1Kao suradnici opominjemo vas da ne primite uzalud milosti Božje.
1Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
2Jer on veli: U vrijeme milosti usliših te i u dan spasa pomogoh ti. Evo sad je vrijeme milosno, evo sad je vrijeme spasa.
2Mungu asema hivi: "Wakati wa kufaa nimekusikiliza, wakati wa wokovu nikakusaidia." Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!
3Ni u čemu ne dajemo nikakve sablazni da se ne kudi ova služba,
3Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuio chochote.
4nego se u svemu iskazujemo kao poslužitelji Božji: velikom postojanošću u nevoljama, u potrebama, u tjeskobama,
4Badala yake, tunajionyesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.
5pod udarcima, u tamnicama, u bunama, u naporima, u bdjenjima, u postovima,
5Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.
6u čistoći, u spoznanju, u velikodušnosti, u dobroti, u Duhu Svetomu, u ljubavi nehinjenoj,
6Tunajionyesha kuwa watumishi wa Mungu kwa usafi wa moyo, elimu, uvumilivu na wema; kwa Roho Mtakatifu, kwa upendo usio na unafiki,
7u riječi istinitoj, u snazi Božjoj; oružjem pravde zdesna i slijeva;
7kwa ujumbe wa kweli na kwa nguvu ya Mungu. Uadilifu ndiyo silaha yetu upande wa kulia na upande wa kushoto.
8slavom i sramotom; zlim i dobrim glasom; kao zavodnici, a istiniti;
8Tuko tayari kupata heshima na kudharauliwa, kulaumiwa na kusifiwa. Twadhaniwa kuwa waongo, kumbe twasema kweli;
9kao nepoznati, a poznati; kao umirući, a evo živimo; kao kažnjeni, a ne ubijeni;
9kama wasiojulikana, kumbe twajulikana kwa wote, kama waliokufa, lakini mwonavyo, sisi ni wazima kabisa.
10kao žalosni, a uvijek radosni; kao siromašni, a mnoge obogaćujemo; kao oni koji ništa nemaju, a sve posjeduju.
10Ingawa tumeadhibiwa, hatukuuawa; ingawa tunayo huzuni, twafurahi daima; ingawa tu maskini hohehahe, lakini twatajirisha watu wengi; twaonekana kuwa watu tusio na chochote, kumbe tuna kila kitu.
11Usta su naša otvorena vama, Korinćani, srce naše rašireno.
11Ndugu Wakorintho, tumezungumza nanyi kwa unyofu; mioyo yetu iko wazi kabisa.
12Nije vam tijesno u nama, ali je tijesno u vašim grudima.
12Kama mnaona kuna kizuizi chochote kile, kizuizi hicho kiko kwenu ninyi wenyewe, na si kwa upande wetu.
13Za uzdarje - kao djeci govorim - raširite se i vi.
13Sasa nasema nanyi kama watoto wangu, wekeni mioyo yenu wazi kama nasi tulivyofanya.
14Ne ujarmljujte se s nevjernicima. Ta što ima pravednost s bezakonjem? Ili kakvo zajedništvo svjetlo s tamom?
14Msiambatane na watu wasioamini. Je, wema na uovu vyapatana kweli? Mwanga na giza vyawezaje kukaa pamoja?
15Kakvu slogu Krist s Belijarom? Ili kakav dio vjernik s nevjernikom?
15Kristo anawezaje kupatana na Shetani? Muumini ana uhusiano gani na asiyeamini?
16Kakav sporazum hram Božji s idolima? Jer mi smo hram Boga živoga, kao što reče Bog: Prebivat ću u njima i hoditi među njima; i bit ću Bog njihov, a oni narod moj.
16Hekalu la Mungu lina uhusiano gani na sanamu za uongo? Maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu mwenyewe alivyosema: "Nitafanya makao yangu kwao, na kuishi kati yao; Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu."
17Zato iziđite iz njihove sredine i odvojite se, govori Gospodin, i ništa nečisto ne dotičite i ja ću vas primiti.
17Kwa hiyo Bwana asema pia: "Ondokeni kati yao, mkajitenge nao, msiguse kitu najisi, nami nitawapokea.
18I bit ću vam otac i vi ćete mi biti sinovi i kćeri, veli Gospodin Svemogući.
18Mimi nitakuwa Baba yenu, nanyi mtakuwa watoto wangu, waume kwa wake, asema Bwana Mwenye Uwezo."