Croatian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

15

1Dozivljem vam, braćo, u pamet evanđelje koje vam navijestih, koje primiste, u kome stojite,
1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2po kojem se spasavate, ako držite što sam vam navijestio; osim ako uzalud povjerovaste.
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3Doista, predadoh vam ponajprije što i primih: Krist umrije za grijehe naše po Pismima;
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4bi pokopan i uskrišen treći dan po Pismima;
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5ukaza se Kefi, zatim dvanaestorici.
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6Potom se ukaza braći, kojih bijaše više od pet stotina zajedno; većina ih još i sada živi, a neki usnuše.
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7Zatim se ukaza Jakovu, onda svim apostolima.
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8Najposlije, kao nedonoščetu, ukaza se i meni.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9Da, ja sam najmanji među apostolima i nisam dostojan zvati se apostolom jer sam progonio Crkvu Božju.
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10Ali milošću Božjom jesam što jesam i njegova milost prema meni ne bijaše zaludna; štoviše, trudio sam se više nego svi oni - ali ne ja, nego milost Božja sa mnom.
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11Ili dakle ja ili oni: tako propovijedamo, tako vjerujete.
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12No ako se propovijeda da je Krist od mrtvih uskrsnuo, kako neki među vama govore da nema uskrsnuća mrtvih?
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13Ako nema uskrsnuća mrtvih, ni Krist nije uskrsnuo.
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14Ako pak Krist nije uskrsnuo, uzalud je doista propovijedanje naše, uzalud i vjera vaša.
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15Zatekli bismo se i kao lažni svjedoci Božji što posvjedočismo protiv Boga: da je uskrisio Krista, kojega nije uskrisio, ako doista mrtvi ne uskršavaju.
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16Jer ako mrtvi ne uskršavaju, ni Krist nije uskrsnuo.
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17A ako Krist nije uskrsnuo, uzaludna je vjera vaša, još ste u grijesima.
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18Onda i oni koji usnuše u Kristu, propadoše.
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19Ako se samo u ovom životu u Krista ufamo, najbjedniji smo od svih ljudi.
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20Ali sada: Krist uskrsnu od mrtvih, prvina usnulih!
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21Doista po čovjeku smrt, po Čovjeku i uskrsnuće od mrtvih!
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22Jer kao što u Adamu svi umiru, tako će i u Kristu svi biti oživljeni.
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23Ali svatko u svom redu: prvina Krist, a zatim koji su Kristovi, o njegovu Dolasku;
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24potom - svršetak, kad preda kraljevstvo Bogu i Ocu, pošto obeskrijepi svako Vrhovništvo, svaku Vlast i Silu.
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25Doista, on treba da kraljuje dok ne podloži sve neprijatelje pod noge svoje.
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26Kao posljednji neprijatelj bit će obeskrijepljena Smrt
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27jer sve podloži nogama njegovim. A kad veli: Sve je podloženo, jasno - sve osim Onoga koji mu je sve podložio.
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28I kad mu sve bude podloženo, tada će se i on sam, Sin, podložiti Onomu koji je njemu sve podložio da Bog bude sve u svemu.
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29Što onda čine oni koji se krste za mrtve? Ako mrtvi uopće ne uskršavaju, što se krste za njih?
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30Što se onda i mi svaki čas izlažemo pogiblima?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31Dan za danom umirem, tako mi slave vaše, braćo, koju imam u Kristu Isusu, Gospodinu našem!
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32Ako sam se po ljudsku borio sa zvijerima u Efezu, kakva mi korist? Ako mrtvi ne uskršavaju, jedimo i pijmo jer sutra nam je umrijeti.
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
33Ne varajte se: "Zli razgovori kvare dobre običaje."
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34Otrijeznite se kako valja i ne griješite jer neki, na sramotu vam kažem, ne znaju za Boga.
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35Ali reći će netko: Kako uskršavaju mrtvi? I s kakvim li će tijelom doći?
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
36Bezumniče! Što siješ, ne oživljuje ako ne umre.
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37I što siješ, ne siješ tijelo buduće, već golo zrno, pšenice - recimo - ili čega drugoga.
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38A Bog mu daje tijelo kakvo hoće, i to svakom sjemenu svoje tijelo.
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39Nije svako tijelo isto tijelo; drugo je tijelo čovječje, drugo tijelo stoke, drugo tijelo ptičje, a drugo riblje.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40Ima tjelesa nebeskih i tjelesa zemaljskih, ali drugi je sjaj nebeskih, a drugi zemaljskih.
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41Drugi je sjaj sunca, drugi sjaj mjeseca i drugi sjaj zvijezda; jer zvijezda se od zvijezde razlikuje u sjaju.
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42Tako i uskrsnuće mrtvih: sije se u raspadljivosti, uskršava u neraspadljivosti;
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43sije se u sramoti, uskršava u slavi; sije se u slabosti, uskršava u snazi;
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44sije se tijelo naravno, uskršava tijelo duhovno. Ako ima tijelo naravno, ima i duhovno.
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45Tako je i pisano: Prvi čovjek, Adam, postade živa duša, posljednji Adam - duh životvorni.
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46Ali ne bi najprije duhovno, nego naravno pa onda duhovno.
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47Prvi je čovjek od zemlje, zemljan; drugi čovjek - s neba.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48Kakav je zemljani takvi su i zemljani, a kakav je nebeski takvi su i nebeski.
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49I kao što smo nosili sliku zemljanoga, nosit ćemo i sliku nebeskoga.
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50A ovo, braćo, tvrdim: tijelo i krv ne mogu baštiniti kraljevstva Božjega i raspadljivost ne baštini neraspadljivosti.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51Evo otajstvo vam kazujem: svi doduše nećemo usnuti, ali svi ćemo se izmijeniti.
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52Odjednom, u tren oka, na posljednju trublju - jer zatrubit će - i mrtvi će uskrsnuti neraspadljivi i mi ćemo se izmijeniti.
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53Jer ovo raspadljivo treba da se obuče u neraspadljivost i ovo smrtno da se obuče u besmrtnost.
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54A kad se ovo raspadljivo obuče u neraspadljivost i ovo smrtno obuče u besmrtnost, tada će se obistiniti riječ napisana: Pobjeda iskapi smrt.
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
55Gdje je, smrti, pobjeda tvoja? Gdje je, smrti, žalac tvoj?
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
56Žalac je smrti grijeh, snaga je grijeha Zakon.
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57A hvala Bogu koji nam daje pobjedu po Gospodinu našem Isusu Kristu!
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58Tako, braćo moja ljubljena, budite postojani, nepokolebljivi, i obilujte svagda u djelu Gospodnjem znajući da trud vaš nije neplodan u Gospodinu.
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.