Croatian

Swahili: New Testament

2 Thessalonians

3

1Uostalom, molite, braćo, za nas da riječ Gospodnja trči i proslavlja se kao i u vas
1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2i da se oslobodimo nezgodnih i opakih ljudi. Jer nemaju svi vjere!
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3Ali, vjeran je Gospodin koji će nas učvrstiti i sačuvati od Zloga.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4A uzdamo se, u Gospodinu, u vas: da vršite i da ćete vršiti ono što vam zapovijedamo.
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5A Gospodin neka upravi srca vaša k ljubavi Božjoj i postojanosti Kristovoj.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6Zapovijedamo vam, braćo, u ime Gospodina Isusa Krista da se klonite svakoga brata što živi neuredno i ne po predaji koju primiste od nas.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7Ta sami znate kako nas treba nasljedovati. Jer dok bijasmo među vama, nismo živjeli neuredno:
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8ničiji kruh nismo badava jeli, nego smo u trudu i naporu noću i danju radili da ne bismo opteretili koga od vas.
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9Ne što ne bismo imali prava, nego da vam sebe damo za uzor koji ćete nasljedovati.
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10Doista, dok bijasmo u vas, ovo vam zapovijedasmo: Tko neće da radi, neka i ne jede!
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
11A čujemo da neki od vas žive neuredno: ništa ne rade, nego dangube.
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12Takvima zapovijedamo i zaklinjemo ih u Gospodinu Isusu Kristu: neka s mirom rade i svoj kruh jedu.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13Vama pak, braćo, neka ne dodija činiti dobro.
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14Ako li se tko ne pokorava našoj riječi u ovoj poslanici, zabilježite ga, ne drugujte s njime, da se postidi,
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15ali ga ne smatrajte neprijateljem, nego ga urazumljujte kao brata.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16A sam Gospodin mira dao vam mir zauvijek i na svaki način! Gospodin sa svima vama!
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17Pozdrav mojom rukom, Pavlovom. Ovo je znak u svakoj poslanici: ovako pišem.
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18Milost Gospodina našega Isusa Krista sa svima vama!
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.