1CHAMIYO fanmanjusga para ti infanmajusga.
1"Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu;
2Sa taemanoja yan manmajusga yan manmañogne jamyo, taegüijija locue infanmajusga; ya taemanoja y minedidamiyo, taegüijija locue infanmamediye.
2kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.
3Sa jafa muna unlilie y migo gui atadog y chelumo, ya ti unjajaso y jayo gui atadogmo?
3Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako?
4Jafa taemano unalog nu y chelumo: Maela ya junajanao enao y migo gui atadogmo; ya enagüija y jayo gui atadogmo?
4Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako, wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?
5Hipocrita! Najanao finenana y jayo gui atadogmo? ya ayo nae siña ungueflie yan para unnajanao y migo gui atadog y chelumo.
5Mnafiki wewe! Ondoa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako na hapo ndipo utaona waziwazi kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilichoko jichoni mwa ndugu yako.
6¶ Chamiyo numanae y galago nu y santos, ni inpelo y perlasmiyo gui menan y babue; sa no seaja ujagacha nu y patasñija ya ujabira sija ya infanyenabalag jamyo.
6"Msiwape mbwa vitu vitakatifu wasije wakageuka na kuwararua ninyi; wala msiwatupie nguruwe lulu zenu wasije wakazikanyaga.
7¶ Gagao ya infanmanae; aligao ya inseda; yajo ya infanmababaye.
7"Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni, nanyi mtafunguliwa.
8Sa jayeja y mangagao, uresibe; ya y manaligao, usoda; ya y manyajo, umababaye.
8Maana, aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye hufunguliwa.
9Ya jayeja guiya jamyo, yaguin uguinagao nu y lajiña pan, ada unnae acho?
9Je, kuna yeyote miongoni mwenu ambaye mtoto wake akimwomba mkate, atampa jiwe?
10Pat yaguin uguinagao un güijan, ada unnae un serpiente?
10Au je, akimwomba samaki, atampa nyoka?
11Ombre manaelaye jamyo, intingo numae mauleg na ninae y famaguonmiyo; ada ti mas y tatanmiyo, ni y gaegue gui langet, unnae mauleg na güinaja todo ayo y gumagaogüe?
11Kama basi ninyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: atawapa mema wale wanaomwomba.
12Enao mina, jaftaemano y malagomiyo na y taotao ufatitinas nu jamyo, taegüijija infatitinas locue nu sija; sa este y lay yan y profeta sija.
12"Watendeeni wengine yale mnayotaka wao wawatendee ninyi. Hii ndiyo maana ya Sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.
13¶ Jalom gui maiot na potta, sa y feda na potta ya micanpo y chalan nu y jumananaogüe y finalingo, ya megae sija y fumapoposgüe.
13"Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.
14Sa y maiot na potta ya dalalae na chalan y jumananaogüe y linâlâ, ya didide sija y sumosoda.
14Lakini njia inayoongoza kwenye uzima ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.
15¶ Adaje jamyo nu y ti manmagajet na profeta, ni ufanmato guiya jamyo maninagagon quininilo, lao y sanjalomñija mangaegue lobo na mañaque.
15"Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali.
16Injatingo pot y tinegchañija. Ada y taotao ufañule ubas guine y títucan jayo, pat igos guine y títucan chaguan?
16Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!
17Taegüijija todo y mauleg na trongcon jayo, siempre mauleg tinegchaña; lao y taelaye na trongcon jayo, siempre taelaye tinegchaña.
17Basi, mti mwema huzaa matunda mema, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
18Ti siña y mauleg na trongcon jayo manogcha taelaye; ni y taelaye na trongcon jayo manogcha mauleg.
18Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mema.
19Todo y trongcon jayo ni ti manogcha mauleg, umautut ya umayute gui guafe,
19Kila mti usiozaa matunda mema utakatwa na kutupwa motoni.
20Enao mina pot y tinegchañija, injatingo.
20Kwa hiyo, mtawatambua kwa matendo yao.
21¶ Ti todo y umalog nu guajo: Señot! Señot! ujalom gui raenon langet; lao ayo y fumatinas y minalago y tatajo, ni y gaegue gui langet.
21"Si kila aniambiaye, Bwana, Bwana, ataingia katika Ufalme wa mbinguni; ila ni yule tu anayetimiza mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22Megae, güije na jaane, ualog nu guajo: Señot! Señot! ada ti inprofetisa pot y naanmo, yan innajanao y anite pot y naanmo, yan infatinas megae námanman na chocho pot y naanmo?
22Wengi wataniambia Siku ile ya hukumu: Bwana, Bwana! kwa jina lako tulitangaza ujumbe wako, na kwa jina lako tuliwatoa pepo na kufanya miujiza mingi.
23Ya ayo nae jusangane sija, ni y magajet ti jutungo jamyo, fanjanao guiya guajo, jamyo manmamatitinas inechong.
23Hapo nitawaambia: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni mbele yangu, enyi watenda maovu.
24¶ Enao mina jayeja y jumungog este sija y sinanganjo ya fumatinas, güiya parejo yan y méjnalom na taotao, na jafatinas y guimaña gui jilo acho;
24"Kwa sababu hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
25Ya utunog y ichan, yan ufanmato y sadog, yan ufanmanguaefe y manglo, ya ubinate ayo na guma ya ti upodong, sa mafatinas gui jilo acho.
25Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo. Lakini haikuanguka kwa sababu ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.
26Lao jayeja y jumungog este sija y sinanganjo, ya ti fumatinas, güiya parejo yan y bábaba na taotao na jafatinas y guimaña gui jilo unae;
26"Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
27Ya utunog y ichan yan ufanmato y sadog, yan ufanmanguaefe y manglo ya ubinate ayo na guma, ya upodong; ya gosdangculo y pinedongña.
27Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo, nayo ikaanguka; tena kwa kishindo kikubwa."
28Ya susede, anae munjayan este sija jasangan si Jesus, ninafanmanman y linajyan taotao sija nu y doctrinaña.
28Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati wa watu ukashangazwa na mafundisho yake.
29Sa jafanagüe sija, calang uno ni gaeninasiña, lao ti calang y escriba sija.
29Hakuwa kama walimu wao wa Sheria, bali alifundisha kwa mamlaka.