Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Matthew

13

1AYO na jaane, jinanaoña si Jesus gui guima, matachong gui oriyan tase.
1Siku hiyohiyo, Yesu alitoka katika ile nyumba, akaenda na kuketi kando ya ziwa.
2Ya mato guiya güiya dangculo na linajyan taotao; ya jumalom güe gui un batco, ya matachong; ya todo y linajyan taotao manmatachong gui oriyan unae.
2Makundi makubwa ya watu yalimzunguka hata Yesu akapanda mashua, akaketi. Hao watu walisimama kwenye ukingo wa ziwa,
3Ya jacuentuse sija megae na acomparasion, ilegña: Estagüe y tátanom na jumuyong para ufananom.
3naye Yesu akawaambia mambo mengi kwa mifano. "Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4Ya anae manananom, palo gui semiya manpodong gui oriyan chalan, ya manmato y pájaro sija ya macano.
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5Palo gui semiya manpodong gui jilo acho na lugat, na ti megae odaña; ya doco ti apmam, sa ti tadong papa gui eda.
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6Lao anae manina y atdao, mansinenggue sa taejale, ya ninamalayo.
6Jua lilipochomoza, zilichomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7Ya palo mamodong gui entalo títuca sija ya mandoco y títuca ya chiniguet.
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga.
8Ya palo manpodong gui mauleg na oda, ya manmanogcha; y uno siento, y otro sesenta, y otro treinta.
8Lakini nyingine zilianguka penye udongo mzuri, zikaota, zikazaa: nyingine punje mia moja, nyingine sitini na nyingine thelathini.
9Y gaetalanga para ufanjungog, güiya ujungog.
9Mwenye masikio na asikie!"
10Ayo nae manmato y disipuluña sija ya ilegñija: Jafajao na cumuecuentuse sija pot acomparasion sija?
10Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwuliza, "Kwa nini unasema na watu kwa mifano?"
11Ya güiya manope ilegña. Sa esta manmanae jamyo, para intingo y misterion y raenon langet, lao sija ti ufanmanae.
11Yesu akawajibu, "Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakujaliwa.
12Sa jayeja y guaja, umanae para uguaja mas; lao ayo y taya iyoña, achog uguaja y iyoña, umachule.
12Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa; lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
13Enaomina jucuentuse sija pot acomparasion; sa y manmanaatan, ya ti manmanlie, ya manecungog, ya ti manmanjujungog, ni ujatungo.
13Ndiyo maana ninasema nao kwa mifano, kwa sababu wanatazama lakini hawaoni, wanasikiliza lakini hawasikii, wala hawaelewi.
14Y ya sija nae umacumple y sinangan Isaias ni ilegña: Anae manmanjujungog, ujungog ya ti utungo; ya anae manmanaatan, ufanmanlie, ya ti ujasiente.
14Kwao yametimia yale aliyosema nabii Isaya: Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
15Sa y corasonñija este na taotao sija manmacat, ya y talangañija mapot manmanjungog, ya y atadogñija jajujuchom; para chañija fanmanlilie ni atadogñija, yan ufanmanjungog ni talangañija, ya ujatungo ni corasonñija, ya ujatolaeca sija, ya guajo junajomlo sija.
15Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameyaziba masikio yao, wameyafumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao. wangesikia kwa masikio yao, wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.
16Lao mandichoso y atadogmiyo, sa manmanlie, yan y talanganmiyo sa manmanjungog.
16"Lakini heri yenu ninyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia.
17Sa magajet jusangane jamyo, na megae na profeta, yan manunas na taotao jagasja manmalago na ujalie y liniinmiyo, ya ti jalie; yan ujajungog y jiningogmiyo, ya ti jajungog.
17Kweli nawaambieni, manabii na watu wengi wema walitamani kuyaona yale mnayoyaona, wasiyaone, na kuyasikia yale mnayoyasikia, wasiyasikie.
18¶ Ecungog jamyo y acomparision y tátanom.
18"Basi, ninyi sikilizeni maana ya mfano huo wa mpanzi.
19Jayeja y umecungog y sinangan y raeno, ya ti jatungo, mato y Taelaye ya janajanao y esta matanme gui corasonña. Este yuje semiya ni y pedong gui oriyan chalan.
19Yeyote asikiaye ujumbe wa ufalme bila kuuelewa, ni kama zile mbegu zilizoanguka njiani; yule Mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake.
20Ya ayo y matanme gui jilo acho na lugat, este yuje y jumungog y sinangan, ya jaresibe ni y minagofña.
20Ile mbegu iliyopandwa penye mawe ni mfano wa mtu asikiaye ujumbe huo na mara akaupokea kwa furaha.
21Lao taya jale guiya güiya, ya gaegue un ratoja; sa anae mato y triniste yan minamajlao pot causan di y sinangan, ti apmam matompo gui isao.
21Lakini haumwingii na kuwa na mizizi ndani yake; huendelea kuuzingatia ujumbe huo kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya ujumbe huo, anakata tamaa mara.
22Ya ayo y matanme gui entalo títuca sija; este yuje y jumungog y sinangan; lao y inadajiña ni y tano, yan dinague ni güinaja, jañucot y sinangan ya sumaga sin tinegchaña.
22Ile mbegu iliyoanguka kati ya miti ya miiba, ni mfano wa mtu asikiaye huo ujumbe, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu na anasa za mali huusonga ujumbe huo, naye hazai matunda.
23Lao ayo y matanme gui mauleg na oda; este yuje y jumungog y sinangan ya jatungo, ya manogcha locue; ya y tinegchaña y uno siento, ya y otro sesenta, ya y otro treinta.
23Ile mbegu iliyopandwa katika udongo mzuri ni mfano wa mtu ausikiaye ujumbe huo na kuuelewa, naye huzaa matunda; mmoja mia, mwingine sitini na mwingine thelathini."
24¶ Otro acomparasion jasangane sija ilegña: Y raenon langet parejoja yan un taotao ni manananom gui fangualuanña, mauleg na semiya.
24Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
25Ya y tiempo nae manmamaego y taotao sija, mato y enemigo ya jatanme y taelaye na chaguan gui entalo y trigo, ya mapos.
25Lakini watu wakiwa wamelala, adui yake akaja akapanda magugu kati ya ngano, akaenda zake.
26Ya anae mandoco y trigo ya manmanogcha, y taelaye na chaguan mandoco locue.
26Basi, mimea ilipoota na kuanza kuchanua, magugu pia yakaanza kuonekana.
27Ya manmato y tentago y tatan familia ya ilegñija nu güiya: Señot, ada ti mauleg na semiya tinanommo gui fangualuanmo? Jafa mina guaja taelaye na chaguan?
27Watumishi wa yule mwenye shamba wakamwendea, wakamwambia, Mheshimiwa, bila shaka ulipanda mbegu nzuri katika shamba lako. Sasa magugu yametoka wapi?
28Ylegña nu sija: Un enemigo fumatinas este. Ya y tentagoña ilegñija nu güiya: Malagojao ya infanjanao ya inchile?
28Yeye akawajibu, Adui ndiye aliyefanya hivyo. Basi, watumishi wake wakamwuliza, Je, unataka twende tukayang'oe
29Ylegña: Munga, sa no sea yaguin inchile y taelaye na chaguan, innabineog locue y trigo.
29Naye akawajibu, La, msije labda mnapokusanya magugu, mkang'oa na ngano pia.
30Polo ya ufandaña mandoco sija na dos asta y quineco; an mato y tiempon quineco, bae jualog ni para ufanmangoco: Chile finena y taelaye na chaguan, ya inguede famanojo para umasonggue; ya y trigo polo gui jalom y camalinjo.
30Acheni vikue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji: kusanyeni kwanza magugu mkayafunge mafungumafungu ya kuchomwa. Lakini ngano ikusanyeni mkaiweke ghalani mwangu."
31¶ Otro acomparasion sinangane sija ilegña: Y raenon langet parejoja yan y pepitas y mostasa, ni jachule un taotao ya jatanme gui fangualuanña.
31Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja, akaipanda katika shamba lake.
32Magajet na güiya mas diquique gui todo y semiya sija; lao anae esta mandoco, güiya mas dangculo gui manmagogulae, ya mamatrongconjayo, ya manmato sija y pájaron y aire, ya manmamatinas y chenchon gui ramasña.
32Yenyewe ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini ikishaota huwa kubwa kuliko mimea yote. Hukua ikawa mti, na ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake."
33¶ Otro acomparasion sinangane sija ilegña: Y raenon langet, parejoja yan y libadura, ni y un palaoan jachule ya janana gui tres medidan arina, asta qui todo manbolacho.
33Yesu akawaambia mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyotwaa mama mmoja, akaichanganya na unga pishi tatu, hata unga wote ukaumuka."
34Todo estesija jasangan si Jesus pot acomparasion gui linajyan taotao; ya taya jasangane sija sin acomparasion.
34Yesu aliwaambia watu hayo yote kwa mifano. Hakuwaambia chochote bila kutumia mifano,
35Para umacumple y munjayan masangan pot y profeta na ilegña: Jubaba y pachotto pot acomparasion: ya jusangan güinaja sija ni manafanatog desde y plinantan y tano.
35ili jambo lililonenwa na nabii litimie: "Nitasema kwa mifano; nitawaambia mambo yaliyofichika tangu kuumbwa ulimwengu."
36Ayo nae jadingo y linajyan taotao ya mapos, ya jumalon gui guima; ya manmato guiya güiya y disipuluña sija, ya ilegñija: Naclaruyejam ni y acomparasion y taelaye na chaguan gui fangualuan.
36Kisha Yesu aliwaaga wale watu, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, "Tufafanulie ule mfano wa magugu shambani."
37Ya manope sija ilegña: Ayo y mananom mauleg na semiya y Lajin taotao yuje.
37Yesu akawaambia, "Mpanzi wa zile mbegu nzuri ni Mwana wa Mtu.
38Y fangualuan, y tano; y manmauleg na semiya, y famaguon y raeno, ya y taelaye na chaguan y famaguon y Maligno.
38Lile shamba ni ulimwengu. Zile mbegu nzuri ni watu wale ambao Ufalme ni wao. Lakini yale magugu ni wale watu wa yule Mwovu.
39Y enemigo, ni y tumanme, y anitegüe; ya y quineco, y jinecog y siglo; ya y para ufanmangone, y angjet sija.
39Adui aliyepanda yale magugu ni Ibilisi. Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika.
40Sa taegüenao machule y taelaye na chaguan ya masonggue gui guafe, taegüijija locue y jinecog y siglo.
40Kama vile magugu yanavyokusanywa kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati;
41Ya utago y Lajin taotao y angjetña sija; ya urecoje todo ayo sija y fumatitinas y tinempo, yan y fumatitinas y tinaelaye;
41Mwana wa Mtu atawatuma malaika wake wawakusanye kutoka katika Ufalme wake wale wote wenye kusababisha dhambi, na wote wenye kutenda maovu,
42Ya uyute gui jetnon guafe; ya ayo nae uguaja tumanges, yan chegcheg nifen.
42na kuwatupa katika tanuru ya moto, na huko watalia na kusaga meno.
43Ayo nae y manunas, ufanmanina calang y atdao, gui raenon y Tatanñija. Y gaetalanga para ufanjungog, güiya ujungog.
43Kisha, wale wema watang'ara kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Sikieni basi, kama mna masikio!
44¶ Y raenon langet locue, parejoja yan un senguaguan na güinaja ni y mananana gui un fangualuan, ya un taotao, anae jasoda, janana, ya mapos yan pot y minagofña jabende todo y iyoña ya jafajan ayo na fangualuan.
44"Ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu mmoja aliigundua, akaificha tena. Alifurahi sana hata akaenda kuuza yote aliyokuwa nayo, akalinunua shamba lile.
45¶ Y raenon langet parejoja locue yan un taotao ni manbebende, na manaliligao bonito na petlas:
45"Tena, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara mmoja mwenye kutafuta lulu nzuri.
46Ya anae mañoda un petlas na senguaguan, mapos ya jabende todo y güinajaña ya jafajan ayo.
46Alipopata lulu moja ya thamani kubwa, alienda akauza yote aliyokuwa nayo, akainunua lulu ile.
47¶ Y raenon langet parejoja locue, yan un lagua ni y mayute guato gui tase, ya mangone todo clase:
47"Tena, Ufalme wa mbinguni unafanana na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina.
48Ya anae esta bula, majala guato gui oriyan unae; ya manmatachong, ya majoca y manmauleg ya masajguane gui sajguanñija, ya y manaelaye mayute juyong.
48Ulipojaa, watu waliuvuta pwani, wakaketi, wakachagua samaki wazuri wakawaweka ndani ya vikapu vyao, na wabaya wakawatupa.
49Taegüinija locue y jinecog y siglo: ufato y angiet sija ya ujanafanjanao y manaelaye gui entalo y manunas;
49Ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati: malaika watatokea, watawatenganisha watu wabaya na watu wema,
50Ya ujayute gui jetnon guafe; ya ayo nae uguaja güije tumanges, yan chegcheg nifen.
50na kuwatupa hao wabaya katika tanuru ya moto. Huko watalia na kusaga meno."
51Ayo nae si Jesus ilegña nu sija: Intingo todo estesija? Sija ilegñija nu guiya: Junggan.
51Yesu akawauliza, "Je, mmeelewa mambo haya yote?" Wakamjibu, "Naam."
52Ya güiya ilegña nu sija: Pot este todo escriba ni mafatinas disipulo gui raenon langet, parejoja yan y tatan un familia, ni y jachuchule gui güinajaña bijo sija, yan nuebo sija.
52Naye akawaambia, "Hivyo basi, kila mwalimu wa Sheria aliye mwanafunzi wa Ufalme wa mbinguni anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale."
53¶ Ya anae janafonjayan si Jesus todo este sija na acomparasion, mapos güije.
53Yesu alipomaliza kusema mifano hiyo alitoka mahali hapo,
54Ya anae mato gui tanoña, mamanagüe gui guimayuusñija, ya sija ninafanmanman, ya ilegñija: Guine mano nae jumuyong este na tiningoña, ya este sija mandangculo na ninasiña?
54akaenda kijijini kwake. Huko akawa anawafundisha watu katika sunagogi hata wakashangaa, wakasema, "Huyu amepata wapi hekima hii na maajabu?
55Ada ti güiya este y lajin y catpintero? Ada si nanaña ti mafanaan si Maria? yan y mañeluña, ti sija si Santiago, si José, si Simon, yan si Judas?
55Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56Ya ada ti manjijita yan y mañeluña palaoan? Guine mano nae uguaja este na taotao todo estesija? Ya guaja guiya güiya disgusto.
56Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?"
57Lao si Jesus ilegña nu sija: Y profeta taya onraña, gui tanoña yan y guimaña; lao gaeonraña gui otro lugat.
57Basi, wakawa na mashaka naye. Lakini Yesu akawaambia, "Nabii hakosi kuheshimiwa, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani mwake!"
58Ya ti jafatinas güije megae na mannamanman, sa taya jinengguenñija.
58Kwa hiyo, hakutenda miujiza mingi pale kwa sababu ya kutoamini kwao.