1Tko bi se od vas u sporu s drugim usudio parničiti se pred nepravednima, a ne pred svetima?
1Anathubutuje mmoja wenu kumshtaki ndugu muumini mbele ya mahakama ya watu wasiomjua Mungu badala ya kumshtaki mbele ya watu wa Mungu?
2Ili zar ne znate da će sveti suditi svijet? Pa ako ćete vi suditi svijet, zar niste vrijedni suditi sitnice?
2Je, hamjui kwamba watu wa Mungu watauhukumu ulimwengu? Ikiwa basi, ulimwengu utahukumiwa nanyi, kwa nini hamstahili kuhukumu hata katika mambo madogo?
3Ne znate li da ćemo suditi anđele, kamo li ne ono svagdanje?
3Je, hamjui kwamba, licha ya kuhukumu mambo ya kawaida ya kila siku, tutawahukumu hata malaika?
4A vi, kad imate sporove o svagdanjem, sucima postavljate one do kojih Crkva ništa ne drži!
4Mnapokuwa na mizozo juu ya mambo ya kawaida, je, mnawaita wawe mahakimu watu ambao hata hawalijali kanisa?
5Vama na sramotu govorim. Tako? Zar nema među vama ni jednoga mudra koji bi mogao rasuditi među braćom?
5Aibu kwenu! Ndiyo kusema hakuna hata mmoja miongoni mwenu mwenye hekima kiasi cha kuweza kutatua tatizo kati ya ndugu waumini?
6Nego brat se s bratom parniči, i to pred nevjernicima?
6Badala yake, kweli imekuwa mtindo ndugu kumpeleka ndugu yake mahakamani, tena mbele ya mahakimu wasioamini.
7Zapravo, već vam je to nedostatak što se parničite među sobom. Zašto radije ne trpite nepravdu? Zašto se radije ne pustite oplijeniti?
7Kwa kweli huko kushtakiana tu wenyewe kwa wenyewe kwabainisha kwamba mmeshindwa kabisa! Je, haingekuwa jambo bora zaidi kwenu kudhulumiwa! Haingekuwa bora zaidi kwenu kunyang'anywa mali yenu?
8Nego vi činite nepravdu i plijenite, i to braću.
8Lakini, badala yake, ninyi ndio mnaodhulumu na kunyang'anya; tena, hayo mnawafanyia ndugu zenu!
9Ili zar ne znate da nepravednici neće baštiniti kraljevstva Božjega? Ne varajte se! Ni bludnici, ni idolopoklonici, ni preljubnici, ni mekoputnici, ni muškoložnici,
9Au je, hamjui kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msijidanganye! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti,
10ni kradljivci, ni lakomci, ni pijanice, ni psovači, ni razbojnici neće baštiniti kraljevstva Božjega.
10wevi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang'anyi, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu.
11To evo, bijahu neki od vas, ali oprali ste se, ali posvetili ste se, ali opravdali ste se u imenu Gospodina našega Isusa Krista i u Duhu Boga našega.
11Baadhi yenu mlikuwa hivyo; lakini sasa mmeoshwa, mkafanywa watakatifu, na kupatanishwa na Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.
12"Sve mi je dopušteno!" Ali - sve ne koristi. "Sve mi je dopušteno!" Ali - neću da mnome išta vlada.
12Mtu anaweza kusema: "Kwangu mimi kila kitu ni halali." Sawa; lakini si kila kitu kinafaa. Nakubali kwamba kila kitu ni halali kwangu lakini sitaki kutawaliwa na kitu chochote.
13"Jela trbuhu, a trbuh jelima; Bog će i jedno i drugo uništiti." Ali ne tijelo bludnosti, nego Gospodinu, i Gospodin tijelu!
13Unaweza kusema: "Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula." Sawa; lakini Mungu ataviharibu vyote viwili. Mwili wa mtu si kwa ajili ya uzinzi bali ni kwa ajili ya kumtumikia Bwana, naye Bwana ni kwa ajili ya mwili.
14Ta Bog koji je Gospodina uskrisio i nas će uskrisiti snagom njegovom.
14Basi, Mungu aliyemfufua Bwana kutoka wafu atatufufua nasi pia kwa nguvu yake.
15Ne znate li da su tijela vaša udovi Kristovi? Hoću li dakle uzeti udove Kristove i učiniti ih udovima bludničinim? Nipošto!
15Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya mwili wa Kristo? Je, mnadhani naweza kuchukua sehemu ya mwili wa Kristo na kuifanya kuwa sehemu ya mwili wa kahaba? Hata kidogo!
16Ili zar ne znate: tko uz bludnicu prione, jedno je tijelo? Jer veli se: Bit će njih dvoje jedno tijelo.
16Maana, kama mjuavyo, anayeungana na kahaba huwa mwili mmoja naye--kama ilivyoandikwa: "Nao wawili watakuwa mwili mmoja."
17A tko prione uz Gospodina, jedan je duh.
17Lakini aliyejiunga na Bwana huwa roho moja naye.
18Bježite od bludnosti! Svaki grijeh koji učini čovjek, izvan tijela je, a bludnik griješi protiv svojega tijela.
18Jiepusheni kabisa na uzinzi. Dhambi nyingine zote hutendwa nje ya mwili lakini mzinzi hutenda dhambi dhidi ya mwili wake mwenyewe.
19Ili zar ne znate? Tijelo vaše hram je Duha Svetoga koji je u vama, koga imate od Boga, te niste svoji.
19Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, ambaye mlimpokea kutoka kwa Mungu? Ninyi basi, si mali yenu wenyewe.
20Jer kupljeni ste otkupninom. Proslavite dakle Boga u tijelu svojem!
20Mlinunuliwa kwa bei kubwa. Kwa hiyo, itumieni miili yenu kwa ajili ya kumtukuza Mungu.