1YA jaagang ya mandaña y dose disipuluña ya janae ninasiña gui jilo y manganite todo, yan para ufanmanamte nu y chetnot sija.
1Yesu aliwaita wale kumi na wawili, akawapa uwezo juu ya pepo wote, na uwezo wa kuponya wagonjwa.
2Ya jatago na ujapredica y raenon Yuus, yan unafanjomlo y manmalango.
2Halafu akawatuma waende kuhubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
3Ya ilegña nu sija: Chamiyo fanmañuñule ni jafa para y chalan, ni baston, ni botsa, ni pan, ni salape; ni infangaemagago dos.
3Akawaambia, "Mnaposafiri msichukue chochote: msichukue fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha, wala hata koti la ziada.
4Ya cuatquiera na guma nae manjalom jamyo, fañaga güije asta que manjanao jamyo.
4Nyumba yoyote mtakayoingia na kukaribishwa, kaeni humo mpaka mtakapoondoka katika kijiji hicho.
5Ya todo ayo sija y ti rumesibe jamyo, anae manjanao jamyo güije na siuda, sacude y petbos gui adengmiyo para testimonio contra sija.
5Watu wakikataa kuwakaribisha, tokeni katika mji huo, nanyi mnapotoka kung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao."
6Ya manjanao sija, ya manmalofan sija gui sengsong, mapredidica y ibangelio, yan mannanajomlo gui todo y lugat.
6Basi, wakaanza safari, wakapitia vijijini wakihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
7Lao si Herodes tetrarca jajungog masangan este sija na finatinas, ya estaba guefinestotba ni y sinañgan palo na si Juan esta cumajulo guinin manmatae.
7Sasa, mtawala Herode, alipata habari za mambo yote yaliyokuwa yanatendeka, akawa na wasiwasi kwa vile walikuwa wakisema: "Yohane amefufuka kutoka wafu!"
8Ya y pumalo ilegñija: Si Elias jumuyong talo; ya otros umalog; na uno gui manamco na profeta lâlâ talo.
8Wengine walisema kwamba Eliya ametokea, na wengine walisema kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amerudi duniani.
9Ya ilegña si Herodes: Si Juan guajo dumegüeya; ya jaye este nae jujungog sija na güinaja? Ya japrocura lumie güe.
9Lakini Herode akasema, "Huyo Yohane nilimkata kichwa; sasa ni nani huyu ninayesikia habari zake?" Akawa na hamu ya kumwona.
10¶ Ya anae manalo guato y apostoles sija, masangane güe todo ni y finatinasñija. Ya jacone sija ya mañuja asta un banda, gui un siuda ni mafanaan Betsaida.
10Wale mitume waliporudi, walimweleza yote waliyoyafanya. Yesu akawachukua, wakaenda peke yao mjini Bethsaida.
11Ya anae esta matungo ni y linajyan taotao sija, madálalag güe; ya güiya jaresibe, ya jasangane ni y raenon Yuus; ya janafanjomlo y numesesita manmaamte.
11Lakini wale watu walipojua alikokwenda, walimfuata. Yesu akawakaribisha akawazungumzia juu ya Ufalme wa Mungu, akawaponya wale waliohitaji kuponywa.
12Ya y jaane jatutujon pumuenge; ya mafatoigüe nu y dose ya ilegñija nu güiya: Nafanjanao, y linajyan taotao, para ufanjanao asta y sengsong yan y fangualuan gui oriya, ya ufañaga ya ufanmanaligao nañija; sa mangaeguejit güine gui desierto na lugat.
12Jua lilipokuwa linaanza kutua, wale kumi na wawili walimwendea wakamwambia, "Waage watu waende kwenye vijiji na mashamba ya karibu, wakajipatie chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tulipo ni nyikani."
13Ya ilegña nu sija: Jamyo innafañocho. Ya ilegñija: Taya guajata na sincoja na pan yan dos güijan, patsino nije tafanjanao tafanmamajan nengcano para todo este sija na taotao.
13Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Wakamjibu, "Hatuna chochote ila mikate mitano na samaki wawili. Labda twende wenyewe tukawanunulie chakula watu wote hawa!"
14Ya guaja buente sinco mit na taotao. Ya ilegña ni disipuluña: Nafanmatachong pot compania, cada compania sincuenta.
14(Walikuwepo pale wanaume wapatao elfu tano.) Basi, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Waambieni watu waketi katika makundi ya watu hamsinihamsini."
15Ya taegüije mafatinas, ya mannafamatachong todos.
15Wanafunzi wakafanya walivyoambiwa, wakawaketisha wote.
16Ya jachule y sinco na pan yan y dos güijan, ya jaatan julo y langet ya jabendise ya jaipe; ya janae y disipoluña para upolo gui menan y linajyan taotao.
16Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu.
17Ya mañocho ya manjaspog todos; ya esta majatsa y sebla y pedaso sija, dose canastra.
17Wakala wote, wakashiba; wakakusanya makombo ya chakula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
18¶ Ya susede, anae mananaetae güiyaja namaesa, estabaja mangaegue guiya güiya y disipuluña, ya jafaesensija, ilegña: Jaye ilegñiñija y taotao nu guajo?
18Siku moja, Yesu alikuwa anasali peke yake, na wanafunzi wake walikuwa karibu. Basi, akawauliza, "Eti watu wanasema mimi ni nani?"
19Ya sija manmanope ya ilegñija: Si Juan Bautista; lao guaja umalog: Si Elias; yan palo umalog na uno gui manamco na profeta lâlâ talo.
19Nao wakamjibu, "Wengine wanasema kuwa wewe ni Yohane mbatizaji, wengine wanasema wewe ni Eliya, hali wengine wanasema kuwa wewe ni mmoja wa manabii wa kale ambaye amefufuka."
20Ya ilegña nu sija: Lao jamyo, jaye ilegmimiyo nu guajo? Ya manope si Simon Pedro ya ilegña: Si Cristo, gui as Yuus.
20Hapo akawauliza, "Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?" Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo wa Mungu."
21Ya manguenesencatga sija ya jatago na chañija sumangangane ni jaye nu este;
21Halafu Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hiyo.
22Ilegña: Y Lajin taotao nesesita ufamadese megae, ya umarechasa ni y manamco sija, yan y manmagas y mamale yan y escriba sija, ya umapuno ya umanacajulo gui mina tres na jaane.
22Akaendelea kusema: "Ni lazima Mwana wa Mtu apate mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria; atauawa, lakini siku ya tatu atafufuliwa."
23Ya ilegña nu sija todos: Yaguin guaja y malago tumatiyego, upunenaesa güe, ya uchule y quiluusña cada jaane ya udalalagyo.
23Kisha akawaambia watu wote, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane nafsi yake, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
24Sa masqueseaja jaye y malago na usatba y linâlâña, ufinalingaeguan; ya masquesea jaye y malingo y linâlâña pot y naanjo, güiya usatba.
24Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza; lakini atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayaokoa.
25Sa jafa probechoña y taotao yaguin jagana todo y tano, ya güiya unafalingo maesa güe pat uyulang maesa gue?
25Je, kuna faida gani mtu kuupata utajiri wote wa dunia kwa kujipoteza au kujiangamiza yeye mwenyewe?
26Sa masqueseaja jaye pot y mamajlao guajo yan pot y sinanganjo, mamajlao locue nu este y Lajin taotao, yaguin mato gui minalagña yan y minalag tata yan y mañantos na angjet sija.
26Mtu akinionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu.
27Lao magajet jusangane jamyo: Na guaja palo gui mangaegue güine, na ti uchague y finatae asta que ujalie y raenon Yuus.
27Nawaambieni kweli, kuna wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu."
28¶ Ya susede mina ocho na jaane, despues di estesija na sinangan, jacone mañija yan Pedro, yan si Juan, yan si Santiago, ya cajulo gui egso ni taquilo para ufanaetae.
28Yapata siku nane baada ya kusema hayo, Yesu aliwachukua Petro, Yohane na Yakobo, akaenda nao mlimani kusali.
29Ya mientras mananaetae güe, y jechuran mataña tolaeca; ya y magaguña jumuyong apaca ya malag.
29Alipokuwa akisali, sura yake ilibadilika, mavazi yake yakawa meupe na kung'aa sana.
30Ya, estagüe, dos taotao na cumuecuentos yan güiya; ya si Moises, yan Elias,
30Na watu wawili wakaonekana wakizungumza naye, nao ni Mose na Eliya,
31Ya manjuyong yan y minalagñija, ya manguecuentos pot y jinanaoña, na para ucumple guiya Jerusalem.
31ambao walitokea wakiwa wenye utukufu, wakazungumza naye juu ya kifo chake ambacho angekikamilisha huko Yerusalemu.
32Lao si Pedro yan y mangachogña, mansenmatujog; ya anae manmagmata, malie y minalagña yan ayo na dos taotao ni mangachongña.
32Petro na wenzake walikuwa wamelemewa na usingizi mzito, hata hivyo waliamka, wakauona utukufu wake, wakawaona na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33Ya susede, mientras sumusuja sija guiya güiya, si Pedro ilegña as Jesus: Maestro, maulegñaja tafañaga güine; ya nije tafanmamatinas tres na tabetnaculo; uno para jago, uno para si Moises, yan uno para si Elias; ti jatungo jafa jasasangan.
33Basi, watu hao wawili walipokuwa wakiondoka, Petro alimwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri kwamba tupo hapa: basi, tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya." --Kwa kweli hakujua anasema nini.
34Ya mientras jasasangan este, mato un mapagajes ya mantinampe; ya ninafanguefmaañao anae manjalom gui mapagajes.
34Petro alipokuwa akisema hayo, mara wingu likatokea na kuwafunika; na wingu hilo lilipowajia, wale wanafunzi waliogopa sana.
35Ya mato un inagang gui mapagajes na ilegña: Este y lajijo, inayigco; ecungog güe.
35Sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ndiye Mwanangu niliyemchagua, msikilizeni."
36Ya anae malofan ayo na inagang, esta masoda si Jesucristo güigüiyaja namaesa; ya sija manmamatquiloja, ya güije sija na jaane, taya jasangane ni jaye pot y liniiñija.
36Baada ya hiyo sauti kusikika, Yesu alionekana akiwa peke yake. Wanafunzi walikaa kimya juu ya tukio hilo, na wakati ule hawakumwambia mtu yeyote mambo hayo waliyoyaona.
37¶ Ya susede inagpaña güije na jaane, anae manunog guinin y egso, ya y dangculon linajyan taotao masoda güe.
37Kesho yake walipokuwa wakishuka kutoka kule mlimani, kundi kubwa la watu lilikutana na Yesu.
38Ya, estagüe, un taotao gui entalo y linajyan, na umagang ilegña: Maestro jutayuyut jao na unlie y lajijo; sa y unoja patgonjo:
38Hapo, mtu mmoja katika lile kundi akapaaza sauti, akasema, "Mwalimu! Ninakusihi umwangalie mwanangu--mwanangu wa pekee!
39Sa, estagüe, un espiritu na quinene, ya enseguidas umagang; ya ninalaolao güe ya numanajuyong buo, ya aapmam na pinadese na sumuja guiya güiya, na ninalalamenja,
39Pepo huwa anamshambulia, na mara humfanya apige kelele; humtia kifafa, na povu likamtoka kinywani. Huendelea kumtesa sana, asimwache upesi.
40Ya guinin jutayuyut y disipulumo na ujayute juyong; ya ti manasiña.
40Niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze, lakini hawakuweza."
41Ya manope si Jesus ya ilegña: O generasion na ti manjonggue, yan manchatpayon! asta ngaean nae utafanjijita, ya jujasusungon jamyo? conieyo fan mague ni y lajimo.
41Yesu akasema, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini?" Kisha akamwambia huyo mtu, "Mlete mtoto wako hapa."
42Lao anae mámamamaela, y anite yinite papa ya guefninalaolao. Lao si Jesus jalalatde y espiritun áplacha ya janajomlo y patgon ya janatalo guato as tataña.
42Wakati mtoto huyo alipokuwa anamjia Yesu, yule pepo alimwangusha chini na kumtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu akamponya mtoto na kumkabidhi kwa baba yake.
43Ya todos ninafanman nu y minagas Yuus, lao mientras manmamanman todos pot todo estesija ni y jafatinas, ilegña ni disipuluña;
43Watu wote wakashangazwa na uwezo mkuu wa Mungu. Wale watu walipokuwa bado wanashangaa juu ya mambo yote aliyofanya, Yesu aliwaambia wanafunzi wake,
44Polo ya utatcalon gui talanganmiyo este sija na sinangan: sa umaentrega y Lajin taotao gui canae taotao sija.
44"Tegeni masikio, myasikie mambo haya: Mwana wa Mtu anakwenda kutiwa mikononi mwa watu."
45Lao sija ti jatungo este na sinangan, ya manafaninatogüe para chañija tumutungo: ya manmaañao mafaesen güe ni ayo na sinangan.
45Lakini wao hawakuelewa maana ya usemi huo. Jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao ili wasitambue; nao wakaogopa kumwuliza juu ya msemo huo.
46¶ Ya jumuyong manafaesen entre sija, jaye guiya sija udangculoña.
46Kukatokea majadiliano kati ya wale wanafunzi kuhusu nani kati yao aliyekuwa mkuu zaidi.
47Lao si Jesus anae jaliija y jinason y corasonñija, jacone un patgon ya japolo gui bandaña,
47Yesu aliyajua mawazo yaliyokuwa mioyoni mwao; basi akamchukua mtoto mdogo akamweka karibu naye,
48Ya ilegña nu sija: Jaye y rumesibe este na patgon pot naanjo jaresibeyo; ya y rumesibeyo, jaresibe y tumagoyo; sa jaye y mas diquique guiya jamyo, ayo dangculo.
48akawaambia, "Mtu yeyote anayempokea mtoto huyu mdogo kwa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma. Maana yule aliye mdogo kuliko wote kati yenu ndiye aliye mkubwa kuliko wote."
49¶ Ya manope si Juan ya ilegña: Maestro inlie uno na manyuyute juyong y manganite pot y naanmo; ya inchema sa ti jadadalalagjit.
49Yohane alidakia na kusema, "Bwana, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
50Ya ilegña si Jesus ni sija; chamiyo chumochoma, sa ayo ni ti contra jamyo, guiya para jamyo.
50Lakini Yesu akamwambia, "Msimkataze; kwani asiyepingana nanyi yuko upande wenu."
51¶ Ya susede, anae mato y jaane nae jijot para umaresibe gui sanjilo; janameton y mataña para ujanao para Jerusalem,
51Wakati ulipokaribia ambapo Yesu angechukuliwa juu mbinguni, yeye alikata shauri kwenda Yerusalemu.
52Ya manago tentago sija na ufanmofona gui menaña; ya majanao manjalom gui un songsong Samaritano, para umanalistuye güe güije.
52Basi, akawatuma wajumbe wamtangulie, nao wakaenda wakaingia kijiji kimoja cha Wasamaria ili wamtayarishie mahali.
53Ya ti maresibe güe, sa y mataña meton para ujananao para Jerusalem.
53Lakini wenyeji wa hapo hawakutaka kumpokea kwa sababu alikuwa anaelekea Yerusalemu.
54Ya anae malie este ni disipuluña, si Santiago, yan si Juan, ilegñija: Señot, malago jao ya utafanmanago ya utunog guafe guinin y langet, ya ufanlinachae?
54Basi, wanafunzi wake, kina Yohane na Yakobo, walipoona hayo, wakasema, "Bwana, wataka tuamuru moto ushuke kutoka mbinguni uwateketeze?"
55Ayonae jabira güe ya manlinalatde.
55Lakini yeye akawageukia, akawakemea akasema, "Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo;
56Ya manjanao para y otro songsong.
56kwa maana Mwana wa Mtu hakuja kuyaangamiza maisha ya watu, bali kuyaokoa." Wakatoka, wakaenda kijiji kingine.
57¶ Ya anae manjajanao sija, un taotao ilegña nu güiya gui chalan: Señot, bae judalalagjao manoja y unjanao guato.
57Walipokuwa wakisafiri njiani, mtu mmoja akamwambia Yesu, "Nitakufuata kokote utakakokwenda."
58Ya ilegña si Jesus nu güiya: Y sora sija mangaeliyang, ya y pajaro sija gui langet mangaechenchon; lao y Lajin taotao taya sangaña ni anae para upolo y iluña.
58Yesu akasema, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
59Ya ilegña ni otro: Dalalagyo. Ya güiya ilegña; Señot, sottayo naya ya finenana jujanao ya jujafot si tatamo.
59Kisha akamwambia mtu mwingine, "Nifuate." Lakini huyo akasema, "Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu."
60Lao ilegña nu güiya: Polo y manmatae ya ufanajafot y manmataeñija; lao jago janao ya unpredica y raenon Yuus.
60Yesu akamwambia, "Waache wafu wazike wafu wao; bali wewe nenda ukatangaze Ufalme wa Mungu."
61Ya ilegña locue otro; judalalagja jao Señot; lao sottayo naya ya judespideyo ni y mangaegue guiya jame.
61Na mtu mwingine akamwambia, "Nitakufuata, lakini niruhusu kwanza nikawaage wale walio nyumbani kwangu."
62Ya ilegña si Jesus: Ni uno ni pumopolo y canae gui alado ya uatan tateña ni y digno para y raenon Yuus.
62Yesu akamwambia, "Yeyote anayeshika jembe tayari kulima na huku anaangalia nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu."