1O bezumni Galaćani, tko li vas opčara? A pred očima vam je Isus Krist bio ocrtan kao Raspeti.
1Enyi Wagalatia, mmekuwa wajinga kweli! Ni nani aliyewaloga? Habari juu ya kusulubiwa kwake Yesu Kristo ilielezwa waziwazi mbele ya macho yenu.
2Ovo bih samo htio doznati od vas: jeste li primili Duha po djelima Zakona ili po vjeri u Poruku?
2Napenda kujua tu kitu kimoja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kutimiza matakwa ya Sheria ama kwa sababu ya kuisikia na kuiamini Habari Njema?
3Tako li ste bezumni? Započeli ste u Duhu pa da sada u tijelu dovršite?
3Je, mu wajinga kiasi hicho? Ninyi mlianza yote kwa msaada wa Roho je, mnataka sasa kumaliza kwa nguvu zenu wenyewe?
4Zar ste toliko toga uzalud doživjeli? A kad bi doista bilo uzalud!
4Je, mambo yale yote yaliyowapata ninyi yamekuwa bure tu? Haiwezekani!
5Onaj dakle koji vam daje Duha i čini među vama silna djela, čini li to zbog djela Zakona ili zbog vjere u Poruku?
5Je, Mungu huwajalia Roho na kutenda miujiza kati yenu ati kwa sababu mnatimiza yanayotakiwa na sheria, ama kwa sababu mnasikia Habari Njema na kuiamini?
6Tako Abraham povjerova Bogu i uračuna mu se u pravednost.
6Chukueni kwa mfano habari za Abrahamu: yeye alimwamini Mungu, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.
7Shvatite dakle: oni od vjere, to su sinovi Abrahamovi.
7Sasa basi jueni kwamba watu wenye kumwamini ndio walio watoto halisi wa Abrahamu.
8A Pismo, predvidjevši da Bog po vjeri opravdava pogane, unaprijed navijesti Abrahamu: U tebi će blagoslovljeni biti svi narodi.
8Maandiko Matakatifu yalionyesha kabla kwamba Mungu atawakubali watu wa mataifa kuwa waadilifu kwa njia ya imani. Hivyo Maandiko Matakatifu yalitangulia kumtangazia Abrahamu Habari Njema: "Katika wewe mataifa yote yatabarikiwa."
9Tako: oni od vjere blagoslivlju se s vjernikom Abrahamom.
9Basi, wale walio na imani wanabarikiwa pamoja na Abrahamu aliyeamini.
10Doista, koji su god od djela Zakona, pod prokletstvom su. Ta pisano je: Proklet tko se god ne drži i tko ne vrši svega što je napisano u Knjizi Zakona.
10Lakini wote wanaotegemea tu kutimiza yanayotakiwa na Sheria, wako chini ya laana. Maana, Maandiko Matakatifu yasema: "Yeyote asiyeshika na kutimiza yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria, yuko chini ya laana."
11A da se pred Bogom nitko ne opravdava Zakonom, očito je jer: Pravednik će od vjere živjeti.
11Ni dhahiri kwamba Sheria haiwezi kumfanya mtu akubaliwe kuwa mwadilifu; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
12Zakon pak nije od vjere, nego veli: Tko ga vrši, u njemu će naći život.
12Lakini Sheria haitegemei imani, ila Maandiko yasema: "Mwenye kutimiza yanayotakiwa na Sheria ataishi."
13Krist nas otkupi od prokletstva Zakona, postavši za nas prokletstvom - jer pisano je: Proklet je tko god visi na drvetu -
13Kristo alitukomboa kutoka katika laana ya Sheria kwa kujitwalia laana hiyo kwa ajili yetu; maana Maandiko yanasema: "Yeyote aliyetundikwa msalabani amelaaniwa."
14da u Kristu Isusu na pogane dođe blagoslov Abrahamov: da Obećanje, Duha, primimo po vjeri.
14Jambo hili lilifanyika kusudi ile baraka aliyopewa Abrahamu iwashukie watu wa mataifa mengine kwa njia ya Kristo, na ili kwa imani, tumpokee yule Roho ambaye Mungu alituahidia.
15Braćo, po ljudsku govorim: već i ljudski valjan savez nitko ne poništava niti mu što dodaje.
15Ndugu, nitawapeni mfano kutoka maisha yetu ya kila siku. Fikirini juu ya mkataba kati ya watu wawili. Mkataba ukisha fanyika na kutiwa sahihi hapana mtu anayeuweka kando au kuuongezea kitu.
16A ova su obećanja dana Abrahamu i potomstvu njegovu. Ne veli se: "i potomcima" kao o mnogima, nego kao o jednomu: I potomstvu tvojem, to jest Kristu.
16Basi, Abrahamu alipewa ahadi, yeye pamoja na mzawa wake. Maandiko hayasemi: "Na wazawa wake," yaani wengi, bali yasema, "Na mzawa wake," yaani mmoja, naye ndiye Kristo.
17Ovo hoću kazati: Saveza koji je Bog valjano sklopio ne obeskrepljuje Zakon, koji je nastao četiri stotine i trideset godina poslije, i ne dokida obećanja.
17Ninachotaka kusema ni hiki: Mungu alifanya agano lake akalithibitisha; Sheria ambayo ilitokea miaka mia nne na thelathini baadaye, haiwezi kulitangua hilo agano wala kuibatilisha hiyo ahadi.
18Doista, ako se baština zadobiva po Zakonu, ne zadobiva se po obećanju. A Abrahama je Bog po obećanju obdario.
18Maana, kama urithi ya Mungu inategemea Sheria, basi, haiwezi kutegemea tena ahadi ya Mungu. Kumbe, lakini Mungu alimkirimia Abrahamu kwa sababu aliahidi.
19Čemu onda Zakon? Dometnut je poradi prekršaja dok ne dođe potomstvo komu je namijenjeno obećanje; sastavljen je po anđelima preko posrednika.
19Ya nini basi, Sheria? Iliongezwa hapo ili kuonyesha uhalifu ni kitu gani, mpaka atakapokuja yule mzawa wa Abrahamu aliyepewa ile ahadi. Sheria ililetwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20Posrednika pak nema gdje je samo jedan. A Bog je jedan.
20Ama hakika, mpatanishi hahitajiwi ikiwa jambo lenyewe lamhusu mtu mmoja; na Mungu ni mmoja.
21Zar je dakle Zakon protiv obećanja Božjih? Nipošto! Jer da je dan Zakon koji bi mogao oživljavati, pravednost bi doista proizlazila iz Zakona.
21Je, Sheria inapingana na ahadi za Mungu? Hata kidogo! Maana, kama kungalitolewa sheria ambayo ingeweza kuwapa watu uzima, basi, tungeweza kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Sheria.
22Ali je Pismo sve zatvorilo pod grijeh da se, po vjeri u Isusa Krista, obećano dade onima koji vjeruju.
22Lakini sivyo; Maandiko Matakatifu yamekwisha sema kwamba ulimwengu wote upo chini ya utawala wa dhambi; na hivyo, kwa kumwamini Yesu Kristo, wenye kuamini watimiziwe ile ahadi.
23Prije dolaska vjere, pod Zakonom zatvoreni, bili smo čuvani za vjeru koja se imala objaviti.
23Kabla ya kujaliwa imani, Sheria ilitufanya wafungwa mpaka imani hiyo iliyokuwa inakuja ifunuliwe.
24Tako nam je Zakon bio nadzirateljem sve do Krista da se po vjeri opravdamo.
24Basi, hiyo Sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani, tukubaliwe kuwa waadilifu.
25A otkako je nadošla vjera, nismo više pod nadzirateljem.
25Tangu kufika kwa hiyo imani, Sheria si mlezi wetu tena.
26Uistinu, svi ste sinovi Božji, po vjeri u Kristu Isusu.
26Kwa njia ya imani, ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika kuungana na Kristo.
27Doista, koji ste god u Krista kršteni, Kristom se zaodjenuste.
27Ninyi nyote mliobatizwa mkaungana na Kristo ni kama vile mmemvaa Kristo.
28Nema više: Židov - Grk! Nema više: rob - slobodnjak! Nema više: muško - žensko! Svi ste vi Jedan u Kristu Isusu!
28Hivyo, hakuna tena tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki, mtumwa na mtu huru, mwanamume na mwanamke. Nyote ni kitu kimoja katika kuungana na Kristo Yesu.
29Ako li ste Kristovi, onda ste Abrahamovo potomstvo, baštinici po obećanju.
29Ikiwa ninyi ni wa Kristo, basi ni wazawa wa Abrahamu, na mtapokea yale aliyoahidi Mungu.