1YA susede anae y linajyan taotao manoriya yan machichiguet güe ya jaecungog y sinangan Yuus, na güiya gaegue tumotojgue gui oriyan jagoe Genesaret.
1Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
2Ya jalie dos batco na estaba jijot gui oriyan y jagoe; ya y manpescadot manunog güije, ya jafagase y laguañija.
2Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
3Ya jumalom güine gui un batco ya y iyon Simon; ya jagagao na unafalag y tano didide. Ya matachong ya mamanagüe desde y batco ni linajyan taotao.
3Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
4Ya anae munjayan cumuentos, ilegña as Simon: Juyong gui tadong na tase ya innatunog y laguanmiyo para un quinene.
4Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, "Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki."
5Ya manope si Simon ya ilegña: Maestro estajam manmachocho todo puenge ya taya quinenemame; lao pot y sinanganmo bae innatunog y lagua.
5Simoni akamjibu, "Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu."
6Ya anae manmatinas este, japongle un dangculo na quinenen güijan; ya esta tiniteg y laguanñija.
6Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7Ayo nae jaseñat y mangachongñija ni mangaegue gui otro batco, para ufanmato ya ufaninayuda. Ya manmato, ya janabulaja y dos batco, ya jatutujon manmañoñogñog.
7Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
8Ya anae jalie este si Simon Pedro, dumimo papa gui as Jesus ya ilegña: Suja guiya guajo, Señot; sa taotao isaoyo.
8Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, "Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!"
9Sa ninamaañao yan todos y mangaegue guiya güiya, pot causa de y quinenen güijan ni y inquene;
9Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
10Ya taegüije ja locue as Santiago yan si Juan, famaguon Sebedeo, ya sija mangachong Simon. Ya ilegña si Jesus as Simon: Chamo maaaño: sa desde pago ufangone jao y taotao.
10Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, "Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu."
11Ya anae esta mañule gui tano y batcoñija; todo jayute ya madalaggüe.
11Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
12¶ Ya susede anae gaegue güe gui uno gui siuda sija, estagüe un taotao na bula ategtog: güiya anae jalie si Jesus, podong gui mataña gui menaña ya jagagao, ilegña: Señot, yaguin malagojao, siñajao unnagasgasyo?
12Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: "Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa."
13Ya jaestira y canaeña ya japacha, ilegña: Malagoyo, gasgasjao; ya enseguidas y ategtog jumanao guiya güiya.
13Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka, takasika!" Mara ule ukoma ukamwacha.
14Ya tinago güe, na chaña sangangane ni jaye: lao janao, unfanue y pale nu jago ya unofrese ni y guinasgasmo, taemanoja y tinagon Moises para testimonio nu sija.
14Yesu akamwamuru: "Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
15Lao y masanganña jumanao megae; ya mandaña y dangculon linajyan taotao para umajungog yan para ufanmagong y chetnotñija.
15Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16Lao güiya jaapatta güe asta y jalomtano ya manaetae.
16Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
17¶ Ya susede gui un jaane na estabagüe mamanagüe; ya mangaegue y Fariseo sija yan y magas y lay, manmatatachong, sa sija manmato guinen y sengsong Galilea, yan Judea, yan y ya Jerusalem; ya y ninasiñan y Señot gaegue güije para unamagong.
17Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
18Ya estagüe sija taotao na macocone un taotao gui jilo un cama na paralitico; ya maaliligao mano nae mañule jalom para umapolo gui menaña.
18Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
19Ya anae ti masoda mano nae umapolo pot causa y linajyan taotao, mangajulo gui jilo guma ya guinin y atof nae manatunog yan camaña gui entalo, asta y gui menan Jesus.
19Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
20Ya anae jalie y jinengguenñija yuje sija, ilegña: Taotao, y isaomo umaasie.
20Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, "Rafiki, umesamehewa dhambi zako."
21Ya y escriba yan y Fariseo sija jatutujon manmanjaso, ya ilegñija: Jaye güe este na usangan chatfino contra si Yuus? Jaye siña manasie isao, na si Yuusja?
21Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: "Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!"
22Lao si Jesus jatungo y jinasonñija; manope ya ilegña nu sija: Jafa injajaso gui corasonmiyo?
22Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, "Mnawaza nini mioyoni mwenu?
23Jafa sen taeminapot masangan: Y isaomo unmaasie; pat masangan: Cajulo ya unfanmocat?
23Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
24Lao para intingoja na y Lajin taotao guaja ninasiñaña gui tano para umasie isao (ilegña nu y paralitico), jusanganejao: Cajulo, chule y camamo ya unjanao para iyajamyo.
24Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani."
25Ya enseguidas güiya cajulo gui menanñija, ya jachule ayo anae umaasongüe ya jumanao para y guimaña, ya jatuna si Yuus,
25Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
26Ya ninafanmanman todosija, ya matuna si Yuus; ya manbula y minaañao, ilegñija: Inlie námanman sija pago.
26Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: "Tumeona maajabu leo."
27¶ Ya despues di estesija, jumanao, ya jalie un publicano na y naanña si Levi, matatachong gui bancon y tributo ya ilegña: Dalalagyo.
27Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, "Nifuate!"
28Ya japolo todo y güinajaña ya cajulo ya jadalalaggüe.
28Lawi akaacha yote, akamfuata.
29Ya jafatinas si Levi un dangculon gupot gui guimaña: ya guaja un dangculon linajyan publicano sija, yan otro sija manmatachong gui lamasa yan sija.
29Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
30Ya y Fariseo sija yan y escribañija, mangogonggong contra y disipuluña sija, ilegñija: Sajafa na manjajamyo mañocho yan manguimen yan y publicanosija yan y manisao?
30Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: "Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
31Ya manope si Jesus ya ilegña nu sija: Y manaechetnot ti janesesita medico; lao y manmalango.
31Yesu akawajibu, "Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
32Ti matoyo para juagang y manunas, lao y manisao para ufanmañotsot.
32Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu."
33¶ Ya ilegñija nu güiya: Y disipulon Juan manayuyunat megae na biaje, ya jafatitinas tinayuyut; parejoja yan y disipulon Fariseo sija; ya iyoco mañochocho yan manguiguimen?
33Watu wengine wakamwambia Yesu, "Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa."
34Ya si Jesus ilegña nu sija: Siña innaayunat y mangaegue gui guipot uma sagua anae mañisijaja yan y nobio?
34Yesu akawajibu, "Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
35Lao ufato jaane na y nobio umana suja; ayo nae ufanayunat güije na jaane sija.
35Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga."
36Ya mansinangane sija locue un acomparasion: Taya taotao janajanao pidason magago gui nuebo na bestido ya japolo gui bijo na bestido; no sea ujatiteg y nuebo ya locue y magago guinin nuebo ti parejo yan y bijo.
36Yesu akawaambia mfano huu: "Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
37Ya taya mananaye nuebo na bino gui bijo na boteyan cuero: ya no sea, y bino ni nuebo uyinamag y boteyan cuero, ya y bino umachuda, ya y boteyan cuero ufalingo.
37Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
38Lao y nuebo bino na nasesita y nuebo na boteyan cuero nae umapolo.
38Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
39Ya ni un taotao ni gumimen y bijo na bino umalago ni nuebo; sa ualog: Y bijo maulegña.
39Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi."