1Radi toga ja, Pavao, sužanj Krista Isusa za vas pogane...
1Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
2Zacijelo ste čuli za rasporedbu milosti Božje koja mi je dana za vas:
2Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
3objavom mi je obznanjeno otajstvo, kako netom ukratko opisah.
3Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
4Čitajući to, možete dokučiti kako ja shvaćam Kristovo otajstvo,
4nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
5koje nije bilo obznanjeno sinovima ljudskim drugih naraštaja. Ono je sada u Duhu objavljeno svetim njegovim apostolima i prorocima:
5Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
6da su pogani subaštinici i "sutijelo" i sudionici obećanja u Kristu Isusu - po evanđelju,
6Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
7kojega postadoh poslužiteljem darom milosti Božje koja mi je dana djelotvornošću snage njegove.
7Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
8Meni, najmanjemu od svih svetih, dana je ova milost: poganima biti blagovjesnikom neistraživog bogatstva Kristova
8Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
9i osvijetliti rasporedbu otajstva, pred vjekovima skrivena u Bogu, koji sve stvori,
9tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele,
10da sada - po Crkvi - Vrhovništvima i Vlastima na nebesima bude obznanjena mnogolika mudrost Božja
10kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
11zasnovana - po naumu o vjekovima - u Kristu Isusu Gospodinu našemu.
11Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
12U njemu, s pouzdanjem po vjeri u njega, imamo slobodan pristup.
12Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
13Zato ne klonite, molim, s nevolja mojih za vas! One su slava vaša!
13Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
14Zato prigibam koljena pred Ocem,
14Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
15od koga ime svakom očinstvu na nebu i na zemlji:
15aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
16neka vam dadne po bogatstvu Slave svoje ojačati se po Duhu njegovu u snazi za unutarnjeg čovjeka
16Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
17da po vjeri Krist prebiva u srcima vašim te u ljubavi ukorijenjeni i utemeljeni
17naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
18mognete shvatiti sa svima svetima što je Dužina i Širina i Visina i Dubina
18kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
19te spoznati nadspoznatljivu ljubav Kristovu da se ispunite do sve Punine Božje.
19Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
20Onomu pak koji snagom u nama djelatnom može učiniti mnogo izobilnije nego li mi moliti ili zamisliti -
20Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
21Njemu slava u Crkvi i u Kristu Isusu za sva pokoljenja vijeka vjekovječnoga! Amen.
21kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina.