1Hvaliti se treba? Ne koristi doduše ali - dolazim na viđenje i objave Gospodnje.
1Nitajivuna basi, ingawa haifai! Lakini sasa nitasema juu ya maono na ufunuo alivyonijalia Bwana.
2Znam čovjeka u Kristu: prije četrnaest godina - da li u tijelu, ne znam; da li izvan tijela, ne znam, Bog zna - taj je bio ponesen do trećeg neba.
2Namjua mtu mmoja Mkristo, ambaye miaka kumi na minne iliyopita alinyakuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
3I znam da je taj čovjek - da li u tijelu, da li izvan tijela, ne znam, Bog zna -
3Narudia: najua kwamba mtu huyo alinyakuliwa mpaka peponi. (Lakini sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
4bio ponesen u raj i čuo neizrecive riječi, kojih čovjek ne smije govoriti.
4Huko akasikia mambo ya siri ambayo binadamu hastahili kuyatamka.
5Time ću se hvaliti, a samim se sobom neću hvaliti osim slabostima svojim.
5Basi, nitajivunia juu ya mtu wa namna hiyo, na si juu yangu mimi binafsi, isipokuwa tu juu ya udhaifu wangu.
6Uistinu, kad bih se i htio hvaliti, ne bih bio bezuman; istinu bih govorio. Ali se uzdržavam da ne bi tko mislio o meni više nego što vidi na meni ili što čuje od mene.
6Kama ningetaka kujivuna singekuwa mpumbavu hata kidogo, maana ningekuwa nasema ukweli mtupu. Lakini sitajivuna; sipendi mtu anifikirie zaidi ya vile anavyoona na kusikia kutoka kwangu.
7I da se zbog uzvišenosti objava ne bih uzoholio, dan mi je trn u tijelu, anđeo Sotonin, da me udara da se ne uzoholim.
7Lakini, kusudi mambo haya makuu niliyofunuliwa yasinifanye nilewe majivuno, nilipewa maumivu mwilini kama mwiba, mjumbe wa Shetani mwenye kunipiga nisijivune kupita kiasi.
8Za to sam triput molio Gospodina, da odstupi od mene. A on mi reče:
8Nilimsihi Bwana mara tatu kuhusu jambo hili ili linitoke.
9"Dosta ti je moja milost jer snaga se u slabosti usavršuje." Najradije ću se dakle još više hvaliti svojim slabostima da se nastani u meni snaga Kristova.
9Lakini akaniambia: "Neema yangu inatosha kwa ajili yako; maana uwezo wangu hukamilishwa zaidi katika udhaifu." Basi, ni radhi kabisa kujivunia udhaifu wangu ili uwezo wake Kristo ukae juu yangu.
10Zato uživam u slabostima, uvredama, poteškoćama, progonstvima, tjeskobama poradi Krista. Jer kad sam slab, onda sam jak.
10Kwa hiyo nakubali kwa radhi udhaifu, madharau, taabu, udhalimu na mateso, kwa ajili ya Kristo; maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.
11Postao sam bezuman! Vi me natjeraste. Ta trebalo je da me vi preporučite jer ni u čemu nisam manji od "nadapostola", premda nisam ništa.
11Nimekuwa kama mpumbavu, lakini, ninyi mmenilazimisha kuwa hivyo. Ninyi ndio mngalipaswa kunisifu. Maana, ingawa mimi si kitu, kwa vyovyote, mimi si mdogo zaidi kuliko hao "mitume wakuu."
12Znamenja apostolstva moga ostvarena su među vama u posvemašnjoj postojanosti: znakovima i čudesima i silnim djelima.
12Miujiza na maajabu yaonyeshayo wazi kwamba mimi ni mtume yalifanyika miongoni mwenu kwa uvumilivu wote.
13Ta u čemu ste to manji od drugih crkava, osim što vam ja nisam bio na teret? Oprostite mi ovu "nepravdu".
13Je, mlipungukiwa nini zaidi kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi kwa upande wangu sikuwasumbueni kupata msaada wenu? Samahani kwa kuwakoseeni haki hiyo!
14Evo, spremam se treći put doći k vama i neću vam biti na teret jer ne ištem vaše, nego vas. Djeca doista nisu dužna stjecati roditeljima, nego roditelji djeci.
14Sasa niko tayari kabisa kuja kwenu mara ya tatu, na sitawasumbua. Maana ninachotafuta si mali zenu, bali ni ninyi wenyewe. Ni kawaida ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba, na si watoto kuwawekea wazazi wao.
15A ja ću najradije trošiti i istrošiti se za duše vaše. Ako vas više ljubim, zar da budem manje ljubljen?
15Mimi ni radhi kabisa kutumia nilicho nacho, na hata kujitolea mimi mwenyewe kabisa, kwa faida ya roho zenu. Je, mtanipenda kidogo ati kwa kuwa mimi nawapenda ninyi mno?
16Ali neka! Ja vas nisam opterećivao, nego, "lukav" kako jesam, "na prijevaru vas uhvatih".
16Basi, mtakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu. Lakini labda mtu mwingine atasema: "Kwa vile Paulo ni mwerevu, amewafanyieni ulaghai."
17Da vas možda nisam zakinuo po kome od onih koje poslah k vama?
17Je, mimi niliwanyonyeni kwa njia ya mjumbe yeyote niliyemtuma kwenu?
18Zamolio sam Tita i poslao s njime brata. Da vas možda Tit nije u čemu zakinuo? Zar nismo hodili u istom duhu? I istim stopama?
18Mimi nilimwita Tito, nikamtuma kwenu na ndugu yetu mwingine. Je, Tito aliwanyonyeni? Je, hamjui kwamba sisi tumekuwa tukiongozwa na roho yuleyule, na mwenendo wetu ni mmoja?
19Odavna smatrate da se pred vama branimo. Pred Bogom u Kristu govorimo: sve je to, ljubljeni, za vaše izgrađivanje.
19Labda mnafikiri kwamba mpaka sasa tumekuwa tukijitetea wenyewe mbele yenu! Lakini, tunasema mambo haya mbele ya Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo. Mambo hayo, yote, wapenzi wangu, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
20Bojim se doista da vas kada dođem, možda neću naći kakve bih htio i da ćete vi mene naći kakva ne biste htjeli: da ne bi možda bilo svađa, zavisti, žestina, spletkarenja, klevetanja, došaptavanja, nadimanja, buna;
20Naogopa, huenda nitakapokuja kwenu nitawakuta katika hali nisiyopenda, nami itanilazimu kuwa katika hali msiyoipenda. Naogopa huenda kukawa na ugomvi, wivu, uhasama, ubishi, masengenyano, kunong'ona, majivuno na fujo kati yenu.
21da me opet kada dođem, ne bi ponizio Bog moj kod vas kako ne bih morao oplakivati mnoge koji su prije sagriješili, a nisu se pokajali za nečistoću i bludnost i razvratnost koju počiniše.
21Naogopa huenda hapo nitakapokuja safari ijayo Mungu wangu atanifanya niaibike mbele yenu, nami nitaomboleza kwa ajili ya wengi wa wale waliotenda dhambi lakini hawakujutia huo uchafu, tamaa zao mbaya na uzinzi waliokuwa wamefanya.