1AYO na tiempo si Herodes y tetrarca jajungog y faman Jesus;
1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2Ya ilegña nu y tentagoña sija: Este si Juan Bautista: güiya cajulo gui entalo y manmatae, enao mina mandangculo na mannamanman jafatitinas guiya güiya.
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
3¶ Sa si Herodes esta jacone si Juan, ya jagode, ya japolo gui calaboso, pot si Herodias, asaguan Felipe y cheluña.
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4Sa si Juan ilegña nu güiya: Ti tunas na un guaja jao nu este na palaoan.
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
5Ya anae malago na upinino güe, maañao ni y linajyan taotao; sa pineloñija na si Juan profeta güe.
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6Ya anae mato y jaanin y mafañagon Herodes, y jagan Herodias bumaela gui talo, ya ninamagof si Herodes,
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7Ya pot este japromete ya manjula na uninae todo y guinagaoña.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8Ya güiya guinin umatungo finena an nanaña, ya ilegña: Naeyo güine gui un plato ni y ilon Juan Bautista.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
9Ayo nae y ray ninatriste; lao pot causa y juramentoña yan y mangachongña na mangaegue gui lamasa, manago na umanae.
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10Ya, manago na umautot y ilon Juan gui calaboso.
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11Ya machule guato y ilo gui un plato, ya manae y patgon palaoan, ya güiya chumule para si nanaña.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12Ya y disipuluña sija, manmato ya machule y tataotaoña, ya majafot, ya manmapos, ya masangane si Jesus.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13¶ Ya anae jajungog este si Jesus, mapos güije gui un batco para y desierto na lugat na sumajnge: ya anae majungog ni y linajyan taotao sija, madalalague güe, manmamocatja desde siuda sija.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14Ya jumanao si Jesus, ya jalie y dangculo na linajyan taotao: ya ninamaase ni ayo sija, ya janafanjomlo y manmalango sija.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15¶ Ya anae estaba pupnenge güije na jaane, manmato guiya güiya y disipuluña sija ya ilegñija; Este na lugat desierto ya y tiempo esta ufalofan; tago y linajyan taotao ya ufanjanao, ya ufanmalag y sengsong sija, ya ufanmamajan nañija.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
16Lao si Jesus ilegña nu sija: Taya nesesida na sija ufanjanao: jamyo innae nañija.
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
17Sija ilegñija nu güiya: Taya güine guaja na sincoja na pan, ya dos na güijan.
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
18Güiya ilegña: Chulieyofan güine mague.
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
19Ya jatago y linajyan taotao na ufanmatachong gui jilo chaguan, jachule y sinco na pan yan dos na güijan ya jaatan julo y langet, ya jabendise: ya jaipe y pan ya janae y disipulo sija, ya y disipulo janae y linajyan taotao.
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20Ya mañocho todos, ya manjaspog; ya anae majoca y sebblan pedaso sija na maipe, bula dose na canastra.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21Ya y mañocho sija, sinco mit na lalaje, ti matufong y famalaoan yan y famaguon.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22¶ Enseguidas si Jesus janafanjalom y disipuluña sija gui un batco, ya manjanao manmofona, manmalag y otro bandan sadog, y tiempo nae güiya janafanjanao y linajyan taotao.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23Ya anae munjayan jadespide y linajyan taotao, cajulo gui un ogso na sumajnge, ya manaetae. Ya estaba gui puenge, ya sumasaga güigüiyaja namaesa.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24Lao y batco pago estaba gui talo gui tase, pinapada ni napo, sa y manglo contra.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25Ya y mina cuatro na guatdia gui puenge, si Jesus jumanao para iyasija mamomocat gui jilo tase.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26Ya anae malie ni disipuluña sija na mamomocat gui jilo tase, ninafañatsaga, ya ilegñija: Fafañagüe este; ya managang ni y minaañaoñija.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
27Enseguidas si Jesus cumuentos, ilegña nu sija: Angoco jamyo; guajoyo; chamiyo fanmaaañao.
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
28Ayo nae manope si Pedro ilegña: Señot, yaguin jago, tago yo ya jufalag iyajago gui jilo janom.
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
29Güiya ilegña: Maela. Ya tumunog si Pedro gui batco, ya mamocat gui jilo janom para uguaguato gui as Jesus.
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30Lao anae jalie na dangculo na manglo, ninamaañao; ya anae jatutujon dimafondo, jaagang, ilegña: Señot, nalibreyo.
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
31Ya enseguidas si Jesus jajuto mona y canaeña, ya guiniut güe, ya ilegña nu güiya: Taotao na didide jinengguemo! Sa jafa ti unjonggue?
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
32Ya anae manjalom julo gui batco, y manglo quieto.
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33Ayo nae y mangaegue gui batco, maadora güe ilegñija: Magajet na jago Lajin Yuus.
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
34¶ Ya anae manmalofan gui tase, manmato gui tano Genesaret.
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35Ya y taotao ayo na lugat anae matungo güe, manmanago y oriyan todo ayo na tano, na umacone guato todo y manmalango.
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36Ya magagao güe na upolo na umapacha y madobbla y magaguña; ya todo y pumacha güe, guefjomlo sija.
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.