1Djeco, slušajte svoje roditelje u Gospodinu jer to je pravedno.
1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2Poštuj oca svoga i majku - to je prva zapovijed s obećanjem:
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3da ti dobro bude i da dugo živiš na zemlji.
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
4A vi, očevi, ne srdite djece svoje, nego ih odgajajte stegom i urazumljivanjem Gospodnjim!
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5Robovi, slušajte svoje zemaljske gospodare kao Krista - sa strahom i trepetom, u jednostavnosti srca.
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6Ne naoko, kao oni koji se ulaguju ljudima, nego kao sluge Kristove koje zdušno vrše volju Božju;
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7dragovoljno služe - kao Gospodinu, a ne ljudima,
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8znajući da će svatko, bio on rob ili slobodnjak, učini li što dobro, za to dobiti plaću od Gospodina.
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9I vi, gospodari, isto se tako vladajte prema njima: kanite se prijetnje, znajući da je i njihov i vaš Gospodar na nebesima i da u njega nema pristranosti.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10Ubuduće jačajte se u Gospodinu i u silnoj snazi njegovoj.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11Obucite svu opremu Božju da se mognete oduprijeti lukavstvima đavlovim.
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12Jer nije nam se boriti protiv krvi i mesa, nego protiv Vrhovništava, protiv Vlasti, protiv upravljača ovoga mračnoga svijeta, protiv zlih duhova po nebesima.
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
13Zbog toga posegnite za svom opremom Božjom da uzmognete odoljeti u dan zli i održati se kada sve nadvladate.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14Držite se dakle! Opašite bedra istinom, obucite oklop pravednosti,
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15potpašite noge spremnošću za evanđelje mira!
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16U svemu imajte uza se štit vjere: njime ćete moći ugasiti ognjene strijele Zloga.
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17Uzmite i kacigu spasenja i mač Duha, to jest Riječ Božju.
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18Svakovrsnom se molitvom i prošnjom u svakoj prigodi u Duhu molite. Poradi toga i bdijte sa svom ustrajnošću i molitvom za sve svete,
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19i za me, da mi se otvore usta i dade riječ hrabro obznaniti otajstvo evanđelja
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20kojeg sam poslanik u okovima, da se ohrabrim o njemu kako treba govoriti.
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21A da i vi znate što je sa mnom, kako mi je, o svemu će vas obavijestiti Tihik, ljubljeni brat i vjerni poslužitelj u Gospodinu.
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22Njega šaljem k vama baš zato da znate kako smo i da ohrabri srca vaša.
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23Mir braći i ljubav, s vjerom, od Boga Oca i Gospodina Isusa Krista!
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24Milost sa svima koji ljube Gospodina našega Isusa Krista - u neraspadljivosti.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.