1O darima Duha ne bih, braćo, htio da budete u neznanju.
1Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2Znate kako ste se dok bijaste pogani, zavedeni, zanosili nijemim idolima.
2Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3Zato vam obznanjujem: nitko tko u Duhu Božjem govori ne kaže: "Prokletstvo Isusu". I nitko ne može reći: "Gospodin Isus" osim u Duhu Svetom.
3Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4Različiti su dari, a isti Duh;
4Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
5i različite službe, a isti Gospodin;
5Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
6i različita djelovanja, a isti Bog koji čini sve u svima.
6Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
7A svakomu se daje očitovanje Duha na korist.
7Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
8Doista, jednomu se po Duhu daje riječ mudrosti, drugomu riječ spoznanja po tom istom Duhu;
8Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
9drugomu vjera u tom istom Duhu, drugomu dari liječenja u tom jednom Duhu;
9Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
10drugomu čudotvorstva, drugomu prorokovanje, drugomu razlučivanje duhova, drugomu različiti jezici, drugomu tumačenje jezika.
10humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
11A sve to djeluje jedan te isti Duh dijeleći svakomu napose kako hoće.
11Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
12Doista, kao što je tijelo jedno te ima mnogo udova, a svi udovi tijela iako mnogi, jedno su tijelo - tako i Krist.
12Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
13Ta u jednom Duhu svi smo u jedno tijelo kršteni, bilo Židovi, bilo Grci, bilo robovi, bilo slobodni. I svi smo jednim Duhom napojeni.
13Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
14Ta ni tijelo nije jedan ud, nego mnogi.
14Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
15Rekne li noga: "Nisam ruka, nisam od tijela", zar zbog toga nije od tijela?
15Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
16I rekne li uho: "Nisam oko, nisam od tijela", zar zbog toga nije od tijela?
16Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
17Kad bi sve tijelo bilo oko, gdje bi bio sluh? Kad bi sve bilo sluh, gdje bi bio njuh?
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
18A ovako, Bog je rasporedio udove, svaki od njih u tijelu, kako je htio.
18Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
19Kad bi svi bili jedan ud, gdje bio bilo tijelo?
19Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20A ovako, mnogi udovi - jedno tijelo!
20Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
21Ne može oko reći ruci: "Ne trebam te", ili pak glava nogama: "Ne trebam vas."
21Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."
22Naprotiv, mnogo su potrebniji udovi tijela koji izgledaju slabiji.
22Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
23A udove koje smatramo nečasnijima, okružujemo većom čašću. I s nepristojnima se pristojnije postupa,
23Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
24a pristojni toga ne trebaju. Nego, Bog je tako sastavio tijelo da je posljednjem udu dao izobilniju čast
24ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
25da ne bude razdora u tijelu, nego da se udovi jednako brinu jedni za druge.
25ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
26I ako trpi jedan ud, trpe zajedno svi udovi; ako li se slavi jedan ud, raduju se zajedno svi udovi.
26Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
27A vi ste tijelo Kristovo i, pojedinačno, udovi.
27Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
28I neke postavi Bog u Crkvi: prvo za apostole, drugo za proroke, treće za učitelje; onda čudesa, onda dari liječenja; zbrinjavanja, upravljanja, razni jezici.
28Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
29Zar su svi apostoli? Zar svi proroci? Zar svi učitelji? Zar svi čudotvorci?
29Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
30Zar svi imaju dare liječenja? Zar svi govore jezike? Zar svi tumače?
30Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
31Čeznite za višim darima! A evo vam puta najizvrsnijega!
31Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.