman Simon; ya y suegran Simon esta umaason, malingo nu y dangculo na calenturaña; ya matayuyutgüe pot güiya.
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39Ya jatojgue gui jijutña, ya jalalatde y calentura ya y calentura pinelo; ya güiya cajulo ensiguidas ya jasetbe.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40¶ Ya y tiempo y minachom y atdao nae, todo y mangaemalango ni y megae na chetnot, manmaconie guiya güiya; ya japolo y canaeña gui jilo cada uno guiya sija, ya janafanjomlo sija.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41Ya anite sija manjuyong locue guiya megae, na manaagang ya ilegñija: Jago, y Lajin Yuus! Lao güiya jalalatde ya ti japolo ya ufanguentos, sa matungo güe na güiya si Cristo.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42¶ Ya anae esta taftaf y jaane, jumanao para un jalomtano: ya y linajyan taotao sija maaliligao güe ya manmafato guiya güiya ya manmalago sija ufanmantiene güe para munga mapos guiya sija.
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43Ya güiya ilegña nu sija: Nesesitayo locue gui palo siuda umapredica y raenon Yuus: sa para este na matagoyo.
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
44Ya japredidica gui guimayuus sija guiya Galilea.
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.