1YA despues di munjayan todo y finanagüeña si Jesucristo gui talangan taotao sija, güiya jumalom guiya Capernaum.
1Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.
2Ya y tentago un senturion ni y guefyaña, estaba malango, ya esta para umatae.
2Huko kulikuwa na jemadari mmoja Mroma ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu kufa.
3Lao anae y senturion jajungog na masasangan si Jesus, jatago y manamco na Judios, para umagagao na ufato ya unajomlo y tentagoña.
3Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje amponye mtumishi wake.
4Ya anae manmato as Jesus, guefmagagao ilegñija: Dignogüe na unfatinas este pot güiya:
4Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: "Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,
5Sa jagüaeya y nasionmame ya japlantaye jam sinagoganmame.
5maana analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi."
6Ya manjanao yan si Jesus. Ya anae esta manjijot gui guima y senturion jatago y amiguña sija para ualog as Jesus: Señot chamo ninachachatsaga; sa ti dignoyo na junajalom jao gui papa atofjo;
6Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu kufika nyumbani kwa yule jemadari Mroma, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: "Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.
7Pot este ti jujaso na dignoyo na jufato guiya jago; lao sanganja ya ujomlo y tentagojo.
7Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako; amuru tu, na mtumishi wangu atapona.
8Sa guajo locue na taotao gaegeuyo gui papa y ninasiña, ya guaja gui papajo sendalo sija; yan ileco nu este: Janao, ya mapos; ya y otro: Maela, ya mato; ya y tentagojo: Fatinas este, ya jafatinas.
8Mimi pia ni mtu niliye chini ya mamlaka, na ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda!, naye huenda; namwambia mwingine, Njoo! naye huja; na nikimwambia mtumishi wangu, Fanya hiki!, hufanya."
9Ya anae jajungog si Jesus este, ninamanman nu güiya, ya jabiragüe ilegña ni y linajyan taotao ni y dumalalag güe: Jusangane jamyo na ti jusoda taegüije na dinangculon jinenggue ni iya Israel.
9Yesu aliposikia hayo, alishangaa; halafu akauelekea ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akasema, "Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli."
10Ya anae manalo sija guato gui guima y manmanago, jasoda na jomlo y tentago ni estaba malango.
10Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.
11¶ Ya susede un rato despues di este na, si Jesus jumanao asta un siuda ni mafanaan Nain; ya mañisija yan y disipuluña yan y dangculon manadan taotao.
11Baadaye kidogo Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake pamoja na kundi kubwa la watu waliandamana naye.
12Ya anae esta jijot gui pettan y siuda, estagüe na macocone un matae, güiyaja lajin nanaña, ya biuda locue, ya linajyan taotao siuda mangachongchongña.
12Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya kijana mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.
13Ya anae linie ni y Señot ninamaase nu güiya, ya ilegña nu güiya: Chamo cumacasao.
13Bwana alipomwona mama huyo, alimwonea huruma, akamwambia, "Usilie."
14Ya lumatguato ya japacha y andas; ya y chumuchule mañaga. Ya ilegña: Patgon, guajo jao sumangane, cajulo.
14Kisha akaenda, akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wanalichukua wakasimama. Halafu akasema, "Kijana! Nakuamuru, amka!"
15Ya y estaba matae matachong ya jatutujon cumuentos, ya inentrega as Jesus gui as nanaña.
15Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16Ya ninafanmaaañao todosija, ya maalaba si Yuus ilegñija: Dangculo na profeta esta cajulo entre yya jita: ya, si Yuus jagas jabisita taotaoña.
16Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema: "Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake."
17Ya jumanao este na famaña gui todo yya Judea yan todo oriya y tano.
17Habari hizo zikaenea kote katika Uyahudi na katika nchi za jirani.
18¶ Ya y disipulon Juan masangane güe todo estesija.
18Wanafunzi wa Yohane walimpa habari Yohane juu ya mambo hayo yote. Naye Yohane, baada ya kuwaita wawili kati ya wanafunzi wake,
19Ya jaagang si Juan dos gui disipuluña ya jatago para as Jesus, ilegña: Cao jago yuje y para ufato pat infanmannangga jam otro?
19aliwatuma kwa Bwana wamwulize: "Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
20Ya anae manmato y taotao sija guiya güiya, ilegñija: Si Juan Bautista tumagojam para yya jago, ilegña: Cao jago yuje y para ufato pat infanmannangga jam otro?
20Wale wanafunzi walipomfikia Yesu wakamwambia, "Yohane Mbatizaji ametutuma kwako tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
21Ya ayo mismo na ora, janafanjomlo megae ni y manmalango yan y mangaechetnotsija yan espiritun manaelaye; yan megae na manbachet ninafanmanlie.
21Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena.
22Ya maninepe as Jesus ya ilegña nu sija: Janao yan sangane si Juan ni y liniimiyo yan y jiningogmiyo; sa y manbachet manmanlie, ya y mangojo manmamocat, ya y manategtog mangasgas, ya y mananga manmanjungog, y manmatae manafangajulo, ya umapredica y ibangelio gui mamobble.
22Basi, Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa Habari njema.
23Ya dichoso ayo y ti sumosoda y lugat para umatompo guiya guajo.
23Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami!"
24¶ Ya anae manmapos y mantinago as Juan, jatutujon cumuentuse y taotao sija pot si Juan: Jafa injanagüe jamyo para inlie gui desierto? un piao ni y yinengyong ni y manglo?
24Hapo wajumbe wa Yohane walipokwisha kwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu juu ya Yohane: "Mlikwenda kule jangwani, hivi mlitaka kuona kitu gani? Mlitaka kuona unyasi unaotikiswa na upepo?
25Lao jafa injanagüe jamyo para inlie? un taotao na puru suabe magaguña? Estagüe, ayo sija y manminagagago ni y malagno magago yan manlalâlâ gui guinatbo, gui palasyon y ray nae mañasaga.
25Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevalia mavazi maridadi? La hasha! Wanaovaa mavazi maridadi na kuishi maisha ya anasa, hukaa katika majumba ya wafalme!
26Lao jafa injanagüe para inlie? un profeta? magajet, jusangane jamyo na mas que un profeta.
26Basi, niambieni, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
27Este yuje y esta matugue: Estagüe na jatago y tentagojo gui menan matamo, ni para ufamauleg y chalanmo gui menamo.
27Huyu Yohane ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Hapa ni mtumishi wangu, asema Bwana; ninamtuma akutangulie, akutayarishie njia."
28Jusangane jamyo, na entre ayo sija y manmafañago gui famalaoan, taya dangculoña qui si Juan; lao y diquiqueja gui raenon Yuus dangculoña qui güiya.
28Yesu akamalizia kwa kusema, "Nawaambieni, kati ya binadamu wote hakuna aliye mkubwa zaidi kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa Mungu ni mkubwa zaidi kuliko yeye."
29Ya todo y taotao anae majungog güe, yan y publicano sija, jajustifica si Yuus ya manmatagpange ni y tinagpangen Juan.
29Waliposikia hayo watu wote na watoza ushuru waliusifu wema wa Mungu; hao ndio wale waliokuwa wameupokea ubatizo wa Yohane.
30Lao y Fariseo yan y manmagas y lay, jarechasa y consejon Yuus contra sijaja; sa ti manmatagpange pot güiya.
30Lakini Mafarisayo na walimu wa Sheria walikataa mpango wa Mungu uliowahusu wakakataa kubatizwa na Yohane.
31Ya ilegña: Jafa nae juacompara y taotao este na generasion? ya jafa parejonñija?
31Yesu akaendelea kusema, "Basi, nitawafananisha watu wa kizazi hiki na kitu gani? Ni watu wa namna gani?
32Manparejo yan y famaguon ni manmatatachong gui plasa ya manaagang uno yan otro ya ilegñija: Indadane jamyo flauta, y ti manbaela jamyo, manuugonge jamyo, ya ti manatanges jamyo.
32Ni kama vijana waliokuwa wamekaa sokoni na kuambiana, kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma, lakini hamkucheza! Tumeomboleza, lakini hamkulia!
33Sa mato si Juan Bautista ni uchocho pan ni uguimen bino, ya ilelegmiyo: Guaja anitiña.
33Kwa maana Yohane alikuja, yeye alifunga na hakunywa divai, nanyi mkasema: Amepagawa na pepo!
34Mato y Lajin taotao, ya chumocho yan gumimen, ya ilelegmiyo: Estagüe, un taotao na gachumocho yan gagumimen bino, yan amigon y publicano sija, yan y manisao.
34Akaja Mwana wa Mtu; anakula na kunywa, mkasema: Mwangalieni mlafi huyu na mlevi; rafiki ya watoza ushuru na wenye dhambi!
35Lao y tiningo manacabales ni y todo famaguonña.
35Hata hivyo, hekima ya Mungu imethibitishwa kuwa njema na wote wale wanaoikubali."
36¶ Ya malago uno gui Fariseo sija na ufañija mañocho. Ya jumalom gui guima y Fariseo ya matachong gui lamasa.
36Mfarisayo mmoja alimwalika Yesu kula chakula nyumbani kwake. Akaingia nyumbani mwa huyo Mfarisayo, akakaa kula chakula.
37Ya estagüe, un palaoan gui siuda, na miisao, ya anae jatungo na gaegue si Jesus matatachong gui lamasa gui guima y Fariseo, mañule un boteyan alabastro na ingüente.
37Basi, katika mji ule kulikuwa na mama mmoja aliyekuwa anaishi maisha mabaya. Alipopata habari kwamba Yesu yuko nyumbani kwa huyo Mfarisayo, alichukua chupa ya alabasta yenye marashi.
38Ya tumojgue gui taten Jesus, ya cumasao; ya jatutujon munafotgon ni lagoña y adeng Jesus, ya jasaosao ni y gapuniluña; ya jachichico y adengña ya japapalae ni y inggüente.
38Akaja, akasimama karibu na miguu yake Yesu, akilia, na machozi yake yakamdondokea Yesu miguuni. Huyo mwanamke akaipangusa miguu ya Yesu kwa nywele zake. Kisha akaibusu na kuipaka yale marashi.
39Ya anae jalie este y Fariseo ni y umagange güe, cumuentos gui sumanjalomña, ilelegña: Este na taotao yaguin profeta güe, jatungo jafa este na palaoan y pumapacha güe sa güiya miisao.
39Yule Mfarisayo aliyemwalika Yesu alipoona hayo, akawaza moyoni mwake, "Kama mtu huyu angekuwa kweli nabii angejua huyu mwanamke ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi."
40Ya manope si Jesus ya ilegña nu güiya: Simon, guaja para jasangane jao. Ya güiya ilegña: Sangan Maestro.
40Yesu akamwambia huyo Mfarisayo, "Simoni, ninacho kitu cha kukwambia." Naye Simoni akamwambia, "Ndio Mwalimu, sema." Yesu akasema,
41Un taotao guaja dos dumídibe: ya y uno mandidibe quinientos monedan denario, ya y otro sincuenta.
41"Watu wawili walikuwa wamemkopa mtu fedha: mmoja alikuwa amekopa dinari mia tano, na mwingine hamsini.
42Ya anae taya apasñija, inasie todo y dos. Enao mina, jaye guiya sija mas güinaeya?
42Waliposhindwa kulipa madeni yao, huyo mtu aliwasamehe wote wawili. Sasa ni yupi kati ya hao wawili atampenda zaidi huyo bwana?"
43Manope si Simon, ya ilegña: Y pineloco na ayo y mas maasie; ya güiya ilegña: Tunas jinisgamo.
43Simoni akamjibu, "Ni dhahiri kwamba yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi atampenda zaidi yule bwana." Yesu akamwambia, "Sawa."
44Ya jabira güe guato gui palaoan, ya ilegña as Simon: Unlilie este na palaoan? Jumalomyo gui guimamo, ti unnaeyo janom para y adengjo; lao este janafotgon y adengjo ni lagoña, ya jasaosao ni y gapuniluña.
44Halafu akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, "Unamwona huyu mwanamke, sivyo? Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake.
45Jago ti unnaeyo un chico: lao este na palaoan desde que jumalomyo ti pumapara jachico y adengjo.
45Wewe hukunisalimu kwa kunibusu, lakini huyu mwanamke tangu nilipoingia hapa amekuwa akiibusu miguu yangu.
46Ti unpalae y ilujo ni laña, lao este japalae y adengjom inggüente.
46Wewe hukunionyesha ukarimu wako kwa kunipaka mafuta kichwani, lakini huyu mwanamke amefanya hivyo kwa kunipaka mafuta miguu yangu.
47Enao mina jusangane jao, na y isaoña, ni y megae, umaasie; sa güiya megae maguaeyaña; lao y didide maasiiña, didide maguaeyaña.
47Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo."
48Ya ilegña nu güiya: Y isaomo maasie.
48Basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, "Umesamehewa dhambi zako."
49Ya y mangachochongña manmatachong gui lamasa, jatutujon sumangan gui sumanjalomñija: Jaye este na ufanasie locue isao?
49Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, "Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?"
50Ya ilegña ni palaoan: Y jinengguemo unsinatba; janao yan pas.
50Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, "Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani."