1Petar, apostol Isusa Krista: putnicima Raseljeništva u Pontu, Galaciji, Kapadociji, Aziji i Bitiniji,
1Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
2po predznanju Boga Oca, posvećenjem Duha izabranima da budu poslušni te poškropljeni krvlju Isusa Krista. Punina vam milosti i mira!
2Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
3Blagoslovljen Bog i Otac Gospodina našega Isusa Krista koji nas po velikom milosrđu svojemu uskrsnućem Isusa Krista od mrtvih nanovo rodi za životnu nadu,
3Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
4za baštinu neraspadljivu, neokaljanu i neuvelu, pohranjenu na nebesima za vas,
4na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
5vas koje snaga Božja po vjeri čuva za spasenje, spremno da se objavi u posljednje vrijeme.
5Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
6Zbog toga se radujte, makar se sada možda trebalo malo i žalostiti zbog različitih kušnja:
6Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
7da prokušanost vaše vjere - dragocjenija od propadljivog zlata, koje se ipak u vatri kuša - stekne hvalu, slavu i čast o Objavljenju Isusa Krista.
7Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
8Njega vi ljubite iako ga ne vidjeste; u njega, iako ga još ne gledate, vjerujete te klikćete od radosti neizrecive i proslavljene
8Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
9što postigoste svrhu svoje vjere: spasenje duša.
9kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
10To su spasenje istraživali i pronicali proroci koji prorokovahu o milosti vama namijenjenoj.
10Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
11Pronicali su na koje ili kakvo je vrijeme smjerao Duh Kristov u njima koji je unaprijed svjedočio o Kristovim patnjama te slavama što su nakon njih imale doći:
11Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
12bi im objavljeno da ne sebi nego vama poslužuju ono što vam sada u Duhu Svetom s neba poslanom navijestiše vaši blagovjesnici, a nada što se i anđeli žude nadviti.
12Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
13Zato opašite bokove pameti svoje, trijezni budite i savršeno se pouzdajte u milost koju vam donosi Objavljenje Isusa Krista.
13Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
14Kao poslušna djeca ne supriličujte se prijašnjim požudama iz doba neznanja.
14Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
15Naprotiv, kao što je svet Onaj koji vas pozva, i vi budite sveti u svemu življenju.
15Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
16Ta pisano je: Budite sveti jer sam ja svet.
16Maandiko yasema: "Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu."
17Ako dakle Ocem nazivate njega koji nepristrano svakoga po djelu sudi, vrijeme svoga proputovanja proživite u bogobojaznosti.
17Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
18Ta znate da od svog ispraznog načina života, što vam ga oci namriješe, niste otkupljeni nečim raspadljivim, srebrom ili zlatom,
18Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
19nego dragocjenom krvlju Krista, Jaganjca nevina i bez mane.
19bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
20On bijaše doduše predviđen prije postanka svijeta, ali se očitova na kraju vremena radi vas
20Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
21koji po njemu vjerujete u Boga koji ga uskrisi od mrtvih te mu dade slavu da vjera vaša i nada bude u Bogu.
21Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
22Pošto ste posluhom istini očistili duše svoje za nehinjeno bratoljublje, od srca žarko ljubite jedni druge.
22Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
23Ta nanovo ste rođeni, ne iz sjemena raspadljiva nego neraspadljiva: riječju Boga koji živi i ostaje.
23Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele.
24Doista, svako je tijelo kao trava, sva mu slava ko cvijet poljski: sahne trava, vene cvijet,
24Kama Maandiko yasemavyo: "Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
25ali Riječ Gospodnja ostaje dovijeka. Ta pak riječ jest evanđelje koje vam je naviješteno.
25Lakini neno la Bwana hudumu milele." Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu.