1Nasljedovatelji moji budite, kao što sam i ja Kristov.
1Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
2Hvalim vas što me se u svemu sjećate i držite se predaja kako vam predadoh.
2Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
3Ali htio bih da znate: svakomu je mužu glava Krist, glava ženi muž, a glava Kristu Bog.
3Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
4Svaki muž koji se moli ili prorokuje pokrivene glave sramoti glavu svoju.
4Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
5Svaka pak žena koja se moli ili prorokuje gologlava sramoti glavu svoju. Ta to je isto kao da je obrijana.
5Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
6Jer ako se žena ne pokriva, neka se šiša; ako li je pak ružno ženi šišati se ili brijati, neka se pokrije.
6Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
7A muž ne mora pokrivati glave, ta slika je i slava Božja; a žena je slava muževa.
7Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
8Jer nije muž od žene, nego žena od muža.
8Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
9I nije stvoren muž radi žene, nego žena radi muža.
9Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
10Zato žena treba da ima "vlast" na glavi poradi anđela.
10Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
11Ipak, u Gospodinu - ni žena bez muža, ni muž bez žene!
11Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
12Jer kao što je žena od muža, tako je i muž po ženi; a sve je od Boga.
12Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
13Sami sudite dolikuje li da se žena gologlava Bogu moli?
13Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
14Ne uči li nas i sama narav da je mužu sramota ako goji kosu?
14Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
15A ženi je dika ako je goji jer kosa joj je dana mjesto prijevjesa.
15lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
16Ako je kome do prepirke, takva običaja mi nemamo, a ni Crkve Božje.
16Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
17Kad već dajem ta upozorenja, ne mogu pohvaliti što se ne sastajete na bolje, nego na gore.
17Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
18Ponajprije čujem, djelomično i vjerujem: kad se okupite na Sastanak, da su među vama razdori.
18Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
19Treba doista da i podjela bude među vama da se očituju prokušani među vama.
19maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
20Kad se dakle tako zajedno sastajete, to nije blagovanje Gospodnje večere:
20Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
21ta svatko se pri blagovanju prihvati svoje večere te jedan gladuje, a drugi se opija.
21Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
22Zar nemate kuća da jedete i pijete? Ili Crkvu Božju prezirete i postiđujete one koji nemaju? Što da vam kažem? Da vas pohvalim? U tom vas ne hvalim.
22Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
23Doista, ja od Gospodina primih što vama predadoh: Gospodin Isus one noći kad bijaše predan uze kruh,
23Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
24zahvalivši razlomi i reče: "Ovo je tijelo moje - za vas. Ovo činite meni na spomen."
24akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: "Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
25Tako i čašu po večeri govoreći: "Ova čaša novi je Savez u mojoj krvi. Ovo činite kad god pijete, meni na spomen."
25Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: "Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka."
26Doista, kad god jedete ovaj kruh i pijete čašu, smrt Gospodnju navješćujete dok on ne dođe.
26Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
27Stoga, tko god jede kruh ili pije čašu Gospodnju nedostojno, bit će krivac tijela i krvi Gospodnje.
27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
28Neka se dakle svatko ispita pa tada od kruha jede i iz čaše pije.
28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
29Jer tko jede i pije, sud sebi jede i pije ako ne razlikuje Tijela.
29maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
30Zato su među vama mnogi nejaki i nemoćni, i spavaju mnogi.
30Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
31Jer kad bismo sami sebe sudili, ne bismo bili suđeni.
31Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
32A kad nas sudi Gospodin, odgaja nas da ne budemo sa svijetom osuđeni.
32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33Zato, braćo moja, kad se sastajete na blagovanje, pričekajte jedni druge.
33Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
34Je li tko gladan, kod kuće neka jede da se ne sastajete na osudu. Drugo ću urediti kada dođem.
34Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.