Croatian

Swahili: New Testament

2 Corinthians

11

1O kad biste podnijeli nešto malo bezumlja mojega! Da, podnesite me!
1Laiti mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni kidogo.
2Ljubomoran sam doista na vas Božjim ljubomorom: ta zaručih vas s jednim mužem, kao čistu djevicu privedoh vas Kristu.
2Ninawaoneeni wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
3Ali se bojim da se - kao što zmija zavede Evu svojom lukavštinom - misli vaše ne pokvare i odmetnu od iskrenosti prema Kristu.
3Lakini naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa, fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
4Uistinu, ako tko dođe i propovijeda drugog Isusa, kojega mi nismo propovijedali - ili ako drugoga Duha primate, kojega niste primili; ili drugo evanđelje, koje niste prigrlili - takva lijepo podnosÄite.
4Maana mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa na ile mliyopokea kutoka kwetu!
5Smatram, eto, da ni u čemu nisam manji od "nadapostola".
5Sidhani kwamba mimi ni mdogo kuliko hao "mitume wakuu."
6Jer ako sam i nevješt u govoru, nisam u znanju; naprotiv, u svemu vam ga i pred svima očitovasmo.
6Labda sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi kwenu, kila mahali na kila wakati.
7Ili sam grijeh počinio što sam vam - ponizujući sebe da se vi uzvisite - besplatno navješćivao Božje evanđelje?
7Mimi niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
8Druge sam crkve plijenio, od njih primao potporu da bih mogao vama služiti. I dok bijah u vas, premda u oskudici, nikomu nisam bio na teret.
8Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine. Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
9U oskudici su mi pomogla braća koja dođoše iz Makedonije. U svemu sam se čuvao da vam ne budem težak, a i čuvat ću se.
9Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
10Istine mi Kristove u meni, ove mi hvale nitko neće oduzeti u ahajskim krajevima.
10Naahidi kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
11Zašto? Jer vas ne ljubim? Bog znade!
11Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba nawapenda!
12A što činim, i dalje ću činiti da izbijem izliku onima koji izliku traže ne bi li se s nama izjednačili u onom čime se hvastaju.
12Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
13Jer takvi su ljudi lažni apostoli, himbeni radnici, prerušuju se u apostole Kristove.
13Maana, hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa Kristo.
14I nikakvo čudo! Ta sam se Sotona prerušuje u anđela svjetla.
14Wala si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
15Ništa osobito dakle ako se i službenici njegovi prerušuju u službenike pravednosti. Svršetak će im biti po djelima njihovim.
15Kwa hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo yao.
16Opet velim: da me tko ne bi smatrao bezumnim! Uostalom, primite me makar i kao bezumna da se i ja nešto malo pohvalim.
16Tena nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi, nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
17Što govorim, ne govorim po Gospodnju, nego kao u bezumlju, u ovoj hvalisavoj smionosti.
17Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna, nasema tu kama mtu mpumbavu.
18Budući da se mnogi hvale po ljudsku, i ja ću se hvaliti.
18Maadam wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
19Ta rado podnosÄite bezumne, vi umni!
19Ninyi ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
20Da, podnosÄite ako vas tko zarobljava, ako vas tko proždire, ako tko otima, ako se tko uznosi, ako vas tko po obrazu bije.
20Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
21Na sramotu govorim: bili smo, biva, slabi! Ipak, čime se god tko osmjeljuje - u bezumlju govorim - osmjeljujem se i ja!
21Kwa aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu yeyote anayethubutu kujivunia kitu--nasema kama mtu mpumbavu--mimi nathubutu pia.
22Hebreji su? I ja sam! Izraelci su? I ja sam! Potomstvo su Abrahamovo? I ja sam!
22Je, wao ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa Abrahamu? Hata mimi.
23Poslužitelji su Kristovi? Kao mahnit govorim: ja još više! U naporima - preobilno; u tamnicama - preobilno; u batinama - prekomjerno; u smrtnim pogiblima - često.
23Wao ni watumishi wa Kristo? Hata mimi--nanena hayo kiwazimu--ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
24Od Židova primio sam pet puta po četrdeset manje jednu.
24Mara tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
25Triput sam bio šiban, jednom kamenovan, triput doživio brodolom, jednu noć i dan proveo sam u bezdanu.
25Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
26Česta putovanja, pogibli od rijeka, pogibli od razbojnika, pogibli od sunarodnjaka, pogibli od pogana, pogibli u gradu, pogibli u pustinji, pogibli na moru, pogibli od lažne braće;
26Kila mara safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama; hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine; hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu wa uongo
27u trudu i naporu, često u nespavanju, u gladu i žeđi, često u postovima, u studeni i golotinji!
27Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
28Osim toga, uz drugo, salijetanje svakodnevno, briga za sve crkve.
28Na, licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
29Tko je slab, a ja da ne budem slab? Tko se sablažnjuje, a ja da ne izgaram?
29Kama mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa na wasiwasi.
30Treba li se hvaliti, svojom ću se slabošću hvaliti.
30Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
31Bog i Otac Gospodina Isusa, blagoslovljen u vijeke, zna da ne lažem.
31Mungu na Baba wa Bwana Yesu--jina lake litukuzwe milele--yeye anajua kwamba sisemi uongo.
32U Damasku namjesnik kralja Arete čuvaše grad damaščanski hoteći me uhvatiti.
32Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
33Ali kroz prozor spustiše me u košari preko zida te umakoh njegovim rukama.
33Lakini, ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani, nikachopoka mikononi mwake.