1Zato, budući da po milosrđu imamo ovu službu, ne malakšemo.
1Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.
2Ali odrekosmo se sramotnoga prikrivanja: ne nastupamo lukavo niti izopačujemo riječ Božju, nego se objavljivanjem istine preporučujemo svakoj savjesti ljudskoj pred Bogom.
2Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali tunaudhihirisha ukweli kwa kuufanya ukweli, na hivyo kujiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.
3Ako je i zastrto evanđelje naše, u onima je zastrto koji propadaju:
3Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.
4u onima kojima bog ovoga svijeta oslijepi pameti nevjerničke da ne zasvijetli svjetlost evanđelja slave Krista koji je slika Božja.
4Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu.
5Jer ne propovijedamo same sebe, nego Krista Isusa Gospodinom, a sebe slugama vašim poradi Isusa.
5Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
6Ta Bog koji reče: Neka iz tame svjetlost zasine!, on zasvijetli u srcima našim da nam spoznanje slave Božje zasvijetli na licu Kristovu.
6Mungu ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao katika uso wa Kristo.
7To pak blago imamo u glinenim posudama da izvanredna ona snaga bude očito Božja, a ne od nas.
7Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.
8U svemu pritisnuti, ali ne pritiješnjeni; dvoumeći, ali ne zdvajajući;
8Daima twapata taabu, lakini hatugandamizwi; twapata mashaka, lakini hatukati tamaa;
9progonjeni, ali ne napušteni; obarani, ali ne oboreni -
9twateseka, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.
10uvijek umiranje Isusovo u tijelu pronosimo da se i život Isusov u tijelu našem očituje.
10Kila wakati tumekuwa tukichukua mwilini mwetu kifo cha Kristo, ili uhai wake Yesu pia udhihirike katika miili yetu.
11Doista, mi se živi uvijek na smrt predajemo poradi Isusa da se i život Isusov očituje u našem smrtnom tijelu.
11Naam, katika maisha yetu yote tunakabiliwa na kifo daima kwa ajili ya Yesu, ili uzima wake Yesu udhihirike katika miili yetu inayokufa.
12Tako smrt djeluje u nama, život u vama.
12Hii ina maana kwamba ndani yetu kifo kinafanya kazi, lakini ndani yenu uhai unafanya kazi.
13A budući da imamo isti duh vjere kao što je pisano: Uzvjerovah, zato besjedim, i mi vjerujemo pa zato i besjedimo.
13Maandiko Matakatifu yasema: "Niliamini, ndiyo maana nilinena." Nasi pia, tukiwa na moyo huohuo wa imani, tunaamini, na kwa sababu hiyo twanena.
14Ta znamo: onaj koji je uskrisio Gospodina Isusa i nas će s Isusom uskrisiti i zajedno s vama uza se postaviti.
14Tunajua kwamba yule aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.
15A sve je to za vas: da milost - umnožena - zahvaljivanjem mnogih izobiluje Bogu na slavu.
15Yote haya ni kwa faida yenu; ili kama vile neema ya Mungu inavyoenea kwa watu wengi zaidi na zaidi vivyo hivyo watu wengi zaidi watoe shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
16Zato ne malakšemo. Naprotiv, ako se naš izvanji čovjek i raspada, nutarnji se iz dana u dan obnavlja.
16Kwa sababu hiyo hatufi moyo; na hata kama maumbile yetu ya nje yataoza, lakini kwa ndani tunafanywa wapya siku kwa siku.
17Ta ova malenkost naše časovite nevolje donosi nam obilato, sve obilatije, breme vječne slave
17Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho.
18jer nama nije do vidljivog nego do nevidljivog: ta vidljivo je privremeno, a nevidljivo - vječno.
18Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele.