Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Matthew

18

1AYO na tiempo, manmato y disipulo sija gui as Jesus, ya ilegñija: Jaye mas dangculo gui raenon langet?
1Wakati ule wanafunzi walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Ni nani aliye mkuu katika Ufalme wa mbinguni?"
2Ya jaagang si Jesus un patgon, ya japolo gui entaloñija,
2Yesu akamwita mtoto mmoja, akamsimamisha kati yao,
3Ya ilegña: Magajet jusangane jamyo, yaguin ti inbira jamyo, ya ti infanjuyong calang, y diquique na famaguon, sen ti infanjalom gui raenon langet.
3kisha akasema, "Nawaambieni kweli, msipogeuka na kuwa kama watoto, hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni.
4Ya jayeja y umumitde calang este na patgon, este uguefdangculo gui raenon langet.
4Yeyote anayejinyenyekesha kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkubwa katika Ufalme wa mbinguni.
5Ya jayeja y rumesibe un patgon, parejo yan este, pot y naanjo, jaresibeja yo locue.
5Yeyote anayemkaribisha mtoto mmoja kama huyu kwa jina langu, ananikaribisha mimi.
6Lao jayeja y munamatompo uno güine gui estesija mandiquique ni y jumonggue yo, mas mauleg umagode gui agagaña y dangculo na molinon acho, ya umayute gui anae tadodong y tase.
6"Yeyote atakayemkosesha mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingekuwa afadhali afungwe shingoni jiwe kubwa la kusagia na kuzamishwa kwenye kilindi cha bahari.
7¶ Ayay y tano pot y tinempo sija! sa nesesita na ufato y tinempo sija, lao, ayay ayo na taotao, y uminafato y tinempo.
7Ole wake ulimwengu kwa sababu ya vikwazo vinavyowaangusha wengine. Vikwazo hivyo ni lazima vitokee lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.
8¶ Enao mina yaguin y canaemo, pat y adengmo, unninaquepodongjao, utut ya unnajanao guiya jago: sa maulegña na unqueyaojao, pat mangcojao, ya unjalom gui linâlâmo, qui uguaja dos canaemo, yan dos adengmo, ya unmapolo gui taejinecog na guafe.
8"Kama mkono au mguu wako ukikukosesha, ukate na kuutupa mbali nawe. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima bila mkono au mguu, kuliko kutupwa katika moto wa milele ukiwa na mikono miwili na miguu yako miwili.
9Yaguin y atadogmo unninaquepodongjao, chule ya unnajanao guiya jago; sa maulegña na unjalom gui linâlâmo yan un atadog, qui uguaja dos atadogmo, ya unmapolo gui guafen sasalaguan.
9Na kama jicho lako likikukosesha, ling'oe na kulitupa mbali nawe. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa chongo, kuliko kutupwa katika moto wa Jehanamu ukiwa na macho yako yote mawili.
10¶ Atan ya chamiyo dumesprenesia uno güine gui estesija y mandiquique; sa guajo sumangane jamyo, na y angjetñija gui langet, siesiempreja jaliliija y matan y Tatajo ni y gaegue gui langet.
10"Jihadharini! Msimdharau mmojawapo wa wadogo hawa. Nawaambieni, malaika wao huko mbinguni wako daima mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
11(Sa y Lajin taotao mato para usatba y manmalingo.)
11Maana Mwana wa Mtu alikuja kuwaokoa wale waliopotea.
12Jafa jinasonmimiyo? Yaguin guaja un taotao na gaega siento na quinilo, ya finalingaeguan uno: Ada ti upolo y noventa y nueve gui jalomtano, ya ujanao ya ujaligao ayo y malingo?
12Mnaonaje? Mtu akiwa na kondoo mia, akimpoteza mmoja, hufanyaje? Huwaacha wale tisini na tisa mlimani, na huenda kumtafuta yule aliyepotea.
13Yanguin jasoda, magajet jusangane jamyo, na magofña ni ayo, qui y noventa y nueve ni y ti manmalingo.
13Akimpata, nawaambieni kweli, humfurahia huyo kuliko awafurahiavyo wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
14Taegüineja, ti minalago Tatanmiyo ni y gaegue gui langet, na uguaja malingo uno güine gui estesija y mandiquique.
14Hali kadhalika, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmoja wa hawa wadogo apotee.
15¶ Yaguin y chelumo inisagüejao, janao, ya unsangane ni y linachiña, jamyoja na dos; yanguin inecungogjao, ungana y chelumo.
15"Ndugu yako akikukosea, mwendee ukamwonye mkiwa ninyi peke yenu. Akikusikia utakuwa umempata ndugu yako.
16Lao, yaguin ti jaecungogjao, fangone gachongmo uno, pat dos, sa para y pachot dos pat tres na testigo, ucabales todo y sinangan.
16Asipokusikia, chukua mtu mmoja au wawili pamoja nawe, ili kwa mawaidha ya mashahidi wawili au watatu, kila tatizo litatuliwe.
17Yanguin ti jaecungog sija, sangane y inetnon mangilisyano; lao yaguin ti malago jaecungog y inetnon mangilisyano, güiya para jago parejo yan un taotaojuyong pat publicano.
17Asipowasikia hao, liambie kanisa. Na kama hatalisikia kanisa, na awe kwako kama watu wasiomjua Mungu na watoza ushuru.
18Magajet jusangane jamyo, na todo y inguede gui tano, ufanmagode locue gui langet: ya todo y inpila gui tano, ufanmapula locue gui langet.
18"Nawaambieni kweli, mtakachofunga duniani kitafungwa mbinguni, na mtakachofungua duniani kitafunguliwa mbinguni.
19Jusangane jamyo talo, na yaguin dos guiya jamyo inguaja un corason gui jilo tano, pot jafa na güinaja ni ingagao; umafatinas para sija, pot y Tatajo na gaegue gui langet.
19Tena nawaambieni, wawili miongoni mwenu wakikubaliana hapa duniani kuhusu jambo lolote la kuomba, Baba yangu wa mbinguni atawafanyia jambo hilo.
20Sa manoja nae guaja dos pat tres, na mandadaña pot y naanjo, gaegue yo güije gui entaloñija.
20Kwa maana popote pale wanapokusanyika wawili au watatu kwa jina langu, mimi nipo hapo kati yao."
21¶ Ayo nae si Pedro mato guiya güiya ya ilegña: Señot, cuanto biaje juasie y chelujo yaguin jaisagüeyo? asta siete biaje?
21Kisha Petro akamwendea Yesu, akamwuliza, "Je, ndugu yangu akinikosea, nimsamehe mara ngapi? Mara saba?"
22Si Jesus ilegña nu güiya: Ti jualog sieteja na biaje, lao, asta setenta na siete.
22Yesu akamjibu, "Sisemi mara saba tu, bali sabini mara saba.
23¶ Enao mina y raenon langet, parejoja yan un ray, na malago na ufatinas cuentas yan y tentagoña sija.
23Ndiyo maana Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyeamua kukagua hesabu za watumishi wake.
24Ya anae jatutujon fumatinas y cuentas sija, maconiegüe guato, uno na mandidibe dies mit talento.
24Ukaguzi ulipoanza, akaletewa mtu mmoja aliyekuwa na deni la fedha talanta elfu kumi.
25Lao anae güiya ti siña jaapase, y amuña manago na umabende güe, yan y asaguaña, yan y famaguonña, yan todo y güinajaña, ya umaapasegüe.
25Mtu huyo hakuwa na chochote cha kulipa; hivyo bwana wake aliamuru wauzwe, yeye, mke wake, watoto wake na vitu vyote alivyokuwa navyo, ili deni lilipwe.
26Ayo na tentago, dumimo papa ya tinayuyutgüe, ilegña: Señot, gaesiningon nu guajo, ya juapasejao todo.
26Basi, huyo mtumishi akapiga magoti mbele yake, akasema, Unisubiri nami nitakulipa deni lote.
27Y amon ayo na tentago, ninagosmaase, ya pinelogüe, ya inasie ni y dibiña.
27Yule bwana alimwonea huruma, akamsamehe lile deni, akamwacha aende zake.
28Ya jumanao ayo na tentago, ya umasoda yan uno gui mangachongña na dinidibegüe cien pesetas; ya jamantiene güe ya jañucut, ya ilegña: Apaseyo todo ni dibimo.
28"Lakini huyo mtumishi akaondoka, akamkuta mmoja wa watumishi wenzake aliyekuwa na deni lake fedha denari mia moja. Akamkamata, akamkaba koo akisema, Lipa deni lako!
29Ayo nae y gachongña dumimo papa, ya tinayuyutgüe ilegña: Gaesiningon nu guajo, ya juapasejao.
29Huyo mtumishi mwenzake akapiga magoti, akamwomba, Unisubiri nami nitalipa deni langu lote.
30Lao güiya ti malago, ya mapos ya pinelo gui catset asta qui uinapase ni y dibiña.
30Lakini yeye hakutaka, bali alimtia gerezani mpaka hapo atakapolipa lile deni.
31Ya anae malie ni y mangachongña, jafa y susede, ninafangostriste, ya manmato, ya masangane y amuñija y susede.
31"Basi, watumishi wenzake walipoona jambo hilo walisikitika sana, wakaenda kumpasha habari bwana wao juu ya mambo hayo yaliyotukia.
32Ayo nae y amuña inagang güe, ya ilegña: Taelayejao na tentago. Juasiijao todo ni y dibimo, sa untayuyutyo:
32Hapo yule bwana alimwita huyo mtumishi, akamwambia, Wewe ni mtumishi mbaya sana! Uliniomba, nami nikakusamehe deni lako lote.
33Ada locue ti ninamaase jao ni y gachongmo, calang y maasejo nu jago?
33Je, haikukupasa nawe kumhurumia mtumishi mwenzako kama nilivyokuhurumia?
34Ayo nae y amuña ninalalalo, ya inentrega güe gui mansasapet, asta qui uapase todo y dinidibegüe.
34"Basi, huyo bwana alikasirika sana, akamtoa huyo mtumishi aadhibiwe mpaka hapo atakapolipa deni lote.
35Taegüenaoja locue ufatinas nu jamyo y Tatajo ni gaegue gui langet, yaguin ti inasie gui corasonmiyo cada uno gui chelonmiyo nu y dibiña.
35Na baba yangu aliye mbinguni atawafanyieni vivyo hivyo kama kila mmoja wenu hatamsamehe ndugu yake kwa moyo wake wote."