Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Luke

6

1YA susede y un sabado, jumajanao si Jesus gui fangualuan maies; ya y disipuluña sija, manmanjajala ni y masotcan maies, ya jacano, jagugugan ni y canaeñija.
1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2Ya y Fariseo sija ilegñija: Jafa na infatitinas y ti tunas na umafatinas gui sabado na jaane:
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
3Ya maninepe as Jesus iligña: Taya nae intaetae este y finatinas David anae ñalang yan y mangachongña?
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4Anae jumalom gui guimayuus, ya jachule ya jacano y pan ni y mafamamauleg, yan janae locue y mangachongña: ni y ti tunas na ucano na para y mamaleja?
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
5Ya ilegña nu sija: Y Lajin Taotao locue Señot y sabado.
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
6¶ Ya susede y otro sabado, na jumalom gui guimayuus ya mamanagüe: ya estaba güije un taotao na anglo y agapa na canaeña.
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7Ya y escriba yan y Fariseo sija maaatan güe, cao unajomlo gui sabado na jaane; para uquefanmañoda jafa ya umafaaela.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8Lao jatungoja y jinasonñija; ya ilegña ni ayo na taotao y anglo canaeña: Cajulo ya untojgue gui tálolo! ya tumojgue julo.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9Ya ilegña si Jesus nu sija: Jufafaesen jamyo uno. Tunas gui sabado na umafatinas y mauleg pat y taelaye? numalibre linâlâ pat mamuno?
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
10Ya jaatan todos y oriyañija ya ilegña nu güiya: Estira mona y canaemo. Ya guiya jafatinas taegüije, ya y canaeña numalo ya magong taegüije y otro.
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11Ya sija mansénbubo, ya manguecuentos uno yan otro, jafa mojon ujafatinas gui as Jesus.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12¶ Ya susede gui ayo sija na jaane, jumanao para ufanaetae gui un ogso ya todo y puenge jasigue di manaetaeja para as Yuus.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13Ya anae manana, jaagang y disipuluña sija; ya jaayig dose guiya sija, ni manmafanaan locue apostoles.
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14Si Simon ni jafanaan locue Pedro, yan si Andres cheluña, yan si Santiago, yan si Juan, si Felipe, yan si Bartolome,
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15Yan si Mateo, yan si Tomas, yan si Santiago, lajin Alfeo, yan si Simon ni mafanaan Selote,
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16Yan si Judas chelun Santiago, yan si Judas Iscariote ni y traidot;
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17Ya manunog yan sija ya tumojgue gui un lugat ni yano; yan y dangculon linajyan disipuluña sija, yan y dangculon linajyan taotao, guinin todo yya Judea, yan yya Jerusalem, yan y tano Tiro yan yya Sidon, ni manmato para umaecungog, yan para uninafanmagong y chetnotñija;
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18Yan manafanmagong ayo sija y munafanachatsaga ni y espiritun áplacha.
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19Ya manmalago pumapacha güe y linajyan taotao: sa manjujuyong guiya güiya ninasiña ya janafanmamagong todo sija.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20¶ Ya güiya manatan julo gui disipuluña, ya ilegña: Mandichoso jamyo ni mamobble; sa iyonmiyo y raenon Yuus.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21Mandichoso jamyo ni y manñalang pago: sa ufanjaspog. Mandichoso y manatanges: sa ufañaleg.
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22Mandichoso jamyo yaguin y taotao sija infanchinatlie, yan ujaapatta sija guiya jamyo ya ujalalatde jamyo ya ujayute juyong y naanmiyo pot taelaye pot causa y Lajin taotao.
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23Fansenmagof güije na jaane; yan infanayog ni minagofmiyo: sa, estagüe, y premionmiyo dangculo gui langet; sa taegüenaoja jafatitinas y tatañija ni y profeta sija.
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24Lao ay jamyo ni manrico! sa esta guaja consuelonmiyo.
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Ay jamyo ni esta manjaspog pago! sa infanñalang. Ay jamyo ni mañachaleg pago! sa jamyo infanugong yan infananges.
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26Ay jamyo yaguin todo y taotao sija manguecuentos mauleg nu jamyo! sa taegüenaoja ujafatinas y tatañija ni y manfatso na profeta.
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27¶ Lao jusangangane jamyo ni jumujungog: Güaeya y enemigonmiyo; fatinas mauleg ni y chumatlie jamyo,
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28Bendise y mumatdise jamyo, ya infanmanaetae pot y namamajlao jamyo.
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29Ya pumatmada y un banda fasumo, naeja locue ni y otro, ya y chumule y capamo, chamo chumochoma na uchule y chininamo locue.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30Ya cada uno ni y gumagaojao, nae; ya y chumule y güinajamo, chamo tumalulugua gumagao.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31Ya jafa y malagomiyo ni y taotao jafatinas nu jamyo; taegüijija fatinas locue nu sija:
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32Sa yaguin inguaeya y gumaeya jamyo, jafa na grasia guajanmiyo? sa y manisao locue jaguaeya y gumaeya sija.
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33Yaguin infatinas mauleg ni y fumamamauleg jamyo, jafa na grasia guajanmiyo? sa y manisao locue jafatitinasja taegüenao.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34Yanguin innaayao na ayo sija ni y guaja ninanggamo para infanresibe, jafa na grasia guajanmiyo: sa y manisao janaayao y manisao para ufanmanresibe taegüije talo.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35Lao guaeya jamyo y enimigunmiyo ya infatinas mauleg nu sija: ya innaaayao, ya chamiyo fantataeninangga, ya udangculo y premionmiyo yan infanfamaguon y Gueftaguilo: sa güiya cariñoso nu y ingrato sija, yan y taelaye.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36Jamyo locue fanyóase, taegüije y tatanmiyo ni y gaegue gui langet yóase.
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37Chamiyo jumusga, sa ti infanjinisga: chamiyo sumetetensia, sa ti infansinentensia: nafanlibre, ya y ninafanlibre:
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38Fanmanae, ya infanmanae; mauleg na medida y majoño papa, ya umachaochao ya umachúchuda, ufanmannae y taotao sija gui jalom pechonmiyo; sa ayoja na medida y anae manmide jamyo: infanmamediye talo jamyo.
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
39¶ Ya jasangane sija un acomparasion ilegña: Siña y bachet jaosgaejon y otro bachet? ti ujaachapodong y dos gui joyo?
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40Y disipulo ti taquiloña qui y maestro: lao cada uno ni y cabales, güiya utaegüijija y maestroña.
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41Ya jafa muna unlilie y migo gui atadog y chelumo; ya ti unlilie y jayo gui atadogmo?
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42Ya jafa muna siña unalog ni y chelumo: Chelujo, maela ya junajanao y migo gui atadogmo, yanguin jago ti unlilie y jayo gui atadogmo? Hipocrita jao, yute juyong finena y jayo gui atadogmo, ya ayo nae unlie claro para unnajanao y migo gui atadog y chelumo.
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43Sa taya mauleg na trongco, ni y fanogcha taelaye, ni y taelaye na trongco ni y fanogcha mauleg.
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44Sa cada trongco matungoja pot y tinegchaña. Sa ti ufanmanrecoje y taotao sija igos gui manituca ni ufanmanrecoje ubas gui jalom gadon.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45Y mauleg na taotao, ni y mauleg na guinaja gui corasonña, mañuñule mauleg; ya y taelaye na taotao, ni y taelaye na güinaja gui corasonña, mañuñule taelaye: sa y minegae y corason jasasangan y pachotña.
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46¶ Ya jafa na infananaanyo Señot, Señot, ya ti infatitinas y jusangangane jamyo?
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47Jaye y mato guiya guajo ya jaecungog y sinanganjo ya jafatinas; jufanue jaye parejuña:
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48Parejo yan un taotao ni y manjatsa guma, ya jaguadog tadong ya japolo y simiento gui jilo y fitme na acho; ya yanguin cajulo y manadan janom, ya milag y sadog chineneg ayo na guma; lao ti umayengyong, sa maplanta gui jilo y acho.
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49Lao ayo y umeecungog ya ti jafatinas; parejo yan y taotao ni y manjatsa guma gui jilo oda ya ti janaye simiento; ya anae milag y sadog ya chineneg, enseguidas upodong; ya dangculo y yinilang ayo na guma.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"