1De sada, bogataši, proplačite i zakukajte zbog nevolja koje će vas zadesiti!
1Na sasa sikilizeni enyi matajiri! Lieni na kuomboleza kwa sababu ya taabu zitakazowajieni.
2Bogatstvo vam istrunu, haljine vaše postadoše hrana moljcima,
2Mali zenu zimeoza, na nguo zenu zimeliwa na nondo.
3zlato vam i srebro zarđa i rđa će njihova biti svjedočanstvo protiv vas te će kao vatra izjesti tijela vaša! Zgrnuste blago u posljednje dane!
3Dhahabu yenu na fedha vimeota kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu, nayo itakula miili yenu kama vile moto. Ninyi mmejilundikia mali katika siku hizi za mwisho!
4Evo: plaća kosaca vaših njiva - koju im uskratiste - viče i vapaji žetelaca dopriješe do ušiju Gospoda nad Vojskama.
4Hamkuwalipa mishahara watumishi waliofanya kazi katika mashamba yenu. Sikilizeni malalamiko yao! Kilio cha hao wanaovuna mashamba yenu kimefika masikioni mwa Bwana, Mwenye Nguvu.
5Raskošno ste na zemlji i razvratno živjeli, utoviste srca svoja za dan klanja!
5Mmeishi duniani maisha ya kujifurahisha na ya anasa. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa.
6Osudiste i ubiste pravednika: on vam se ne suprotstavlja!
6Mmemhukumu na kumwua mtu asiye na hatia, naye hakuwapigeni.
7Strpite se dakle, braćo, do Dolaska Gospodnjega! Evo: ratar iščekuje dragocjeni urod zemlje, strpljiv je s njime dok ne dobije kišu ranu i kasnu.
7Basi, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapokuja. Tazameni mkulima anavyongoja kwa subira mimea yake itoe mavuno mazuri. Yeye hungojea kwa subira mvua za masika na za vuli.
8Strpite se i vi, očvrsnite srca jer se Dolazak Gospodnji približio!
8Nanyi pia mnapaswa kuwa na subira; imarisheni mioyo yenu, maana siku ya kuja kwake Bwana inakaribia.
9Ne tužite se jedni na druge da ne budete osuđeni! Evo: sudac stoji pred vratima!
9Ndugu zangu, msinung'unikiane ninyi kwa ninyi msije mkahukumiwa na Mungu. Hakimu yu karibu, tayari kuingia.
10Za uzor strpljivosti i podnošenja zala uzmite, braćo, proroke koji su govorili u ime Gospodnje.
10Ndugu, mkitaka kuona mfano wa subira na uvumilivu katika mateso, fikirini juu ya manabii ambao walinena kwa jina la Bwana.
11Eto: blaženima nazivamo one koji ustrajaše. Za postojanost Jobovu čuste i nakanu Gospodnju vidjeste jer milostiv je Gospodin i milosrdan!
11Tunawaita hao wenye heri kwa sababu walivumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wa Yobu, na mnajua jinsi Bwana alivyomtendea mwishoni. Maana Bwana amejaa huruma na rehema.
12Prije svega, braćo moja, ne zaklinjite se ni nebom ni zemljom, ni ikojom drugom zakletvom. Vaše "da" neka bude "da", i "ne" - "ne", da ne padnete pod sud.
12Zaidi ya hayo yote, ndugu zangu, msiape kwa mbingu, wala kwa dunia, wala kwa kitu kingine chochote. Semeni "Ndiyo" kama maana yenu ni ndiyo, na "La" kama maana yenu ni la, na hapo hamtahukumiwa na Mungu.
13Pati li tko među vama? Neka moli! Je li tko radostan? Neka pjeva hvalospjeve!
13Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa.
14Boluje li tko među vama? Neka dozove starješine Crkve! Oni neka mole nad njim mažući ga uljem u ime Gospodnje
14Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
15pa će molitva vjere spasiti nemoćnika; Gospodin će ga podići, i ako je sagriješio, oprostit će mu se.
15Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.
16Ispovijedajte dakle jedni drugima grijehe i molite jedni za druge da ozdravite! Mnogo može žarka molitva pravednikova.
16Basi, ungamanianeni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.
17Ilija bijaše čovjek baš kao i mi; usrdno se pomoli da ne bude kiše i kiše nije bilo na zemlji tri godine i šest mjeseci.
17Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo mvua isinyeshe, nayo haikunyesha nchini kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18Zatim se ponovno pomoli te nebo dade kišu i zemlja iznese urod svoj.
18Kisha akaomba tena, mvua ikanyesha kutoka angani na nchi ikatoa mazao yake.
19Braćo moja, odluta li tko od vas od istine pa ga tkogod vrati,
19Ndugu zangu, mmoja wenu akipotoka kuhusu ukweli, na mwingine akamrudisha,
20znajte: tko vrati grešnika s lutalačkog puta njegova, spasit će dušu njegovu od smrti i pokriti mnoštvo grijeha.
20fahamuni kwamba, huyo anayemrudisha mwenye dhambi kutoka njia yake ya upotovu, ataiokoa roho yake kutoka kifo, na dhambi nyingi zitaondolewa.