1Budite dakle nasljedovatelji Božji kao djeca ljubljena
1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
2i hodite u ljubavi kao što je i Krist ljubio vas i sebe predao za nas kao prinos i žrtvu Bogu na ugodan miris.
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
3A bludnost i svaka nečistoća ili pohlepa neka se i ne spominje među vama, kako dolikuje svetima!
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
4Ni prostota, ni ludorija, ni dvosmislica, što se ne priliči, nego radije zahvaljivanje!
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
5Jer dobro znajte ovo: nijedan bludnik, ili bestidnik, ili pohlepnik - taj idolopoklonik - nema baštine u kraljevstvu Kristovu i Božjemu.
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
6Nitko neka vas ispraznim riječima ne zavarava: zbog toga dolazi gnjev Božji na sinove neposlušne.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
7Nemajte dakle ništa s njima!
7Basi, msishirikiane nao.
8Da, nekoć bijaste tama, a sada ste svjetlost u Gospodinu: kao djeca svjetlosti hodite -
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
9plod je svjetlosti svaka dobrota, pravednost i istina -
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
10i odlučite se za ono što je milo Gospodinu.
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
11A nemajte udjela u jalovim djelima tame, nego ih dapače raskrinkavajte,
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
12jer što potajno čine, sramota je i govoriti.
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
13A sve što se raskrinka, pod svjetlošću postaje sjajno; što je pak sjajno, svjetlost je.
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
14Zato veli: "Probudi se, ti što spavaš, ustani od mrtvih i zasvijetljet će ti Krist."
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
15Razmotrite dakle pomno kako živite! Ne kao ludi, nego kao mudri!
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
16Iskupljujte vrijeme jer dani su zli!
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
17Zato ne budite nerazumni, nego shvatite što je volja Gospodnja!
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
18I ne opijajte se vinom u kojem je razuzdanost, nego - punite se Duhom!
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
19Razgovarajte među sobom psalmima, hvalospjevima i duhovnim pjesmama! Pjevajte i slavite Gospodina u svom srcu!
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
20Svagda i za sve zahvaljujte Bogu i Ocu u imenu Gospodina našega Isusa Krista!
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21Podložni budite jedni drugima u strahu Kristovu!
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
22Žene svojim muževima kao Gospodinu!
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
23Jer muž je glava žene kao i Krist Glava Crkve - On, Spasitelj Tijela.
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
24Pa kao što se Crkva podlaže Kristu, tako i žene muževima u svemu!
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
25Muževi, ljubite svoje žene kao što je Krist ljubio Crkvu te sebe predao za nju
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
26da je posveti, očistivši je kupelji vode uz riječ
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
27te sebi predvede Crkvu slavnu, bez ljage i nabora ili čega takva, nego da bude sveta i bez mane.
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
28Tako treba da i muževi ljube svoje žene kao svoja tijela. Tko ljubi svoju ženu, sebe ljubi.
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
29Ta nitko nikada ne mrzi svoga tijela, nego ga hrani i njeguje kao i Krist Crkvu.
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
30Doista, mi smo udovi njegova Tijela!
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
31Stoga će čovjek ostaviti oca i majku da prione uza svoju ženu; dvoje njih bit će jedno tijelo.
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
32Otajstvo je to veliko! Ja smjeram na Krista i na Crkvu.
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
33Dakle, neka svaki od vas ljubi svoju ženu kao samog sebe, a žena neka poštuje svog muža.
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.