1Znamo doista: ako se razruši naš zemaljski dom, šator, imamo zdanje od Boga, dom nerukotvoren, vječan na nebesima.
1Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono.
2U ovome doista stenjemo i čeznemo da se povrh njega zaodjenemo svojim nebeskim obitavalištem;
2Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
3dakako, ako se nađemo obučeni, ne goli.
3Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
4Da, i mi koji smo u ovom šatoru, stenjemo opterećeni jer nećemo da budemo svučeni, nego da se još obučemo da život iskapi što je smrtno.
4Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
5A zato nas je sazdao Bog - on koji nam dade zalog Duha.
5Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
6Uvijek smo stoga puni pouzdanja makar i znamo: naseljeni u tijelu, iseljeni smo od Gospodina.
6Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
7Ta u vjeri hodimo, ne u gledanju.
7Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
8Da, puni smo pouzdanja i najradije bismo se iselili iz tijela i naselili kod Gospodina.
8Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
9Zato se i trsimo da mu omilimo, bilo naseljeni, bilo iseljeni.
9Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
10Jer svima nam se pojaviti pred sudištem Kristovim da svaki dobije što je kroz tijelo zaradio, bilo dobro, bilo zlo.
10Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
11Prožeti dakle strahom Gospodnjim uvjeravamo ljude; razotkriveni smo Bogu, a nadam se - i vašim savjestima.
11Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
12Ne preporučujemo vam opet sami sebe, nego vam dajemo prigodu ponositi se nama, da imate odgovor za one koji se diče licem, a ne srcem.
12Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
13Doista, ako bijasmo "izvan sebe" - Bogu bijasmo; ako li "pri sebi" - vama bijasmo.
13Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
14Jer ljubav nas Kristova obuzima kad promatramo ovo: jedan za sve umrije, svi dakle umriješe;
14Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
15i za sve umrije da oni koji žive ne žive više sebi, nego onomu koji za njih umrije i uskrsnu.
15Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
16Stoga mi od sada nikoga ne poznajemo po tijelu; ako smo i poznavali po tijelu Krista, sada ga tako više ne poznajemo.
16Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
17Dakle, je li tko u Kristu, nov je stvor. Staro uminu, novo, gle, nasta!
17Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
18A sve je od Boga koji nas sa sobom pomiri po Kristu i povjeri nam službu pomirenja.
18Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
19Jer Bog je u Kristu svijet sa sobom pomirio ne ubrajajući im opačina njihovih i polažući u nas riječ pomirenja.
19Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
20Kristovi smo dakle poslanici; Bog vas po nama nagovara. Umjesto Krista zaklinjemo: dajte, pomirite se s Bogom!
20Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
21Njega koji ne okusi grijeha Bog za nas grijehom učini da mi budemo pravednost Božja u njemu.
21Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.