Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Matthew

17

1DESPUES di y saes na jaane, si Jesus jacone si Pedro, yan si Santiago, yan si Juan cheluña, ya jacone julo gui un taquilo na finabeca, na sumajnge.
1Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu.
2Ya jaaggo y jechuraña gui menanñija; ya y mataña manina calang y atdao; ya y magaguña apaca calang y manana.
2Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3Ya estagüe, na manmato güiya sija si Moises yan si Elias, na manguecuentos yan güiya.
3Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
4Ya manope si Pedro, ilegña as Jesus: Señot, mauleg na mangaeguejit güine: yaguin malagojao, bae jufatinas güine tres na tabetnaculo; para jago y uno, para si Moises y uno, yan para si Elias y uno.
4Hapo Petro akamwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
5Anae cumuecuentos güe, estagüe, un malag na mapagajes jananujong gui jiloñija, ya, estagüe, un inagang gui mapagajes na ilegña; Estagüiya y Lajijo na maguflie, na guefyajo: ecungog güe.
5Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni."
6Ya anae jajungog este y disipulo sija, manpodong gui jilo matañija ya mangosmaañao.
6Wanafunzi waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
7Ayo nae si Jesus mato ya manpinacha, ilegña: Fangajulo ya chamiyo fanmaaañao.
7Yesu akawaendea, akawagusa, akasema, "Simameni, msiogope!"
8Ya anae jajatsa y atadogñija, taya jalie na si Jesusja.
8Walipoinua macho yao hawakumwona mtu, ila Yesu peke yake.
9Ya anae manunog papa guine y finabeca, si Jesus mantinago ya ilegña: Chamiyo fanmañangangane ni jaye ni liniimiyo, asta qui y Lajin taotao esta cajulo gui entalo manmatae.
9Basi, walipokuwa wanashuka mlimani, Yesu akawaonya: "Msimwambie mtu mambo mliyoyaona mpaka Mwana wa Mtu atakapofufuliwa kutoka wafu."
10Ayo nae y disipuluña sija mafaesen güe ya ilegñija: Jafa nae na ilegñija y escriba sija na si Elias ufato finena?
10Kisha wanafunzi wakamwuliza, "Mbona walimu wa Sheria wanasema ati ni lazima kwanza Eliya aje?"
11Ya inepe as Jesus, ilegña: Magajet na si Elias ufato finena, ya ujananalo todo y güinaja.
11Yesu akawajibu, "Kweli, Eliya atakuja kutayarisha mambo yote.
12Lao guajo sumangane jamyo, na si Elias esta mato, ya ti matungogüe: lao mafatinas guiya güiya todo y malagoñija. Taegüenaoja locue y Lajin taotao upadese nu sija.
12Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja nao hawakumtambua, bali walimtendea jinsi walivyotaka. Mwana wa Mtu atateswa vivyo hivyo mikononi mwao."
13Ayo nae y disipulo sija jatungo na mansinangane sija as Juan Bautista.
13Hapo hao wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohane mbatizaji.
14¶ Ya anae manmato sija gui linajyan taotao, mato guiya güiya un taotao na dinimumuye güe ya ilegña:
14Walipojiunga tena na ule umati wa watu, mtu mmoja alimwendea Yesu, akampigia magoti,
15Señot, gaease ni lajijo; sa malango baba, ya gogosjapadese; sa megae nae podong gui guafe, yan megae nae podong gui janom.
15akasema, "Mheshimiwa, mwonee huruma mwanangu kwa kuwa ana kifafa, tena anateseka sana; mara nyingi yeye huanguka motoni na majini.
16Ya guinin juchulie guato y disipulumo, lao tisiña manajomio.
16Nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumponya."
17Ya manope si Jesus, ilegña: O generasion na ti manjonggue yan manchatpayon! asta ngaean nae utafanjijitaja? asta ngaean nae jususungonja jamyo? Chulie yo fan mague.
17Yesu akajibu, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia ninyi mpaka lini? Mleteni hapa huyo mtoto."
18Ya jalalatde si Jesus y anite, ya mapos gui malango, ya y patgon jomlo desde ayo na ora.
18Basi, Yesu akamkemea huyo pepo, naye akamtoka, na yule mtoto akapona wakati huohuo.
19Ayo nae manmato y disipulo sija gui as Jesus, ya ilegñija: Jafajam mina ti siña inyite juyong?
19Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha, wakamwuliza, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo?"
20Si Jesus ilegña nu sija: Pot diquique na jinengguenmiyo: sa magajet jusangane jamyo, na yanguin mangaejinenggue jamyo, calang y pepitas mostasa, injaalog ni este na jalom tano: Janao güine; ya ujanao, ya taya ti siña para jamyo.
20Yesu akawajibu, "Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, hata iwe ndogo kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: Toka hapa uende pale, nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu."
21(Lao este na classe ti jumanao juyong, yaguin ti y minauleg y tinayuyut.)
21"Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga."
22¶ Ya anae manmamocat guiya Galilea, ilegña si Jesus nu sija: Y Lajin taotao umaentrega gui canae y taotao sija;
22Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.
23Ya umapuno; lao y mina tres na jaane, ucajulo. Ya sija ninafangostriste.
23Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa." Wanafunzi wakahuzunika mno.
24¶ Ya anae manmato guiya Capernaum, manmato gui as Pedro ayosija y manmangongobbla y medio siclo, y tributo, ya ilegñija: Ada ti manapapase y maestronmiyo y medio siclo y tributo?
24Walipofika Kafarnaumu watu wenye kukusanya fedha ya zaka ya Hekalu walimwendea Petro, wakamwuliza, "Je, mwalimu wenu hulipa fedha ya zaka?"
25Güiya ilegña: Junggan. Ya anae jumalom güe gui jalom guma, si Jesus, cuenentuse güe antes, ilegña: Jafa jinasosomo Simon? Y ray y tano sija, jaye jacocobbla tributo pat senso? y famaguonñija, pat y taotaojuyong?
25Petro akajibu, "Naam, hulipa." Basi, Petro alipoingia ndani ya nyumba, kabla hata hajasema neno, Yesu akamwuliza, "Simoni, wewe unaonaje? Wafalme wa dunia hukusanya ushuru au kodi kutoka kwa kina nani? Kutoka kwa wananchi ama kutoka kwa wageni?"
26Ya anae ilegña, Y taotaojuyong; si Jesus ilegña nu güiya: Ayo nae y famaguon manlibre.
26Petro akajibu, "Kutoka kwa wageni." Yesu akamwambia, "Haya basi, wananchi hawahusiki.
27Lao para mungajit fumatinas y tinempo para sija, Janao falag y tase, ya unyute y jagüet, ya y finenana na güijan na mato, cone; ya an unbaba y pachotña, unsoda y un siclo; chule este ya nae para guajo yan para jago.
27Lakini kusudi tusiwakwaze, nenda ziwani ukatupe ndoana; chukua samaki wa kwanza atakayenaswa, fungua kinywa chake, na ndani utakuta fedha taslimu ya zaka. Ichukue ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako."