1YA susede un rato despues na jajanaogüe y siuda sija yan y sengsong sija manpredidica, yan numanafanungo nu y ibangelion y raenon Yuus; ya mañisija yan y dose,
1Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
2Ya palo sija famalaoan ni guinin nanafanmagong ni manaelayen espiritu yan y chetnot sija; si Maria ni mafanaan magdalena ni jumuyong guiya güiya siete na manganite,
2Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
3Ya si Juana, asaguan Chusa, mayetdomon Herodes; yan si Susana yan megae ni pumalo ni jasesetbe ni güinajañija:
3Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
4¶ Ya anae mandaña y dangculon linajyan taotao, yan y manestaba cada siuda manmato guiya güiya, jacuentuse pot un acomparasion.
4Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
5Un tátanom jumanao para ufananom y semiyaña; ya anae manmananom, palo podong gui oriyan chalan; ya todo magacha, ya manmato sija y pajaro gui langet ya macano.
5"Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
6Yan palo mamodong gui jilo acho; ya anae lachog, ninamalayo sa ti fofotgon.
6Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
7Yan palo mamodong gui jalom tituca; ya mandoco mañija y tituca, ya chiniguit.
7Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
8Yan palo mamodong gui mauleg y tano; ya mandoco, ya manogcha siento pot uno. Ya anae esta jasangan estesija umagang: Y gaetalanga para ufanjungog, uecungog.
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia." Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, "Mwenye masikio na asikie!"
9¶ Ya y disipuluña sija mafaesen güe: Jafa este na acomparasion?
9Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
10Ya guiya ilegña: Esta manmannae jamyo para intingo y misterion y raenon Yuus lao y pumalo pot acomparasion; para ujaaatanja ya ti ujalie, yan ujaecungogja ya ti ujatungo.
10Naye akajibu, "Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
11Pues este ayo na acomparasion: Y semiya y sinangan Yuus.
11"Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
12Y gui oriyan chalan ayo sija y jagas jumungog; ya despues mato y manganite ya janasuja y sinangan gui corasonñija sa ti mojon ufanmanjonggue ya ufanmasatba.
12Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
13Ya y jilo acho, ayo sija y anae jajungog, jaresibe y sinangan nu y minagof; lao estesija manaejale; sa jajonggue un ratoja, lao anae mato tentasion mamodong.
13Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
14Ya y pedong gui jalom tituca, este sija y jumungog; ya mientras jumanao gui chalanñija, manchiniguit ni inadajeñiñija, yan y güinaja, yan y minagof tano gui este linâlâ, ya ti jumuyong tinegchañija cabales.
14Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
15Lao ayo y mangaegue gui mauleg na tano, este sija na guinin jumungog y sinangan gui corason ni mauleg yan tunas, jamantietiene, ya manogcha yan manpasensia.
15Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
16¶ Ni uno ni mañoñonggue candet, utampe nu y batde pat upolo gui papa catre, lao upolo gui jilo lamasa para y jumajalom ulie y manana.
16"Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
17Sa taya manaatog ya ti umafatanñaejon; ni gae gui secreto ya ti umatungo, ujuyong gui manana.
17"Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
18Guesadaje jaftaemano y jiningogmiyo: sa masquesea jaye y guaja, umanae; lao masquesea jaye y taya, unajanao ayo y pineloña na uguaja.
18"Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa."
19¶ Ayonae manmato guiya güiya si nanaña yan y mañeluña, lao tisiña manlatguato guiya güiya pot y linajyan taotao.
19Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
20Ya masangane, ilegñija nu güiya: Si nanamo yan y mañelumo manmatotojgue gui sanjiyong na manmalago na unmalie.
20Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
21Ya manope ya ilegña nu sija: Y nanajo yan y mañelujo, ayosija y jumungog y sinangan Yuus ya jafatinas.
21Lakini Yesu akawaambia watu wote, "Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika."
22¶ Ya susede y uno gui ayosija jaane nae, na jumalom gui un batco, güiya yan y disipoluña sija; ya ilegña nu sija: Nije tafanjanao y otro banda jagoe; ya manjanao.
22Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, "Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo." Basi, wakaanza safari.
23Ya anae mumamayama sija, güiya maego; ya manguaefe un dangculon, pagyo y manglo gui jagoe; ya bula y batco janom ya mangaegue sija gui peligro.
23Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
24Ya manmato guiya güiya, ya mapangon, ilegñija: Maestro, maestro, tafanmalingo. Ya magmata, ya jalalatde y manglo yan y chaochao y janom; ya pumara, ya jumuyong malinao.
24Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, "Bwana, Bwana! Tunaangamia!" Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
25Ya ilegña nu sija: Mano nae gaegue jinengguenmiyo? Ya sija manmaañao ya ninafanmanman, ilegñija uno yan otro: Jaye este, na asta y manglo yan y janom jatago ya maoosgueja?
25Kisha akawaambia, "Iko wapi imani yenu?" Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, "Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?"
26¶ Ya manmato asta, y tano y taotao Gadara sija, ni gaegue gui sanmenan y Galilea.
26Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
27Ya anae jumanao para y tano, umasoda yan un taotao gui jiyong y siuda na gaemanganite; ya apmam na tiempo ti minagagago ni usaga gui guima, na y naftanja.
27Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
28Ya anae jalie si Jesus, umagang, ya jatombagüe gui menaña ya ilegña ni dangculo na inagang: Para jafayo nu jago Jesus, Lajin Yuus Gueftaquilo? Jusuplica jao na chamoyo sumasapet.
28Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa "We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!"
29Sa jatago y espiritun áplacha na ufanjanao gui taotao; sa apmam na tiempo na maguot güe: mamantiene güe preso ya magode nu y cadena yan tale sija; ya jayamag y guinede ya quinene ni y manganite asta y desierto sija.
29Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
30Ya finaesen as Jesus: Jaye naanmo? Ya güiya ilegña: Linajyan; sa megae na manganite manjalom guiya güiya.
30Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Yeye akajibu, "Jina langu ni Jeshi" --kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
31Ya masuplica güe na chaña tumatago na ufanjanao para y tadong na joyo.
31Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho.
32Ya estaba güije un inetnon babue na lajyan na mañochocho gui jalom tano: ya masuplica güe na ufanpinelo ya ufanjalom güije sija. Ya manpinelo.
32Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
33Ya anae manjuyong y manganite gui taotao, manjalom gui babue ya y inetnon manmanunugo sajyao guato gui un didog gui jagoe ya manmatmos.
33Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
34Ya ayo sija munafañochocho y babue anae jalie y mafatinas, manmapos ya jasangane y taotao siuda yan gui fangualuan.
34Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
35Ya manjanao para ujalie y mafatinas; ya manmato gui as Jesus; ya masoda y taotao ni anae guinin jumuyong y manganite, na minagagago ya guaja jinasoña cabales, ya matatachong gui adeng Jesus; ya ninafanmaañao.
35Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
36Ya mansinangane ni lumie, jafa taemano manamagongña ayo y guinin jinatme manganite.
36Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
37¶ Ayonae todo y taotao gui tano y Gadarenos yan todo y oriyan, magagao na ujanao guiya sija; sa mansenmaañao; ya güiya cajulo gui batco ya tumalo tate.
37Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
38Lao ayo na taotao anae guinun manjuyong y manganite, siniplica güe para usaga guiya güiya; lao janajanao ya ilegña:
38Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
39Talo guato guiya jamyo ya unfañangane jaftaemano na dangculon güinaja finatinasña si Yuus nu jago. Ya guiña jumanao, ya jasanganñaejon todo gui siuda jaftaemano finatinasña si Jesus nu güiya.
39"Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea." Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
40¶ Ya anae tumalo guato si Jesus maresibe ni y linajyan taotao sija ya mangosmagof; sa todoja numananggaja.
40Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
41Ya estagüe, un taotao na y naanña si Jairo, ya güiya locue magas y sinagoga; mato ya jatombagüe papa gui adeng Jesus, ya jagagao na ujalom gui guimaña.
41Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
42Sa guaja unoja jagaña na esta guaja dose años, ya estaba jijot na umatae. Ya anae jumanao maapupura güe ni linajyan taotao sija.
42kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
43¶ Ya un palaoan na numanajuyong jâgâ esta dose años, esta jalachae gumasta todo y güinajaña ni jaapaseñaejon medico, lao taya siña munamagong,
43Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
44Mato gui tateña ya japacha y madoblan magaguña, ya enseguidas esta bumasta y jâgâña.
44Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
45Ayonae si Jesus ilegña: Jayeyo pumacha? Lao anae todos japune ilegña si Pedro yan y mangachongña: Maestro, y linajyan taotao umanoriya jao yan machichiguit jao,
45Yesu akasema, "Ni nani aliyenigusa?" Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, "Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!"
46Lao si Jesus ilegña: Guajayo pumacha; sa guajo jutungo na guaja ninasiña jumuyong guiya guajo.
46Lakini Yesu akasema, "Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka."
47Ayonae y palaoan anae jalie na ti siña janaatog, mato ya manlalaolao, ya jatombagüe gui menaña, ya jasangan gui menan y taotao sija todos, pot jafa na japacha, yan jaftaemano na ninajomlo enseguidas.
47Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
48Ya ilegña nu güiya: Hija, y jinengguemo unninajomlo; janao ya upas.
48Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani."
49¶ Ya mientras cumuecuentos, mato uno ni taotao y magas y sinagoga ya ilegña: Y jagamo matae, chamo umestototba y Maestro.
49Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: "Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?"
50Ya anae jajungog si Jesus manopegüe: Chamo maaañao; jonggueja sa güiya ujomlo.
50Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, "Usiogope; amini tu, naye atapona."
51Ya anae mato gui guima, taya japolo na ujalom yan güiya na si Pedro, si Juan, yan si Santiago, yan y tatan y patgon, yan y nanaña.
51Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
52Ya todos mangacasao, yan malamementagüe; lao ilegña: Chamiyo fangacasao; sa ti matae, lao mamaego.
52Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, "Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!"
53Ya macháchatgue güe, sa matungoja na esta matae.
53Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
54Lao güiya jamantiene y canaeña ya jaagang ilegña: Patgon palaoan, cajulo.
54Lakini Yesu akamshika mkono akasema, "Mtoto amka!"
55Ya mato y espirituña talo, ya enseguidas cajulo; ya manago na umanachocho.
55Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
56Ya ninafanmanman y mañaenaña: lao jaencatga na chañija sumangangane ni un taotao jafa y mafatinas.
56Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.